Na Angela Sebastian TAASISI ya kupamba na kuzuia Rushwa mkoani Kagera (TAKUKURU) imeokoa kaisia cha shilingi milioni 4.3 baada ya kupokea taarifa ya ubadhirifu wa fedha za mfuko wa maendeleo wa kunusuru kaya maskini (TASAF) kutoka kwa wananchi wa kijiji cha Kumutana kata ya Kibimba Wilayani Ngara mkoani hapa. Ezekia Sinkala naibu mkuu wa taasisi hiyo mkoa wa Kagera alieleza hayo leo wakati akiongea na vyombo mbalimbali vya habari ofisini kwake mjini Bukoba wakati akitoa taarifa ya utekelezaji kwa kipindi cha Aprili hadi Juni mwaka huu. “Baada ya kufanyika uchunguzi ilibainika kuwa mnamo Septemba 20 mwaka 2020 kulikuwa na zoezi la uhaulishaji wa fedha za TASAF katika kijiji Kumutana ambazo zilikuwa za mwezi Mei hadi Juni na mwezi Julai hadi Agosti ambapo ulikuwa mgao wa madilisha mawili kwa wanufaika 139" Amesema baada ya kufuatilia mwenendo wa ugawaji wa fedha hizo walibaini fedha zilizokuwa zimechukuliwa na kupelekwa kijijini hapo ziliku...
Marato tv - Sauti ya Jamii