Skip to main content

Posts

Showing posts from July 26, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Rais Samia Afanya Mazungumzo na Rais wa Shirika la Fedha na Ujenzi la Nchi ya Korea

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amekutana  na kufanya mazungumzo na Rais wa Shirika la Fedha na ujenzi la Korea (K-FINCO) Dkt. Eun-Jae Lee aliyeambatana na ujumbe wake Ikulu Chamwino mkoani Dodoma tarehe 26 Julai, 2025.

Afisa Elimu Dar apongeza umahiri lugha ya kifaransa St Anne Marie Academy

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imeahidi kuendelea kushirikiana na sekta binafsi katika elimu huku ikiipongeza shule ya St Anne Marie Academy ya jijini Dar es Salaam kwa kufanya vizuri kwenye matokeo ya mitihani ya kitaifa. Pongezi hizo zimetolewa leo jijini Dar es Salaam na Afisa Elimu wa Mkoa wa Dar es Salaam Gift Kyando wakati wa mahafali ya darasa la saba yaliyofanyika kwenye viwanja vya shule hiyo Mbezi Kimara kwa Msuguri. Alisema amefurahishwa na mazingira mazuri ya shule  baada ya kutembelea maeneo mbalimbali ya shule hiyo na kuridhishwa pia na namna maktaba zilivyoboreshwa na kuwekwa vitabu vya kila aina kuwawezesha wanafunzi kupata maarifa wanayotaka. “Waswahili wanasema tembea uone, mimi leo nimejionea mwenyewe kwa macho yangu namna St Anne Marie Academy  ilivyoboresha mazingira ya shule kwa kupanda miti ya kutosha, bustani za mboga mboga na matunda kiasi kwamba mnajitosheleza wenyewe kwa mboga mboga na matunda, naomba wengine nao waige kutoka kwenu,” alisema Alimpongeza ...