Skip to main content

Posts

Showing posts from May 11, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Safari Mpya za Brussels–Kilimanjaro Kufungua Fursa za Utalii na Biashara

  Na Mwandishi Wetu, BRUSSELS KAMPUNI ya ndege ya Brussels Airlines ya nchini Ubelgiji imeandika historia mpya kwa kutangaza kuanza kwa safari za moja kwa moja kati ya Brussels nchini Belgium na Kilimanjaro International Airport kuanzia Juni 3, 2026.  Kwa mujibu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, safari hizo zitafanyika mara mbili kwa wiki, kila Jumatano na Jumamosi, hatua inayotajwa kuwa chachu mpya kwa sekta ya usafiri wa anga, biashara na utalii nchini Tanzania.  Uzinduzi wa safari hizi unaonekana kufungua ukurasa mpya wa ushirikiano wa kiuchumi kati ya Tanzania na Ubelgiji huku ukirahisisha usafiri kwa watalii, wafanyabiashara na wananchi wa pande zote mbili. Kuanzishwa kwa safari hizi za moja kwa moja kunatarajiwa kuongeza ushindani wa huduma za usafiri wa anga kwa kupunguza muda wa safari na kutoa chaguo zaidi kwa abiria wanaosafiri kati ya Afrika Mashariki na Ulaya.  Aidha, hatua hiyo inatajwa kuwa muhimu katika kukuza biashara ya ki...

Rais Samia Awasili Nchini Uganda

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Naibu Waziri Mkuu wa Tatu wa Uganda Mhe. Rukia Isaya Nakadama mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Entebbe nchini humo tarehe 12 Mei, 2026. Rais Dkt. Samia amewasili nchini Uganda kwa ajili ya kuhudhuria Sherehe za Uapisho wa Rais Mteule nchi hiyo, Mhe. Yoweri Kaguta Museveni, zitakazofanyika katika Viwanja vya Kololo Jijini Kampala nchini humo.

Waziri Nyansaho afanya Mazungumzo na Ujumbe wa Kijeshi kutoka Algeria

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Rhimo Nyansaho (kulia pichani juu), jana Mei 11, 2026 alikutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa Jeshi la Algeria ukiongozwa na Brigedia Jenerali Abbas Ibrahim. Mazungumzo hayo ambayo yalifanyika kwenye ofisi ndogo za Wizara hiyo, Upanga jijini Dar es Salaaam, yalijikita katika kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Algeria katika masuala ya ulinzi, usalama na mafunzo ya kijeshi. Brigedia Jenerali Abbas alitumia fursa hiyo kumfikishia Waziri Nyansaho salamu kutoka kwa Waziri wa Ulinzi wa Algeria na Rais wa Jamhuri ya Algeria, Abdelmadjid Tebboune, ambaye ameipongeza Serikali ya Tanzania inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendeleza amani na utulivu, na kuifanya nchi kuwa kisiwa cha amani. Aidha, Brigedia Jenerali Abbas alimueleza Waziri Nyansaho kuwa nchi ya Algeria inajivunia mahusiano ya muda mrefu na kihistoria kati ya nchi hizo mbili. Mazungumzo hayo kati ya Waziri Nyansaho na Uju...

Imani Potofu Zimeua Wengi -Mtaka

Mkuu wa Mkoa wa Njombe Anthony Mtaka amewata wananchi mkoani humo kuachana na imani potofu za kutokupeleka wagonjwa hospitali na kuishia kwa waganga wa kienyeji. Amesema zama hizo zimepitwa na wakati kwani kwa sasa teknolojia imekuwa na huduma za afya zimeboreshwa nchini kwa kuwa na vifaa tiba vya kisasa. Mtaka Ameyasema hayo mkoani Njombe alipokuwa akizindua kambi ya siku 21 ambayo itatoa huduma ya vipimo mbalimbali bure kwa kila mwananchi atakayefika katika kambi hiyo “Unakuta mtu amepata ugonjwa wa kiharusi au sukari badala ya kwenda kwenye vipimo anakimbilia kwa mganga wa kienyeji ambako hawezi kupata huduma inayotakiwa na ugonjwa unaendelea kuwa sugu mwisho wa siku anakufa” amesema Mtaka

Mahera Aipongeza Mageuzi Makubwa Sekta ya afya

MBUNGE wa Jimbo la Butiama, Mhe. Dkt. Charles Mahera ameipongeza Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji mkubwa uliofanyika katika sekta ya afya nchini kuanzia huduma za msingi hadi hospitali za rufaa. Akichangia Bajeti ya Wizara ya Afya jana Mei 11, 2026 Bungeni jijini Dodoma, Dkt. Mahera amesema Serikali imefanya mapinduzi makubwa katika utoaji wa huduma za afya kupitia ujenzi wa zahanati, vituo vya afya, hospitali za wilaya pamoja na ununuzi wa vifaa tiba vya kisasa. “Kabla sijasahau, kwa sababu ya utendaji mzuri wa Waziri wa Afya, ninaunga mkono hoja hii kwa asilimia mia moja,” amesema Dkt. Mahera. Amesema mfumo wa huduma za afya nchini umeendelea kuimarika tangu mwaka 2021 baada ya Serikali kuongeza uwekezaji mkubwa katika sekta hiyo, jambo lililowezesha wananchi wengi kupata huduma bora karibu na maeneo yao. Dkt. Mahera amesema vifaa vya kisasa kama Digital X-Ray, Ultrasound na CT-Scan vilivyosambazwa katika hospitali mbalimbali vimeongeza ubora ...

Rais Samia Mgeni Rasmi Siku ya Mazingira Juni 5

Na Mwandishi Wetu RAIS Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye kilele cha siku ya mazingira duniani yatakayofanyika Juni 5 katika ukumbi wa Jakaya Kikwete mkoani Dodoma. Hayo yalisemwa jana jijini Dar es Salaam na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Hamad Yusuph Masauni alipoongea na waandishi wa habari wakati akitoa tamko la siku ya mazingira duniani. Alitaja baadhi ya mambo yatakayofanyika kuwa ni  pamoja na uzinduzi wa program ya mageuzi ya kimkakati inayohusu mazingira endelevu 2025-2030 ambayo ni nyenzo utekelezaji wa Dira 2050. Alisema pia kutakuwa na kongamano kubwa linalotarajiwa kuwashirikisha watu zaidi ya 1,000 kutoka ndani na nje ya nchi na kampuni zaidi ya 100 zitashiriki kwenye maonesho wakati wa kongamano hilo. Alisema katika shamra shamra za kuelekea kilele cha siku ya mazingira serikali   inatarajia kuzindua mpango mkakati maalum wa mazingira utakaotekelezwa kuanzia mwaka 2026 hadi 2030 katika  kukabiliana na ...

Tànzania kuendelea kutumia akili unde katika Kukabiliana na maafa

Na Mwandishi Wetu, Masvingo - Zimbabwe TANZANIA imesema itaendelea kutumia teknolojia ya Akili Unde (AI) katika kuimarisha mifumo ya usimamizi wa maafa nchini ili kuongeza ufanisi wa utoaji wa tahadhari za mapema na kupunguza madhara yanayosababishwa na majanga mbalimbali. Hayo yameelezwa na Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, Dkt. Jim Yonazi, wakati wa mkutano wa maandalizi ya Mkutano wa Sita wa Kawaida wa Kamati ya Mawaziri Wanaohusika na Usimamizi wa Maafa kwa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) uliofanyika Mei 11, 2026 mjini Masvingo, Zimbabwe. Alisema matumizi ya AI yatasaidia uchakataji na ufuatiliaji wa taarifa mbalimbali zinazoripotiwa kuhusu masuala ya maafa nchini, hatua inayolenga kuongeza uwezo wa Serikali katika kufanya maamuzi ya haraka wakati wa majanga. “Matumizi ya teknolojia ya Akili Unde yatawezesha uchambuzi wa taarifa kwa haraka, kutabiri hatari zinazoweza kujitokeza na k...

Mlezi Chama cha mafundi Mkoa wa Tanga apatikana

Na Mwanamkuu Mwandoro,Tanga . CHAMA cha Mafundi Tanga (CMT)kufuatia juhudi zake za kupiga vita vilainishi visivyo faa(vilainishi feki) kimefanikiwa kuungwa mkono na Mbunge wa jimbo la Tanga Kassim Mbaraka na kuahidi kuwa mlezi wao na kiwasaidia. Mbaraka amefikia maamuzi hayo ikiwa lengo ni kuunga mkono kauli ya waziri wa viwanda na biashara inayotaka kutokomeza bidhaa feki hasa za vilainishi visivyo faa (oil feki). Nae Mkurugenzi wa S.S.M.C Limited ambaye pia ni kiongozi wa Chama cha Mafundi TANGA(CMT) Bw. Said Selemani Mohamed maarufu(Said Kijiko) amesema wao Kwa umoja wao wamempokea Kwa faraha mlezi huyo. Aidha Kijiko ameongeza kuwa kufuatia uwepo wa kiwanda cha MOGAS Tanga ni vema wananchi wakatumia bidhaa kutoka huko ili kulinda mashine zao kudumu Kwa muda mrefu na kuepuka gharama zinazo epukika. Sambamba na hayo CMT wamejipanga kutoa elimi Kwa wananchi ili kuwaongezea uelewa wa namna ya kugundua vilainishi visivyo faa na vinavyofaa.

Taulo za kike kuongeza ufaulu Kwa Wanafunzi Misungwi

Kaimu Mkurugenzi wa Wilaya ya Misungwi Bw.Christopher Legonda ameongoza Zoezi La Ugawaji wa Taulo za Kike zilizo nunuliwa na Halmashauri ya Wilaya Kupitia Mapato ya Ndani ya Halmashauri kwa Lengo la Kuongeza Ufaulu kwa Wanafunzi mapema leo tarehe 11/05/2026 katika Viwanja vya ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi. Amesisitiza kuwa Serikali Itaendelea Kuboresha Miundo Mbinu Mbalimbali Mashuleni Ikiwemo Vyumba vya Kujifunzia Ili Vikalete Tija Kwenye Ufaulu wa Wanafunzi pamoja na Kuendelea Kushilikiana na Wadau Mbalimbali wa Maendeleo Wilayani Misungwi. Kwa Upande wake Afisa Elimu Makundi Maalumu Wilaya ya Misungwi Ndugu.Felician Malongo amewaomba Wadau Mbalimbali Kujitokeza Kuunga Mkono Jitihada Mbalimbali za Serikali Kwenye Elimu ikiwemo Hedhi Salama na Mazingira rafiki. Naye Mwanafunzi wa Misungwi Sekondari Ms Sara Cretus amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dk.Samia Suluhu Hassan Kwa Jitihada Mbalimbali anazochukua Kwenye Sekta ya Elimu Ikiwemo kuboresha  M...

Tiba asili yapata Heshima Mpya serikalini,Dkt.Eyembe Aipongeza Serikali

  MGANGA Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tabora (Kitete), Dkt. Joackim Eyembe, amepongeza hatua ya Serikali kuendelea kuitambua na kuipa nguvu huduma ya tiba asili na tiba mbadala kupitia Bajeti ya Wizara ya Afya ya mwaka wa fedha 2026/2027, akisema hatua hiyo ni mwanzo wa mapinduzi makubwa katika sekta ya afya nchini. Akizungumza katika Viwanja vya Bunge  kufuatia hotuba ya Bajeti iliyowasilishwa Bungeni jijini Dodoma na Waziri wa Afya Mohamed Mchengerwa Mei 11, 2026, Dkt. Lyembe amesema tiba asili imekuwa msaada mkubwa kwa jamii tangu zamani kabla ya uwepo wa hospitali kubwa za kisasa. “Tulikuwa tunaamini tiba nyingi zinapatikana hospitalini pekee, lakini ukweli ni kwamba hata kabla ya kuwepo kwa hospitali hizi kubwa za rufaa, tiba za asili zilikuwepo na ziliwasaidia wananchi wengi,” amesema Dkt. Eyembe. Amesema uamuzi wa Serikali kuunganisha wataalamu wa afya na watoa tiba asili ni hatua muhimu itakayosaidia kuhakikisha huduma zinazotolewa zinakuwa salama, bora na...

Tanzania yahimiza Mageuzi ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imehimiza mageuzi katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ili kuendana na hali halisi ya siasa za Ulimwengu ya sasa, huku ikisisitiza kuwa itakuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha chombo hicho kinakuwa na uwakilishi mpana, uwazi, na uwajibikaji zaidi kwa mataifa yote. Hayo yameelezwa 11 Mei, 2026 na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, anayeshughulikia Masuala ya Afrika Mashariki Mhe. James  Millya (Mb.), wakati wa Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje kuhusu Mageuzi ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa uliofanyika pembezoni mwa Mkutano wa "Africa Forward Summit" unaondelea Jijini Nairobi, Kenya . Mkutano huo umeongozwa na  Waziri wa Mambo ya Nje  wa Ufaransa Mhe. Jean-Noël Barrot  na Waziri wa Mambo ya Nje  na Uhusiano wa Kimataifa wa Kenya Mhe. Musalia Mudavadi.  Aidha, Mhe. Millya alikumbushia msisitizo uliotolewa na Makamu wa Rais Mstaafu, Mhe. Dkt. Philip Mpango,  wak...