Skip to main content

Posts

Showing posts from March 28, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Makamu wa Rais Amwakilisha Rais Katika Mkutano Mkubwa Nchi za Afrika, Karibiani na Pasifiki (Oacps)

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, amemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa 11 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Nchi za Afrika, Karibiani na Pasifiki (OACPS), uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Sipopo kilichopo Jijini Malabo nchini Guinea ya Ikweta. Katika ufunguzi wa Mkutano huo, salamu za Viongozi mbalimbali zimesisitiza umuhimu wa hitaji la kufanya mageuzi ya Kitaasisi na kimfumo kuwezesha Jumuiya ya Nchi za Afrika, Karibiani na Pasifiki (OACPS) kukabiliana na changamoto zinazoikabili Dunia kwa sasa ikiwemo, migogoro ya kisiasa, vita pamoja na mabadiliko ya tabianchi. Vilevile, Ufunguzi wa Mkutano huo, umeweka mkazo kwa nchi wanachama kutoa michango kwa wakati ili kuifanya Taasisi ya OACPS kujitegemea kifedha na kuwa sauti huru kwenye jumuiya ya kimataifa. Pia msisitizo umewekwa katika kutumia vema rasilimali watu ambao ni bilioni 1.5 waliopo ...

Tanzania na China Wajadili Teknolojia Kuzuia Uhalifu

Serikali ya Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya China zimepanga kushirikiana katika masuala mbalimbali ya kuzuia Uhalifu ikiwemo mashirikiano katika Sekta ya Uchunguzi wa Uhalifu,Uhalifu wa Kimtandao(Cyber Crime)na suala nzima la kubadilishana watuhumiwa wa uhalifu baina ya Nchi hizo mbili. Hayo yamebainika wakati wa Kikao Kazi Kati ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mheshimiwa Patrobas Katambi na Balozi wa China nchini Tanzania,Chen Mingjian ambapo pia waliweka wazi mashirikiano hayo pia kuhusisha ubadilishanaji wa teknolojia mbalimbali za Kudhibiti Uhalifu katika maeneo muhimu. Kikao hicho kimefanyika Ofisi Ndogo ya waziri,jijini Dar es Salaam.

Ucsaf Yaendelea Kusaidia Ajenda ya Nishati Safi Kwa Wanawake Wajasiriamali

 KONDOA MFUKO wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) umeendelea kuunga mkono juhudi za Serikali ya Tanzania chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuhamasisha matumizi ya nishati safi na mbadala kwa wananchi, hususan wanawake wajasiriamali nchini. Kupitia mpango huo, UCSAF imegawa Majiko ya Gesi 50 Kwa wanawake Wajasiriamali katika wilaya ya Kondoa Kwa lengo la kupunguza matumizi ya mkaa na kuni ambayo kwa muda mrefu yamekuwa yakichangia uharibifu wa mazingira pamoja na athari za kiafya. Akizungumzia katika Hafla ya Ugawaji wa Mitungi Kwa Wanawake Wajasiriamali katika Wilaya ya Kondoa, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira wa Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa, Ramadhan Hamis, amesema Mitungi hiyo ya Gesi  iliyotolewa na Mfuko wa Mawasiliano Kwa wote  itawasaidia wanawake hao kufanya shughuli zao za uzalishaji kwa ufanisi zaidi, salama na kwa gharama nafuu. “Hapo awali ilikuwa ni vigumu kwa wananchi kubadili mazoea. Lakini sasa elimu imeeleweka ...

Naibu Waziri Ampongeza Mwekezaji Mzalendo Hospitali ya E.M

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Afya, Dk Florence Samizi amewataka watanzania kuwekeza kwenye miundombinu ya afya ili kusogeza huduma za matibabu karibu na wananchi. Naibu Waziri ameipongeza hospitali ya E.M ya Kigamboni kwa uwekezaji mkubwa iliyofanya kwenye mtambo wa kisasa wa uchunguzi wa magonjwa CT SCAN na huduma za usafishaji wa damu (Dialysisi) ambao unasaidia kupunguza rufaa zisizo za lazima. Alitoa pongezi hizo jana Dar es Salaam na wakati wa uzinduzi rasmi wa mashine ya kusafisha damu na mashine ya uchunguzi wa afya CT SCAT ya hospitali hiyo iliyoko kata ya Mjimwema Kigamboni. Alisema uwekezaji kama huo unasaidia jitihada za serikali kupeleka huduma karibu na wananchi na kuepusha muda na gharama za wananchi kufuata huduma hizo maeneo ya mbali na maeneo wanakoishi. “Kwaniaba ya Waziri wa Afya Mohamed Mchengerwa napenda kuwapongeza kwa dhati kabisa kwa uwekezaji huu, nilipofika pale nje nilimwambia msaizidi wangu kumbe kitu chenyewe ni kikubwa hivi, nawapongeza sana kwa uongo...

Tanzania na Israel Zaimarisha Ushirikiano Katika Sekta za Kilimo na Afya

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imesema Israel imekuwa mshirika muhimu katika sekta mbalimbali nchini, ikiwemo kilimo, afya, ulinzi na usalama, hali inayochangia kuimarika kwa ushirikiano wa muda mrefu kati ya nchi hizo mbili. Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.), amesema hayo katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam, wakati akipokea nakala za hati za utambulisho za Balozi Mteule wa Israel nchini, Mheshimiwa Gideon Behar, mwenye makazi yake jijini Nairobi, Kenya. Mhe. Kombo amempongeza Balozi Behar kwa uteuzi wake na kumhakikishia ushirikiano wa kutosha kutoka Serikalini katika kipindi chote cha utumishi wake nchini. Aidha, ameipongeza programu ya MASHAV ya Israel inayotoa mafunzo ya vitendo kwa vijana wa Kitanzania kwenye mashamba nchini humo, na kupendekeza wataalamu wa Israel kuja kufundisha moja kwa moja katika vyuo vya kilimo nchini, ikiwemo Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA). Amebainisha ...

Mkalipa: Ccm Tuna Deni la Kuwaletea Maendeleo Wananchi

Na: Mwandishi Wetu, Pangani Chama Cha Mapinduzi (CCM) kina deni la kuwaletea maendelea wananchi kutokana na imani kubwa waliyonayo wananchi kwa Chama hicho.  Hayo yameelezwa na Katibu wa Umoja wa Vijana CCM (UVCCM) wilaya ya Pangani, Nasri Mkalipa, Machi 27, 2026, katika ziara yake ya ujenzi wa Chama katika Kata za Bushiri na Masaika. Mkalipa amesema CCM iliomba ridhaa kwa wananchi na wananchi wakaichagua wakiamini yale waliyoahidi yatafanyiwa kazi, hivyo Chama kitaisimamia serikali kuhakikisha ahadi zote zinatekelezwa. "Ndugu vijana wenzangu, tuendelee kuiunga mkono CCM, na jukumu letu ni kuwapa wananchi maendeleo. Rais wetu Dk. Samia Suluhu Hassan, Mbunge wetu Jumaa Hamidu Aweso na wadiwami wote wanapambana kuhakikisha changamoto za wananchi zinatatuliwa," amesema Mkalipa.  Sanjari na hilo, Mkalipa amehimiza umuhimu wa vijana kushawishi vijana wenzao kujiunga na CCM na wapate kadi za kieletroniki ili watambuliwe Chamani.  Aidha, Mkalipa amewahimiza vijana kujitokeza kuc...