Skip to main content

Posts

Showing posts from January 10, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Tamasha la Pasaka Mwaka Huu Kupambwa na Wasanii Kutoka Nchi Mbalimbali

 Wasanii nguli wa nyimbo za Injili kutoka mataifa mbalimbali wanatarajiwa kuungana na waimbaji wa Nyimbo za Injili hapa nchini kutumbuiza katika Tamasha la Pasaka ambalo huandaliwa na kuratibiwa na Kampuni ya Msama Promotions ambapo kwa msimu huu linatarajiwa kufanyika kwa mikoa 20 likianzia na Mkoa wa Dar es Salaam. Mapema akizungumza na waandishi wa Habari Mkurugenzi wa Msama Promotions Alex Msama amesema msimu huu wa pasaka Tamasha hilo litaanza tarehe 5 ya mwezi wa nne,likizunguka katika mikoa 20,kutoa burudani likiwa limesheheni wasanii mbalimbali wakubwa kutoka Tanzania na nje ya Tanzania lengo ikiwa ni kuwapa burudani waumini wa dini ya kikristo na wasio wa kristo sambamba na kutoa ujumbe wa kiroho. Kadhalika Msama amesema wasanii wakubwa wanatarajiwa kupanda katika majukwaa hayo kutoa burudani kabambe kwa mikoa 20 kwani hiyo ni dhamira ya wao kama waandaji kuwapa burudani waumini wa Injili. Ikumbukwe Tamasha hilo ambalo huandaliwa na Msama Promotions limekuwa maarufu kwa...

Rais Atangaza Kuwateua Dkt Mpango na Majaliwa

  Rais Samia Suluhu Hassan ametangaza kumteua Makamu wa Rais mstaafu, Dkt Philip Mpango kuwa mshauri wake wa masuala ya uchumi na miradi. Pamoja naye, ametangaza kumemteua Waziri Mkuu mstaafu, Kassim Majaliwa kuwa mshauri wake wa masuala ya jamii. Hata hivyo, uteuzi wa wawili hao ni utekelezaji wa ahadi aliyoitoa Dkt Samia wakati wa kampeni za uchaguzi, aliposema ataendelea kuwatumia wawili hao kwa shughuli za Serikali. Dkt Samia ametangaza uteuzi huo, leo Jumamosi Januari 10, 2026 wakati wa hafla ya kuwapongeza wanamichezo waliofanya vizuri katika mashindano ya kimataifa Ikulu ya Dar es Salaam. Amesema katikati ya Dkt Mpango na Majaliwa watakaomshauri kwenye masuala ya uchumi, miradi na jamii, kutakuwa na Profesa Palamagamba Kabudi akisema ndiye atakayefanya kazi nao kwa karibu. “Vile vichwa viwili vikubwa (Dk Mpango na Majaliwa) vinahitaji mtu aliyetulia anayeweza kudili nao.  Hawa watoto wangu mara wanaweza kujijibia ikaja kesi, lakini Profesa (Kabudi) anaweza kwenda nao vi...