Skip to main content

Posts

Showing posts from September 22, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Tashico Yamshukuru Rais Samia Kwa Kukamilisha Ujenzi wa Meli Mpya Mv Mwanza

Silivia Amandius; Bukoba, Kagera. Kampuni ya Huduma za Meli Tanzania (TASHICO) imetoa shukrani kwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan kwa kufanikisha ukamilishaji wa meli mpya ya MV Mwanza, mradi uliochukua zaidi ya miaka mitano kukamilika. Mkurugenzi Mtendaji wa TASHICO, Ndg. Eric Hamiss, alisema meli hiyo itakuwa chachu ya ukuaji wa uchumi wa taifa na Kanda ya Ziwa kwa ujumla, kwa kuwa itaongeza fursa za biashara na kurahisisha usafirishaji wa abiria na mizigo. Aidha, alibainisha kuwa meli hiyo itaendesha safari zake hadi Port Bell nchini Uganda, jambo litakaloimarisha uhusiano wa kibiashara na kikanda. Meli hiyo imegharimu zaidi ya shilingi bilioni 126 na ina uwezo wa kubeba abiria 1,200 na mizigo yenye tani 400, huku ikikadiria kutumia kati ya saa 6 hadi 6 na nusu katika safari zake. Mwakilishi wa mkandarasi kutoka kampuni ya Gas Entec Co. Ltd, Eng. Rayton Kwembe, alieleza kuwa meli hiyo imekamilika kwa asilimia 99, baada ya kuachwa kwa asilimia 30 kipindi ...

Waziri Kombo Ashiriki Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje Nchini Marekani

 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mahmoud Thabit Kombo, akishiriki Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola, pembezoni mwa Mkutano wa 80 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, unaofanyika jijini New York, Marekani.

Machifu Waupokea kwa Furaha Mradi wa Ujenzi wa Barabara ya Ruanda–Idiwili

22 Septemba 2025 Mbozi – Machifu wa kimila Wilayani Mbozi katika maeneo ambapo mradi wa ujenzi wa barabara ya kiwango cha lami kutoka Ruanda hadi Idiwili unapita, wameupokea mradi huo kwa mikono miwili na kuahidi kuulinda, kuutunza na kushirikiana nao ili kuhakikisha unakamilika kwa mafanikio. Akizungumza wakati wa hafla ya mapokezi ya mradi huo, Mpewa Nzunda, Chifu wa Idiwili, alisema wao kama viongozi wa kimila wako tayari kuupokea mradi huo na kutoa onyo kali kwa yeyote atakayejihusisha na vitendo vya kuikwamisha miradi ya maendeleo. “Mtu yeyote atakayethubutu kuhujumu au kukwamisha mradi huu, sisi kama viongozi wa kimila tutashughulika naye kwa taratibu zetu. Huu ni mradi wa maendeleo kwa manufaa ya vizazi vyote,” alisema Chifu Nzunda. Kwa upande wake, Chifu Mwamlima wa Iyula aliwataka wakandarasi wa mradi huo, ambao ni wanawake, kushirikiana kwa karibu na viongozi wa kimila na wananchi katika kutatua changamoto zitakazojitokeza, ikiwemo tatizo la wizi wa vifaa vya ujenzi. “Wizi ni...

Sekta ya Madini Imeendelea Kuwa Nguzo ya Ukuaji wa Uchumi-Majaliwa

WAZIRI MKUU,Kassim Majaliwa amesema kuwa Sekta ya madini imeendelea kuwa nguzo ya uchumi nchini ambapo katika mwaka 2022 sekta hiyo imekua kwa asilimia 10.9 na kufikia mchango wa asilimia 10.1 kwenye Pato la Taifa mwaka 2024, ikilinganishwa na asilimia 9.0 mwaka 2023. Ametoa kauli hiyo Leo (Jumatatu, Septemba 22, 2025) wakati wa uzinduzi wa Maonesho ya Nane ya Teknolojia ya Madini Mkoa wa Geita, yaliyofanyika katika viwanja vya Dkt. Samia Suluhu Hassan. Amesema kuwa hatua hiyo imetokana na jitihada mbalimbali za Serikali ya awamu ya sita ikiwemo kuimarishwa kwa mifumo ya ukusanyaji wa mapato na udhibiti wa biashara ya madini,  matumizi ya mifumo ya kielektroniki (online mining cadastre system), uwepo wa masoko ya madini na ufuatiliaji wa mikataba ya uwekezaji. "Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuweka kipaumbele katika kuimarisha mazingira ya uwekezaji kwenye sekta ya madini ili rasilimali za madini zichangie kwa katika uk...

Waziri Mkuu Apongeza Huduma Kidijitali za NSSF Maonesho ya Madini Geita

Na MWANDishi WETU, Geita Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, ametembelea banda la Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) katika Maonesho ya Nane ya Madini yanayoendelea kwenye Viwanja vya Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mkoani Geita, na kuipongeza NSSF kwa huduma zake za kidijitali kwa wananchi na wadau. Akiwa kwenye banda hilo tarehe 22 Septemba 2025, Mhe. Waziri Mkuu alipokea maelezo kutoka kwa Meneja Uhusiano na Elimu kwa Umma wa NSSF, Bi. Lulu Mengele, kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu Masha Mshomba, kuhusu ahadi za Mfuko kutekeleza maagizo ya Serikali kufunika elimu ya hifadhi ya jamii inaendelea kutolewa kwa sekta binafsi na wananchi waliojiajiri. Bi. Lulu alisema: “Mafanikio yetu makubwa yametokana na mwongozo wa Serikali wa kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora, rahisi na kwa wakati kupitia mamlaka ya kidijitali.” Aidha, alimwonesha Waziri Mkuu kanuni za kidijitali inayorahisisha huduma kwa huduma zote kwa mwanachama, huduma zinazopatikana kupitia ...

Dkt.Nchimbi Awasili Ludewa,Mkoani Njombe Kuendelea na Mikutano yake ya Kampeni

MGOMBEA Mwenza wa Kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John  Nchimbi, amewasili wilayani Ludewa mkoani Njombe,leo Jumatatu Septemba 22,2025 kuendelea na mikutano yake ya kampeni akitokea  Mkoa wa Ruvuma. Dkt.Nchimbi amewasili kwenye uwanja wa mpira wa Ludewa na kupokewa na Viongozi waandamizi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kuwasalimia Wananchi kabla ya kuwahutubia. Akiwa katika mkutano huo,Dkt Nchimbi ambae ni Mgombea Mwenza wa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan pamoja na mambo mengine atawahutubia Wananchi wa jimbo la Ludewa na kuwanadi Wagombea Ubunge wa majimbo ya  Mkoa huo,akiwemo mgombea Ubunge wa jimbo la Ludewa,Ndugu Joseph Zacharius Kamonga na Madiwani. Dkt. Nchimbi anaendelea kuinadi Sera na  Ilani ya CCM ya Uchaguzi Mkuu 2025-2030,ambayo  inakwenda kuboresha maisha ya wananchi na ustawi wa Maendeleo katika miaka mitano ijayo. Aidha,amekuwa akitumia  nafasi hiyo pia kuwaomba wananchi k...

Majaliwa Kuzindua Maonesho ya Teknolojia ya Madini Geita

WAZIRI MKUU,Kassim Majaliwa leo Septemba 22, 2025 amefungua maonesho ya nane ya teknolojia ya madini kwa mwaka 2025 ambayo yamefanyika kwenye viwanja vya Dkt. Samia Suluhu Hassan mkoani Geita. Maonesho hayo ya Teknolojia ya Madini ambayo yalianzishwa mwaka 2018 yanalenga kuimarisha sekta ya madini nchini na kuhakikisha kuwa rasilimali madini inawanufaisha Watanzania wote.  Maonesho hayo yamekuwa jukwaa mahsusi la Serikali, sekta binafsi, wachimbaji wakubwa na wadogo, taasisi za kifedha, wajasiriamali na wadau mbalimbali wa maendeleo kukutana, kujadili na kubadilishana uzoefu. kaulimbiu ya Maonesho ya Teknolojia ya Madini kwa mwaka huu wa 2025 ni: “Ukuaji wa Sekta ya Madini ni Matokeo ya Matumizi ya Teknolojia Sahihi na Uongozi Bora/Shiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba, 2025.”