Na MASHAKA MHANDO, Pangani SPIKA wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar Zubeir Ali Maulid, amewataka Watanzania wauenzi na kuulinza Muungano kwa kushiriki uchaguzi Mkuu ujao kwa kuchagua viongozi sahihi. Akizungumza Leo April 25 baada ya kukagua na kuzindua madarasa sita ya shule ya sekondari ya Bushiri wilayani hapa, alisema Muungano ni tunu iliyoasisiwa na viongozi hivyo hakuna budi kuulinda kwa nguvu zote. Alisema Watanzania wanapoazimisha miaka 61 ya Muungano, wanatakiwa kukumbuka faida na fursa zilizotokana na Muungano huo lakini pia kutazama namna ya kuepuka chokochoko zenye viashiria vya kuvunja Muungano huo. "Wote hapa zaidi ya asilimia 80 tuliopo hapa tumezaliwa ndani ya Muungano hivyo tunayo sababu kubwa ya kuenzi, kuulinda kwa kushiriki uchaguzi Mkuu ujao ili tuwapate viongozi wetu," alisema na kuongeza, "Tunapoadhimisha maadhimisho ya miaka 61 ya Muungano wetu tunatakiwa tukumbuke faida na fursa zilizopatikana kupitia Muungano wetu,". Akizungumza kuhusu s...
Marato tv - Sauti ya Jamii