Halmashauri Zitoe Tenda Kwa Vikundi Vya Mikopo Ya Asilimia 10 Ili Kuongeza Wigo wa Ajira - Prof. Shemdoe
Na OWM TAMISEMI - Tanga Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amezitaka Halmashauri kuvipa kipaumbele vikundi vya wanawake, vijana na wenye ulemavu vilivyonufaika na mikopo ya aslimia 10 kwa kuvipatia kazi (tenda) ili kuongeza wigo wa ajira kwa wananchi. Prof. Shemdoe ametoa maelekezo hayo hivi karibuni, akiwa jijini Tanga katika Uwanja wa Tangamano, mara baada ya kukagua shughuli za vikundi vya wajasiriamali walionufaika na mikopo ya asilimia 10 mkoani Tanga na kuvikabidhi vikundi hivyo hundi ya mikopo ya asilimia 10 yenye thamani ya Shilingi Bilioni 2.761. “Nimeona kikundi cha vijana kilichokopeshwa na kuanzisha mradi wa kufyatua tofali na kimeweza kuajiri vijana wengine, hivyo nazielekeza Halmshauri zenye miradi ya ujenzi kutoa tenda kwa vikundi vya vijana kama hiki cha uzalishaji wa tofali,” Prof. Shemdoe amesisitiza. Prof. Shemdoe ameongeza kuwa, amejionea kikundi kingine kilichokopeshwa na kuanzisha kam...