Skip to main content

Posts

Showing posts from October 22, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Baada ya Kushindwa "Kulitumia" Jwtz Sasa Wamekuja na "Uzushi" Mpya Kwamba Jeshi la Uganda(Updf)Lipo Nchini

George Michael Uledi.  October 23,2025. Wanaharakati wa Chadema  walio Nje ya Nchi (Sweden Kenya na Marekani) wakishirilkiana na Viongozi wa Chadema wa ndani ya Nchi wamekuwa kwenye kutekeleza "mradi" wao ili Nchi iingie kwenye machafuko. No Reforms No Election Part II ndio ipo katika execution kuelelea Uchaguzi Mkuu wa October  29,2025. Malengo Makuu Matatu ya No Reforms No Election ni (I)kuhamasisha maandamano ili(II)kuvuruga Uchaguzi Mkuu October,2025 (III)kuishinikiza Serikali kufanya mabadiliko ya lazima ambayo wanayataka wao(KATIBA MPYA). MPANGO UNACHORWA HIVI👇🏾👇🏾 I.Strategy ya kwanza ilikuwa ni kuchonganisha vyombo vyetu vya ulinzi na Usalama (JWTZ vs Jeshi la Polisi).Wakasema Jeshi la Wananchi(TPDF)lipo nyuma ya Mwananchi hivyo watu wengi watoke October 29,2025 kwenda kwenye Maandamano na eti hakuna Polisi atakayewagusa. Baada ya kuona Jeshi la Wananchi (JWTZ)limekataa kuwa sehemu ya SIASA kwa matamko mawili ya Kaimu Msemaji Mkuu wa Jeshi,JWTZ wakawa tayari ya...

Waziri wa Mambo ya Nje Ateta na Balozi wa Kenya Nchini

 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo, amekutana na Balozi wa Kenya nchini, Mhe. Isaac Njenga, katika jitihada za kuendelea kuimarisha ushirikiano na kuleta maendeleo kati ya nchi hizo mbili. Wakati wa mazungumzo yao, Waziri Kombo amesisitiza dhamira ya Serikali ya Tanzania kuendeleza uhusiano wa muda mrefu na Kenya, hususan katika maeneo ya biashara, uwekezaji, miundombinu na nishati, ili kukuza uchumi wa pamoja na kuimarisha Jumuiya ya Afrika Mashariki. Kwa upande wake Balozi wa Kenya Mhe. Njenga amepongeza uhusiano mzuri uliopo baina ya mataifa haya mawili jirani na kuahidi kuendelea kushirikiana na Tanzania katika kuendeleza sekta za kipaumbele zinazochangia ustawi wa wananchi wa pande zote mbili.

Kampeni ya "Nipitie Tukatiki" inavyohamasisha wananchi kupiga kura Oktoba 29

Na: Dkt. Reubeni Lumbagala Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ni moja ya Jumuiya muhimu kwa uhai na maendeleo ya CCM. Misingi mikuu ya Jumuiya hii kutoa elimu na malezi kwa jamii. Elimu ni nyenzo muhimu katika kujenga ustawi na maendeleo ya jamii. Ili jamii ipige hatua za kimaendeleo suala la elimu haliepukiki. Jumuiya ya Wazazi licha ya kuwa ni Jumuiya ya kisiasa lakini inatoa elimu ya masuala mbalimbali katika jamii. Kwa kutambua umuhimu wa elimu katika jamii, Jumuiya hii ina miliki shule zake ili kuchagiza vizuri msingi wake wa kutoa elimu kwa jamii. Sambamba na hilo, Jumuiya hii pia imejengwa katika msingi wa kutoa malezi kwa jamii juu ya masuala mbalimbali muhimu katika jamii. Malezi bora katika jamii yanasaidia kujenga jamii yenye raia wenye maadili mazuri na wanaowajibika, hivyo kusaidia katika kufanikisha maendeleo. Jumatano ya Oktoba 29, 2025, ni siku muhimu kwa nchi yetu ya Tanzania. Ni siku ya Uchaguzi Mkuu. Wananchi wanapata fursa ya kutimiza haki yao ya kikatib...