Skip to main content

Posts

Showing posts from May 20, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Miradi ya Chuma Njombe Kutikisa Uchumi, Maelfu ya Ajira Kunukia Ludewa

📍Njombe MKOA  wa Njombe unatarajiwa kuwa kitovu kipya cha uchumi wa madini nchini kufuatia uwekezaji mkubwa katika miradi ya uchimbaji na uchakataji wa madini ya chuma inayolenga kufungua maelfu ya ajira, kukuza biashara za ndani na kuongeza mapato kwa wananchi wa Wilaya ya Ludewa. Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Njombe, Mhandisi Lucas Mlekwa, amesema tayari moja ya miradi mikubwa inayosimamiwa na Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) kwa kushirikiana na kampuni ya kigeni imepata Leseni Kubwa ya Uchimbaji wa Madini baada ya utafiti wa kina uliofanyika kati ya mwaka 2012 na 2013 kubaini uwepo wa zaidi ya tani milioni 126 za madini ya chuma. Amesema tafiti hizo pia zimeonesha uwepo wa madini mengine yenye thamani kubwa yanayoambatana na chuma ikiwemo titanium na vanadium, hatua inayoongeza thamani ya kiuchumi ya mradi huo kwa Taifa. “Kwa sasa tupo katika hatua za mwisho za kukamilisha makubaliano kati ya Serikali na wawekezaji, na tunatarajia ndani ya mwaka mmoja utekelezaji rasmi wa mr...

Waziri wa Ulinzi na Jkt Akutana na Wakuu wa Mikoa ya Mipakani Kuimarisha Ulinzi na Usalama wa Taifa

WAZIRI wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mheshimiwa Dkt. Rhimo Nyansaho (Mb), amefanya mazungumzo na Wakuu wa Mikoa sita ya mipakani nchini katika kikao kilichofanyika tarehe 20 Mei 2026, Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa, Kikombo – Dodoma, kikilenga kuimarisha mikakati ya pamoja ya ulinzi na usalama wa mipaka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kikao hicho kimewakutanisha viongozi wa mikoa ya kimkakati inayopakana na mataifa jirani, ambapo walijadili kwa kina masuala ya usalama wa mipaka, udhibiti wa changamoto za kiusalama, pamoja na kuongeza ushirikiano kati ya taasisi za ulinzi na uongozi wa mikoa katika kuhakikisha amani na utulivu vinaendelea kudumu. Wakuu wa Mikoa waliohudhuria ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. CPA Amos Makalla; Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Balozi Batilda Burian; Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mhe. Kanali Evans Mtambi; Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Jabir Makame; Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Mhe. Kanali Yahya Kido; pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Mhe. Kanali Donald Msengi. Akizu...

Waziri Mkuu Atatua Mgogoro wa Ardhi Uliodumu Kwa Miaka 51 Wilayani Rombo

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba ametatua mgogoro wa ardhi kati ya Parokia ya Mtimhoo ya Kanisa Katoliki Jimbo la Moshi na Mzee Peter Morisi wa Kijiji cha Msaranga, Wilaya ya Rombo Mkoa wa Kilimanjaro, uliodumu kwa kipindi cha miaka 51. Mheshimiwa Waziri Mkuu alipokea malalamiko ya Mzee Peter Morisi alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Halmashauri ya Wilaya ya Rombo wakati wa ziara yake ya kikazi mkoani Kilimanjaro tarehe 17 Februari 2026 ambapo aliahidi kuwa Serikali ingetuma wataalamu wilayani humo kwa ajili ya kuchunguza na kutatua mgogoro huo. Kufuatia maelekezo hayo, Waziri Mkuu alituma timu ya wataalamu kutoka Ofisi yake ambao walifika mkoani Kilimanjaro na kushirikiana na viongozi wa Mkoa pamoja na viongozi wa Kijiji cha Msaranga kutembelea eneo la mgogoro. Aidha, timu hiyo ilifanya vikao na familia iliyokuwa katika mgogoro, viongozi wa kijiji, viongozi wa Parokia ya Mtimhoo pamoja na viongozi wa Jimbo Katoliki la Moshi ambapo pande zote ziliku...

Serikali Yaongeza Nguvu Ushiriki wa Wanawake Katika Miradi ya Barabara

WAZIRI wa Ujenzi, Abdallah Ulega amesema Serikali inaendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuimarisha ushiriki wa wanawake katika utekelezaji wa miradi ya barabara nchini, ikiwa ni sehemu ya kuhakikisha wanawake wanapata nafasi zaidi katika sekta ya ujenzi na miundombinu. Akiwasilisha bungeni jijini Dodoma makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Ujenzi kwa mwaka wa fedha 2026/2027 leo Mei 20, 2026, Ulega amesema kupitia Kitengo cha Ushirikishwaji wa Wanawake, Wizara imeendelea kufanya maboresho ya kanzidata maalum inayohifadhi na kufuatilia taarifa za ushiriki wa wanawake katika miradi ya barabara ili kuongeza ufanisi wa usimamizi na ufuatiliaji. Amesema sambamba na hatua hiyo, Serikali imeendelea kuboresha mwongozo wa ushirikishwaji wa wanawake katika sekta ya ujenzi kwa lengo la kutoa mwelekeo sahihi kwa wadau wote kuhusu namna bora ya kuwawezesha wanawake kushiriki kikamilifu katika miradi ya maendeleo. “Kitengo pia kimeendelea kufanya ukaguzi wa kazi zinazotekelezwa na wakandar...

Wizara ya Ujenzi Yaomba Trilioni 2.564 Kwa Miradi ya Maendeleo na Miundombinu

Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega amewasilisha bungeni jijini Dodoma makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Ujenzi kwa mwaka wa fedha 2026/2027, ambapo wizara hiyo imeomba kuidhinishiwa jumla ya shilingi trilioni 2.564 kwa ajili ya matumizi ya kawaida na utekelezaji wa miradi ya maendeleo nchini. Akiwasilisha bajeti hiyo leo Mei 20, 2026, Ulega amesema fedha hizo zitalenga kuimarisha utekelezaji wa miradi ya miundombinu ya barabara ili kurahisisha usafirishaji wa watu na bidhaa, sambamba na kuchochea ukuaji wa uchumi wa taifa. Kwa mujibu wa makadirio hayo, jumla ya shilingi bilioni 97.1 zimetengwa kwa matumizi ya kawaida ya Wizara na taasisi zake, ambapo shilingi bilioni 92.2 zitatumika kulipa mishahara ya watumishi huku shilingi bilioni 4.8 zikielekezwa kwenye matumizi mengine ya uendeshaji. Aidha, shilingi trilioni 2.467 zimetengwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo, ambapo kati ya fedha hizo shilingi trilioni 1.544 ni fedha za ndani na shilingi bilioni 922.4 ni fedha za nje. Seri...

Ulega: Serikali Kuendelea na Miradi ya Flyovers na Barabara Kupunguza Msongamano wa Magari

Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega amesema Serikali itaendelea kutekeleza miradi mikubwa ya barabara na flyovers katika majiji na miji mbalimbali nchini kwa mwaka wa fedha 2026/2027, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha usafiri mijini na kupunguza msongamano wa magari. Akiwasilisha bajeti ya Wizara ya Ujenzi bungeni jijini Dodoma leo Mei 20, 2026, Ulega amesema miradi hiyo pia inalenga kuongeza tija ya kiuchumi, kurahisisha shughuli za usafirishaji na kuinua ubora wa maisha ya wananchi. Amesema miradi hiyo itatekelezwa katika majiji ya Dar es Salaam, Arusha, Mwanza, Mbeya na Dodoma pamoja na miji ya Pwani Region, Iringa na Singida. Kwa upande wa Dar es Salaam, Serikali itaendelea na ujenzi wa barabara pamoja na flyovers katika maeneo mbalimbali ili kupunguza adha ya foleni ambayo imekuwa ikichangia upotevu wa muda na kuchelewesha shughuli za kiuchumi. Katika Jiji la Dodoma, Serikali inaendelea na ujenzi wa barabara ya mzunguko wa nje yenye urefu wa kilometa 112.3 ambayo ipo katika hat...

DC Rorya aeleza hatua za kutatua changamoto za Kwibuse

RORYA.  Mkuu wa Wilaya ya Rorya Mkoani Mara, Dk. Khalfan Haule, amesema serikali itachukua hatua za haraka za muda mfupi na muda mrefu kukabiliana na changamoto za Barabara, maji, afya na nishati ya umeme zinazoikabili kijiji cha Kwibuse iliyoko Kata ya Kisumwa wilayani humo Dk. Haule ameyasema hayo baada ya kukagua uharibifu wa barabara ya Kuruya–Kwibuse–Marasibora, ambapo amesema kuwa sehemu ya barabara hiyo imekatika katika maeneo yenye makalavati matano mapya yaliyojengwa, hali iliyosababisha usumbufu mkubwa kwa wananchi na wasafiri. Amesema hatua za muda mfupi zitahusisha kujaza mawe na vifusi katika maeneo yote yaliyoathirika ili magari na wananchi waweze kuendelea kutumia barabara hiyo, huku serikali ikiandaa mpango wa matengenezo makubwa zaidi ya kudumu. “Mpango wa muda mrefu ni kunyanyua tuta la barabara hasa kwenye bonde la karibu na eneo la Kukona ili kuondoa kabisa tatizo hili,” alisema Dk. Haule alipokuwa akizungumza na wananchi wa Kwibuse katika mkutano wa hadhara. Ka...

Diwani Serengeti Asifu Ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa, Asema Utafungua Fursa Kubwa za Kiuchumi

DIWANI wa Kata ya Uwanja wa Ndege, Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti mkoani Mara, Matoke Joseph Michael, amesema wananchi wa eneo hilo wamepokea kwa furaha Bajeti ya Wizara ya Uchukuzi baada ya Serikali kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Serengeti, hatua inayotarajiwa kuleta mageuzi makubwa ya kiuchumi na kukuza sekta ya utalii. Amesema mradi huo ni matokeo ya dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuimarisha miundombinu ya uchukuzi na kufungua fursa za maendeleo kwa wananchi. Michael amesema uwanja huo ambao umekuwa ukisubiriwa kwa muda mrefu sasa umeanza kutekelezwa, na utachochea ukuaji wa ajira, biashara na kuongeza mapato yatokanayo na sekta ya utalii katika Wilaya ya Serengeti. Ameeleza kuwa uwanja huo utarahisisha usafiri wa watalii na kufanya Serengeti kuendelea kuwa moja ya maeneo muhimu ya kiuchumi duniani. Pia amewapongeza wananchi waliotoa maeneo kwa ajili ya mradi huo pamoja na wataalamu ...

Mwenyekiti Kitongoji cha Burunga Aipongeza Bajeti ya Wizara ya Uchukuzi, Ampongeza Rais Samia Kwa Mradi wa Kiwanja cha Ndege Serengeti

MWENYEKITI wa Kitongoji cha Burunga wilayani Serengeti mkoani Mara, James Makuru, ameipongeza Bajeti ya Wizara ya Uchukuzi kwa kuendelea kutoa kipaumbele katika utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Serengeti, huku akimpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, kwa uamuzi wa Serikali ya Awamu ya Sita wa kupeleka mradi huo mkubwa katika eneo la Burunga. Akizungumza baada ya kusikia maelezo ya bajeti hiyo, Makuru amesema wananchi wa Burunga na Wilaya ya Serengeti kwa ujumla wanaishukuru Serikali kwa kuona umuhimu wa kujengwa kwa kiwanja hicho ambacho kitafungua fursa nyingi za maendeleo kwa wananchi. “Hii ni fursa kubwa sana kwa wananchi wa Serengeti. Vijana wengi watapata ajira wakati wa ujenzi wa kiwanja hiki, lakini hata baada ya ujenzi kukamilika bado kutakuwa na nafasi nyingi za ajira hapa hapa kwenye uwanja wa ndege,” amesema James Makuru. Amesema mbali na ajira, mradi huo utaongeza shughuli za biashara kutokana na ongezeko...

Wananchi wa Kijiji Cha Burunga Wampongeza Rais Samia Kwa Mradi Wa Kiwanja Cha Ndege Cha Kimataifa Serengeti

WANANCHI wa kijiji cha Burunga wilayani Serengeti Mkoani Mara wamepongeza uamuzi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, wa kuidhinisha ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Serengeti, wakisema mradi huo utafungua ukurasa mpya wa maendeleo ya uchumi, biashara na ajira katika eneo hilo. Pongezi hizo zimekuja baada ya Serikali kupitia Bajeti ya Wizara ya Uchukuzi kueleza hatua mbalimbali za utekelezaji wa mradi huo mkubwa wa kimkakati unaotarajiwa kuongeza ukuaji wa sekta ya utalii nchini huku ukilinda mazingira ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti. Baadhi ya wakazi wa Burunga akiwemo Mzee Joseph Charles,Mboyi Mremi Mancha pamoja na Benjamini Jumanne Kairo, wamesema ujenzi wa kiwanja hicho ni neema kubwa kwa wananchi wa Serengeti kutokana na matarajio ya kuongezeka kwa watalii na shughuli za kiuchumi katika eneo hilo. Wamesema kukamilika kwa mradi huo kutatoa fursa nyingi za biashara kwa wananchi ikiwemo huduma za malazi, usafiri, biashara ndogo ndogo pamoja ...

Serikali Yasifiwa Ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa Serengeti, Wasema ni Mageuzi Makubwa ya Utalii na Uchumi

Mkuu wa Mkoa wa Mara, Kanali Evans Mtambi, ameipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Uchukuzi kwa hatua ya kihistoria ya ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Serengeti, akisema mradi huo ni ukombozi mkubwa kwa sekta ya utalii na uchumi wa taifa kwa ujumla. Amesema uamuzi huo ni matokeo ya maono ya muda mrefu ya wadau wa utalii, viongozi wa serikali pamoja na wananchi wa Mkoa wa Mara waliokuwa wakisisitiza umuhimu wa kuboreshwa kwa miundombinu ya usafiri katika eneo la Serengeti. Aidha, amesema uwanja mdogo uliopo Serengeti kwa sasa ni miongoni mwa viwanja vinavyotumika kwa wingi nchini, ambapo kwa baadhi ya siku hupokea takribani ndege mia moja mchana pekee, hali inayoonesha wazi uhitaji mkubwa wa uwanja wa kisasa wa kimataifa utakaoendana na hadhi ya eneo hilo. Mtambi ameongeza kuwa Serengeti ni hazina ya kipekee duniani, Urithi wa Dunia uliosajiliwa na UNESCO, na moja ya maeneo yanayovutia watalii kutoka kila pembe ya dunia kutokana na uhamaji wa ...