Profesa Kithure Kindiki ameapishwa kuwa naibu rais wa Jamhuri ya kenya. Profesa Kindiki amechukua nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Naibu rais wa Kenya Rigathi Gachagua aliyeondolewa ofisini na Bunge la kitaifa na Bunge la seneti baada ya kuhusishwa na tuhuma kadhaa zikiwemo za kuendeleza ukabila. Akizungumza Mara baada ya kula kiapo,Profesa Kindiki ameahidi kutekeleza majukumu yake kwa kuzingatia sheria za nchi pamoja na kumshauri vyema Rais wa taifa hilo Dkt.William Ruto. Profesa Kindiki ambaye kabla ya uteuzi huo alikuwa waziri wa usalama wa ndani na utawala wa Taifa na anakuwa Naibu rais wa 14 katika historia ya kenya na wa tatu chini ya katiba mpya ya mwaka 2010. Kabla ya kuteuliwa waziri mwaka 2022 na Naibu rais mwaka 2024,Profesa Kithure Kindiki alihudumu kama seneta wa kaunti ya Tharaka Nithi kuanzia mwaka 2013 hadi 2022 ambapo katika kipindi hicho pia alihudumu kama Naibu Spika wa Bunge la Seneti pamoja na kiongozi wa wengi katika Seneti. Akiwa Kiongoz...
Marato tv - Sauti ya Jamii