Mbunge wa Jimbo la Serengeti, Mhe. Mary Daniel Surati, amewahimiza wanafunzi kuendelea kusoma kwa bidii, kuweka malengo makubwa na kutumia fursa za elimu kujijengea msingi imara wa maisha na maendeleo ya jamii. Mhe. Surati ameyasema hayo aliposhiriki Usiku wa Tuzo kwa Wadau wa Elimu uliofanyika katika Shule ya Sekondari Manga wilayani Tarime, ambapo hafla hiyo iliambatana na utoaji wa tuzo kwa wanafunzi waliofanya vizuri katika masomo. Hafla hiyo imekuwa sehemu ya kutambua na kuenzi juhudi za wanafunzi walioonesha umahiri katika masomo, huku ikiwahamasisha wengine kuongeza bidii ili kufikia mafanikio makubwa zaidi kitaaluma. Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Surati amesema amefurahishwa na jitihada zinazofanywa na wanafunzi, walimu, wazazi pamoja na wadau mbalimbali wa elimu katika kuhakikisha wanafunzi wanapata mazingira yanayowawezesha kufanya vizuri na kutimiza ndoto zao. Amesema mafanikio ya mwanafunzi hayajengwi na juhudi za mtu mmoja pekee, bali yanahitaji ushirikiano wa k...
Marato tv - Sauti ya Jamii