MKURUGENZI Mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI), Dkt. Diwani Msemo, amesema saratani ya shingo ya kizazi ndiyo inayoongoza kwa wanawake nchini Tanzania, ikiwa pia miongoni mwa saratani zinazochangia vifo kwa kiwango kikubwa. Dkt. Msemo amesema takribani asilimia 34 ya saratani zinazowapata wanawake nchini ni saratani ya shingo ya kizazi, akisisitiza kuwa hali hiyo inapaswa kuchukuliwa kwa uzito kutokana na ukweli kwamba ugonjwa huo unaweza kuzuilika na kugundulika mapema. Amesema saratani ya shingo ya kizazi inaweza kuzuilika kupitia chanjo, huku uchunguzi wa mara kwa mara ukisaidia kugundua mabadiliko ya awali na kutoa matibabu kabla ugonjwa haujawa mkubwa. “Ni saratani ambayo inaweza kuzuilika kwa chanjo, inaweza kugundulika mapema kupitia uchunguzi na inapogundulika katika hatua za awali, uwezekano wa kupona huwa mkubwa sana,” amesema Dkt. Msemo. Amesema hali hiyo inapaswa kuwa changamoto kwa jamii, kwa kuwa kuna wanawake wanaopoteza maisha kutokana na ugonjwa ambao kwa...
Marato tv - Sauti ya Jamii