Skip to main content

Posts

Showing posts from April 10, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Jaji Mtungi-hakuna Chama cha Siasa cha Kuzuia Uchaguzi Mkuu Mwaka huu

Msajili wa vyama vya Siasa Tanzania, Jaji Francis Mutungi amesema hata kama kauli ya ‘No reform, no Election’ haijavunji sheria ya vyama vya siasa,lakini kamwe isitumike kama kichocheo cha kuvunja sheria za nchi na katiba ya  Jamhuri ya muungano wa Tanzania. Amesema ofisi yangu inafuatia kwa karibu kauli kama hizo zinazotumiwa na baadhi ya vyama vya siasa katika kuvunja sheria na katiba ya nchi. Jaji, Mutungi amesema hayo wakati akizungumza na George Marato Tv huku akisisitiza kuwa hakuna chama cha siasa chenye uwezo wa kuzuia uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika badae mwaka huu 2025. Amesema katika mazungumzo yake na waandishi wahabari baada ya kushiriki warsha ya wadau wa kujadili namna ya kuzuia na kupambana na rushwa katika uchaguzi mkuu 2025,akiwaeleza wazi mazungumzo yake na vyama vya siasa ikiwemo Chadema kwamba ofisi yake hauwezi kuvumilia kauli zinazolenga kuvunja sheria za nchi. Tangu kumalizika kwa uchaguzi wa ndani, CHADEMA wamekuwa wakieleza kuwa, bila mabadiliko katik...

Robbi Samwelly Awakumbusha Wazazi Malezi Bora Kwa Watoto Kwenye Kongamano

Na Shomari Binda-Butiama  MJUMBE wa Baraza la UWT Taifa kutoka mkoa wa Mara na mkurugenzi wa kituo cha malezi ya watoto wa kike cha nyumba salama Robbi Samwelly amewakumbusha wazazi kuzingatia malezi bora ya watoto. Ukumbusho huo ameutoa leo aprili 9,2025 kwenye kilele cha maadhimisho ya wiki ya wazazi kwa mkoa wa Mara. Akizungumza kwenye kongamano la madhimisho hayo kwenye ukumbi wa Kanisa Katoriki Butiama amesema kama malezi yatasimamiwa vizuri kuanzia ngazi ya jamii vitendo vya ukatili havita kuwepo. Amesema kituo cha nyumba salama kimekuwa mstari wa mbele kuwapokea watoto wa kike wanaokimbia na wanaofanyiwa vitendo vya ukatili na kuomba kuwepo kwa usimamizi Nora wa malezi. Robbi amesema kila mmoja akitimiza jukumu lake kwenye suala la malezi hakuna mtoto atakayekimbia nyumbani kutikana na kuogopa kufanyiwa ukatili. Mjumbe huyo amesema kupitia kituo cha nyumba salama kilichopo Butiama na Serengeti wameweza kuwalea watoto kwa kuwaps elimu hadi kufikia ngazi ya chuo kikuu. Mwenyek...

Ccm Yafungua Milango ya Kugombea Nafasi za Dola

 

Wakandarasi Jimbo la Tarime Vijijini Waonyeshwa Maeneo ya Ujenzi wa Miradi 19 Fedha za Csr

Na Shomari Binda-Tarime WAKANDARASI wanaokusudiwa kutekeleza miradi 19 ya maendeleo kwenye vijiji mbalimbali kwenye jimno la Tarime Vijijini wameonyeshwa maeneo ya utekelezaji. Ziara iliyofanyika april 9,2025 iliyowahusisha wataalam na ofisi ya mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini imeshiriki huku lengo ikiwa kuanza utekelezaji wake mara moja. Kwa mujibu wa taarifa kutoka ofisi ya mbunge imesema maeneo yaliyofikiwa ni pamoja na Nyarokoba Kijiji cha Msenge ambapo kuna ujenzi wa jengo la utawala shule ya msingi Musege pamoja na nyumba ya mwalimu. Eneo la pili lililofikiwa ni Kata ya Gorong'a Kijiji cha Kenyamsabi ambapo kuna ukamilishwaji wa zahanati ya Kijiji hicho pamoja na Kijiji cha Nyanungu ambapo pia kuna ujenzi wa zahanati. Kwa mujibu wa taarifa hiyo kutoka ofisi ya mbunge Kata ya Itiryo Kijiji cha Kangariani pia kimefikiwa kikiwa na ujenzi wa nyumba ya mtumishi na zahanati. Ujenzi wa jengo la kufulia na njia za kupita wagonjwa kituo cha afya Magoma Kijiji cha Magoma kimefikiwa n...

Rais Dkt. Samia kuzindua Benki ya Ushirika mkoani Dodoma

Na MWANDISHI WETU RAIS Dkt. Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuzindua Bank ya Ushirika Tanzania (CoopBankTanzania), mkoani Dodoma lengo likiwa ni kufufua benki za kijamii zilizofilisika nchini. Akizungumza mkoani Dodoma Waziri wa Kilimo Husein Bashe, amesema Wizara ilipokea maagizo ya Rais Dkt Samia, kuhakikisha benki za kijamii zilizofilisika zinarejea na katika hatua za awali mnamo April 28 Rais atazindua Benki ya Ushirika nchini. Amesema Benki hiyo itazinduliwa ikiwa na matawi manne ambayo yanapatikana Dodoma, Mtwara, Kilimanjaro na Tabora. “Hatua ya pili itahusisha matawi ya Kagera, Mwanza,Dar es Salaam, Mbeya na Katavi. “Mafunzo kwa mawakala yanaendelea hivyo mbali na matawi hayo kutakuwa na mawakala nchi nzima na kabla ya uzinduzi mnamo April 28 kutatanguliwa na kongamano la wanaushirikika April 27,”amesma. Waziri Bashe amesema, hatua hiyo ni maelekezo mahususi ya Rais Dkt. Samia kwa Wizara ya Kilimo. Amesema, Benki nyingi za ushirika zimefilisika na Rais Dk.Samia ameona haja ya k...

Waziri Mkuu: Sh. Trilioni 1.59 Zatumika Kuunganisha Umeme Katika Vijiji 4,071

*Nguvu sasa kuelekezwa kwenye vitongoji WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema tangu Novemba, 2020 hadi Februari, 2025 Serikali imeunganisha umeme katika vijiji 4,071 kwa gharama ya sh. bilioni 1,593 na hivyo kuwezesha vijiji vyote 12,318 vya Tanzania Bara kuunganishwa na umeme. “Hatua inayofuata baada ya kukamilisha mradi wa kupeleka umeme katika vijiji vyote, ni  kupeleka umeme kwenye vitongoji ambapo jumla ya vitongoji 33,657 kati ya 64,359, sawa na asilimia 52.3 vimeunganishwa na huduma ya umeme,” amesema. Ameyasema hayo jana (Jumatano, Aprili 9, 2025) Bungeni jijini Dodoma, wakati akiwasilisha taarifa ya Mapitio ya Utekelezaji wa Kazi za Serikali kwa mwaka 2024/2025 na mwelekeo wa kazi zake na makadirio ya mapato na matumizi ya fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na Ofisi ya Bunge kwa mwaka 2025/2026. Akitoa taarifa kuhusu uunganishaji wa umeme vijijini, Waziri Mkuu alilieleza Bunge kwamba usambazaji wa umeme katika vijiji na vitongoji utawezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika sh...