■ Ni mkakati wa kuhakikisha madini vito yanaongezewa thamani nchini. ■Ni utekelezaji wa maelekezo ya Rais.Dkt. Samia katika kuendeleza mnyororo wa madini thamani. ■Waziri Mavunde amtaka mkandarasi kuongeza nguvukazi kukamilisha mradi kwa wakati. ▪️Atoa siku 7 kwa Katibu Mkuu kukutana na wakandarasi,TGC na Taasisi za serikali kwa ajili ya upatikanaji vibali muhimu vya kuendeleza ujenzi. *Arusha* Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde amemtaka mkandarasi wa ujenzi wa kituo cha Jemolojia Tanzania (TGC) kukamilisha ujenzi wa majengo ya kituo cha mafunzo ya Uongezaji thamani madini ya vito kwa kuongeza nguvukazi na kufanya kazi kwa masaa 24 ili kukamilisha ujenzi wa jengo kwa muda mfupi. Waziri Mavunde ameyasema hayo leo Desemba 12, 2025 mkoani Arusha wakati wa ziara yake ya kukagua mradi wa kituo hicho ulioanza ujenzi rasmi ambapo katika maelekezo yake amemtaka mkandarasi kuzingatia ujenzi bora wenye kukidhi vigezo vilivyoainishwa kwenye mkataba. Waziri Mavunde amefafanua kuwa, Serika...
Marato tv - Sauti ya Jamii