Skip to main content

Posts

Showing posts from June 20, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

PROF. SHEMDOE AWAASA VIJANA KUWA WAADILIFU, WAZALENDO WANAPOTUMIKIA UMMA NA TAIFA

 Na OWM - TAMISEMI, Morogoro Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amewaasa vijana wa vyuo vikuu kuwa waadilifu na wazalendo pindi watakapoajiriwa Serikalini kuwatumikia wananchi au kupata fursa za uongozi wa kulitumikia taifa. Prof. Shemdoe ametoa wito huo kwa vijana hao Juni 20, 2026, wakati akifungua Kongamano la Vijana (Youth Uongozi Forum) kwa niaba ya Mhe. Prof. Palamagamba John Aaidan Kabudi Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) ambalo linalofanyika katika Ukumbi wa Chuo Kikuu cha Mzumbe mjini Morogoro, lililoandaliwa na taasisi ya Tanzania Leadership Foundation (TLF). “Vijana wangu, watoto wangu, wadogo zangu mjitahidi sana kuwa waadilifu na wazalendo kwani mkishindwa kuwa waadilifu na wazalendo hamtaweza kudumu katika nafasi mtakazoaminiwa kuzitumikia,” amesisitiza Prof. Shemdoe. Sanjari na hilo, Prof. Shemdoe amewataka vijana hao kuwa wanyenyekevu watakapopa...

WAZIRI MKUU AKICHAPA KAZI NDANI YA TRENI

 Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba akiwa katika majukumu yake ya kazi ndani ya Treni ya kisasa (SGR) akitokea Dar es Salaam kuelekea Dodoma leo Juni 20, 2026.

RAIS SAMIA NA RAIS NETUMBO WASHUHUDIA WATIAJI SAINI HATI ZA MAKUBALIANO

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na Mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Namibia Mhe.Dkt.Netumbo Nandi-Ndaitwah wakati wakishuhudia utiaji saini wa Hati nne za makubaliano ya ushirikiano katika Sekta za biashara , Maendeleo ya biashara ndogo na za kati, Ulinzi , pamoja na ushirikiano wa Miji kati ya Manispaa ya mji wa Zanzibar na Manispaa ya Swakopmund kabla ya kuzungumza na waandishi wa habari, Ikulu Jijini Dar-es-salaam, tarehe 20 Juni, 2026.

SALVATOR:MAJI, KILIMO,BARABARA NA USAFIRI WA SGR NDIO KIPAUMBELE CHANGU MISUNGWI

 Mbunge wa Misungwi mkoani Mwanza, Silvery Salvator ameainisha vipaumbele vya maendeleo ya jimbo hilo akisisitiza umuhimu wa sekta za maji, kilimo, barabara, afya, elimu pamoja na fursa zinazotokana na Mradi wa Reli ya Kisasa (SGR). Akizungumza kuhusu hali ya maendeleo ya jimbo hilo, Salvator amesema kipaumbele kikubwa kwa wananchi wa Misungwi ni upatikanaji wa maji safi na salama.  Amesema licha ya jimbo hilo kuwa na vyanzo vikubwa vya maji, bado baadhi ya maeneo yanakabiliwa na changamoto ya uhaba wa maji. Katika sekta ya kilimo, ameeleza kuwa Misungwi ina fursa kubwa ya uzalishaji kupitia mabonde na maeneo yanayofaa kwa umwagiliaji, ambayo yanaweza kutumika kuzalisha mazao ya chakula na biashara kama mboga mboga, matunda na nafaka. Amesisitiza kuwa uwekezaji katika miundombinu ya umwagiliaji utaongeza tija na kuchochea uchumi wa wananchi. Kuhusu miundombinu ya usafiri, Mbunge huyo amesema ujenzi na ukarabati wa barabara pamoja na madaraja ni muhimu katika kufungua shughuli ...

ELIMU YA ULINZI NA USALAMA BINAFSI WA MTOTO YATOLEWA KATIKA KAMBI YA WATOTO YA KANISA LA ROC DODOMA.

 Katika kuhakikisha Watoto wanakuwa na uangalizi mzuri kuanzia ngazi ya familia Kanisa la ROC Dodoma limewapatia  elimu ya ulinzi na usalama binafsi, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuwajengea uwezo wa kujilinda dhidi ya changamoto na vitisho mbalimbali vinavyowakabili katika jamii ya sasa. Akishiriki katika Mafunzo hayo Mkuu wa Polisi Jamii Wilaya ya Kipolisi Mtumba Mrakibu wa Polisi (ASP)Charles Mwamtobe aliwahimiza watoto kuwa waangalifu na kutambua mapema viashiria vya hatari vinavyoweza kuhatarisha usalama wao, ikiwemo ukatili, unyanyasaji wa kijinsia, matumizi mabaya ya teknolojia, dawa za kulevya, biashara haramu ya binadamu pamoja na ushawishi wa makundi yenye mienendo isiyofaa. Alieleza kuwa mtoto si mali ya familia pekee, bali ni tumaini la jamii na taifa la leo, hivyo anapaswa kulindwa na kupewa malezi bora yatakayomwezesha kukua katika mazingira salama, yenye maadili mema na hofu ya Mungu. “Ulinzi na usalama wa mtoto si jukumu la serikali pekee wala wazazi peke yao, b...