Skip to main content

Posts

Showing posts from September 12, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Miaka mitano ijayo wananchi Muheza mtakuwa na maji majumbani- MwanaFA

Na Mwandishi Wetu, Muheza MGOMBEA ubunge wa Jimbo la Muheza kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Hamisi Mwinjuma maarufu MwanaFA amesema endapo atachaguliwa kuwa mbunge wananchi wa kata ya Lusanga na Muheza kwa ujumla wataweka maji ya bomba nyumbani kwao badala ya kuchota kwenye vilula. Akizungumza katika mkutano wa kampeni katika kata ya Lusanga, MwanaFA alisema kuwa tatizo la maji Muheza kabla hajakuwa mbunge, wilaya hiyo ilikuwa na shida ya maji kubwa lakini Sasa kuna ahueni ya kutosha. Alisema kata ya Lusanga pekee ilipata kiasi cha shilingi milioni 700 kwa ajili ya miradi ya maji ambayo ilipunguza tatizo hilo kwa wananchi. Aliwahakikishia wananchi hao kwamba fedha zaidi za maji zitakuja wilayani humo kupitia mradi wa Green Bond ambao umechangiwa kiasi cha shilingi bilioni 100 kwa ajili ya miradi ya maji mkoa wa Tanga na Muheza utashughulikia kiasi cha kilomita 15 ili maji yawe majumbani. "Tunataka ndani ya miaka mitano ijayo sehemu ya Lusanga Kila mtu ameweka maji nyumbani...

Tarura Karagwe Yatangaza Mipango Mikubwa Katika Ujenzi wa Barabara

Na Angela Sebastian; Karagwe  Wilaya ya Karagwe kupitia wakala wa Barabara za vijijini na mjini TARURA imejipanga  kuongeza mtandao wa Barabara za lami kutoka kilometa 25.29 hadi kilometa 28.29  ifikapo  Novemba mwaka baada ya kukamilisha kilometa tatu za Lami katika mradi wa Barabara ya  Nyakahanga -Nyabionza. Mbio za mwenge wa uhuru mwaka 2025 zimeweka jiwe la Msingi katika barabara hiyo ambayo Mradi wake umefikia asilimia 83. Meneja wa TARURA Wilaya ya Karagwe  Kalembula Malimi amesema kuwa  Serikali iliidhinisha shilingi Bilioni 1.5 kwa ajili ya matengenezo ya Barabara hiyo kwa kiwango cha Lami na mpaka sasa mkandarasi amelipwa shilingi Bilioni 1.1   Amesema Barabara hiyo ni moja ya Barabara zinazochochea Uchumi wa wananchi  na kurahisisha huduma za jamii. Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa Ismail Ussi amewataka wananchi Kutumia Fursa za uwepo wa Barabara hiyo kufanya biashara  kwa nyakati zote ili kukuza Uchumi wao na ...

Ujenzi wa Kituo cha Afya Nyabiyonza Mbioni Kukamilika

 Na. Angela Sebastian ;Karagwe  Wananchi 12,325 wa tarafa za Nyabiyonza na Nyakakika Wilayani Karagwe mkoani Kagera wanatarajiwa kupata huduma bora katika kituo cha Afya Nyabiyonza ambacho kimefikia asilimia  98 ya ujenzi. Agnes Mwaifuge ni mganga mkuu wa Wilaya ya Karagwe wakati akisoma taarifa ya mradi huo kwa kiongozi wa mbio za mwenge Kitaifa 2025 Ismail Ali Ussi amesema mradi huo utagharimu kiasi cha shilingi milioni 640.1 na utakapokamilika utaboresha huduma stahiki  kwa wananchi ikwemo akina mama wajawazito na watoto wachanga ili kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi. Amesema ujenzi wa kituo cha Afya Nyabiyonza ulianza Oktoba 25,2024 na unatarajiwa kukamilika Septemba 25 mwaka huu ambapo umefikia asilimia 98 na yapo majengo matano ikiwemo jengo la upasuaji,wagonjwa wa nje,wodi ya wazazi,maabara jengo la kufulia na kichomea taka . Kiongozi wa mbio za mwenge Kitaifa 2025 Ismail Ali Ussi ametembelea na kuweka jiwe la msingi Katika mradi huo na kuridishwa na maendel...

Dkt.Nchimbi amehutubia na kuzindua kampeni za Jimbo la Arusha Mjini

MGOMBEA Mwenza wa Kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John  Nchimbi, akiwahutubia Wananchi kwenye Mkutano wake wa Kampeni leo Ijumaa Septemba 12,2025 katika Uwanja wa Soweto, jijini Arusha. Akiwa katika  mkutano huo Dkt Nchimbi pia alipata wasaa wa kuwanadi wagombea Ubunge  wa mkoa huo, akiwemo Mgombea Ubunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Ndugu Paul  Christian Makonda pamoja na madiwani. Aidha Dkt. Nchimbi pia aliongoza uzinduzi wa mikutano ya kampeni kwa Jimbo la Arusha Mjini mbele ya Wananchi waliofika kumsikiliza. Dkt. Nchimbi ameendelea kuinadi Ilani ya CCM ya Uchaguzi Mkuu ya mwaka 2025-2030, ambayo kimsingi imelenga kwenda kuboresha maisha ya wananchi na ustawi wa maendeleo katika miaka mitano ijayo. Ngombea mwenza huyo amekuwa akitumia  nafasi hiyo kuwaomba wananchi kumchagua mgombea Urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan, wabunge na madiwani wa chama hicho kwa kur...