Skip to main content

Posts

Showing posts from March 17, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Majaliwa Atoa ya Moyoni Kuhusu Hayati John Pombe Magufuli

 WAZIRI Mkuu mstaafu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amemuelezea Hayati Rais John Magufuli kuwa ni mtu mkali, ambaye hakupenda mzaha katika mambo yake, alikuwa mchpakazi, Mzalendo na alikuwa kiongozi Mwenye akili nyingi katika kutekeleza Majukumu yake kiufasaha. Amesema Uzalendo unajengwa Kwa unajengwa na uwajibikaji.  Waziri Mkuu Mstaafu kasimu Majaliwa ameyasema hayo leo katika kumbukizi ya miaka mitano ya kifo cha Hayati rais Dk.John Magufuli Machi 17 katika viwanja vya makazi yake Chato mkoani Geita, Majaliwa amewataka Watanzania kuiga mambo mazuri yaliyofanywa na kiongozi huyo. Amesema yeye alikuwa ni mtu mkweli, hakuwa na mzaha katika mambo yake yaani mkali , alikemea maovu, wezi, wala rushwa, wabadhirifu wa mali za umma, na yule ambaye hakufuata misingi hii aliachana nae huo ndiyo ulikuwa utaratibu wake “Leo hii tunamkumbuka Hayati Magufuli, sisi ambao tulikuwa karibu naye tumeweza kushuhudia wakinufaika na busara zake, hekima zake katika kuongoza taifa hili, na kutambua r...

Mkutano wa Cti, Mawaziri Dar Waibua Changamoto za Kikodi

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imeahidi kuwa katika bajeti ya mwaka huu itazifanyia kazi changamoto za kikodi zinazolalamikiwa na wafanyabiashara na wenye viwanda kama mkakati wa kuendelea kuvutia uwekezaji wa ndani na kutoka nje ya nchi. Ahadi hiyo ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Naibu Waziri wa Fedha, Laurent Luswetula, wakati wa kikao na wanachama wa Shirikisho la Wenye Viwanda (CTI) kilichoangalia changamoto za kikodi na mafanikio ya wenye viwanda. Alisema nia ya serikali ni kuona wafanyabiashara na wenye viwanda wanafanyakazi kwenye mazingira mazuri zaidi yatakayowafanya wazidi kuongeza uzalishaji. “Serikali inatambua umuhimu wenu kwenye ukuaji wa uchumi kwa hiyo kwenye bajeti ijayo itazingatia sana maombi na ushauri wenu kuhusu masuala mbalimbali ya kikodi, sote tunajenga nyumba moja” alisema “Kama mlivyofanya mwaka jana, mwaka huu pia mmetuletea mapendekezo mengine na yale ya mwaka jana kwa asilimia zaidi ya 60 serikali iliyafanyia kazi hii inaonyesha ni jinsi gani ninyi mliv...

Dcp Mutafungwa: Toeni Huduma Bora Kwa Wananchi Siyo Bora Huduma

​Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Wilbrod Mutafungwa, amewakumbusha Maafisa, Wakaguzi na Askari wa vyeo mbalimbali mkoani humo, kuhakikisha wanatoa huduma bora kwa wateja na siyo bora huduma. ​Agizo hilo limetolewa wakati wa Baraza la Kamanda wa Polisi Mkoa lililowakutanisha Wakuu wa Polisi wa Wilaya (OCDs), Wakuu wa Vikosi, Waratibu Polisi jamii wilaya, Wakaguzi wa Kata, pamoja na askari wa vyeo mbalimbali kwa lengo la kufanya tathmini ya utendaji kazi na nidhamu. ​Akizungumza katika baraza hilo, DCP Mutafungwa amesisitiza kuwa mteja wa ndani na nje wa Jeshi la Polisi anapaswa kuhudumiwa kwa weledi na heshima, jambo ambalo ni nguzo muhimu katika kuimarisha ushirikiano kati ya Polisi na jamii. ​"Ni lazima tujikite katika kutoa huduma bora na siyo 'bora huduma'. Katika usimamizi wa sheria, hususan usalama barabarani, tujikite zaidi kutoa elimu na maonyo kwa makosa yanayorekebishika kuliko kukimbilia kuchukua hatua za kisheria kila wakati. Kau...

Kamati ya bunge yaridhishwa mradi wa maji wa hatifungani

Na MASHAKA MHANDO, Tanga KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira imeeleza kuridhishwa na maendeleo ya utekelezaji wa mradi wa maji wa Hatifungani ya Kijani (Green Bond) wenye thamani ya Shilingi Bilioni 53.3, unaolenga kumaliza kero ya upatikanaji wa huduma hiyo kwa wakazi wa Jiji la Tanga na wilaya jirani. Akizungumza jana wakati wa ziara ya kukagua miradi inayotekelezwa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Tanga (Tanga UWASA), Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Jackson Kiswaga, amesema ujenzi huo umefikia asilimia 65 na unatarajiwa kukamilika ifikapo Oktoba mwaka huu. Mhe. Kiswaga amempongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuruhusu ushiriki wa sekta binafsi katika uzalishaji wa maji, huku akiitaka Wizara ya Maji kuhakikisha wakandarasi wanalipwa kwa wakati ili wasikwamishe kasi ya ujenzi. "Tunamshukuru Rais kwa kutoa Shilingi Bilioni 35 kwa ajili ya mradi wa Mkinga-Horohoro kupitia fedha za ndani. Kamati inataka kuona mradi huu unakamilika kwa wakati ili ifikapo m...

Makamu wa Rais Dkt Emmanuel Nchimbi, Aongoza Kumbukizi ya Miaka Mitano ya Kifo Cha Hayati Dkt. John Magufuli

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kumbukizi ya miaka mitano ya kifo cha aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, iliyofanyika Kilimani, Chato mkoani Geita. Akitoa salamu za Serikali, Makamu wa Rais amesema ili kumuezi Hayati Magufuli kwa vitendo ni vema kila Mtanzania kujifunza wito kwa kujitoa na kufanya kazi kwa bidii. Amesema Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, aliyejitambulisha kwa Falsafa yake ya “Hapa Kazi tu”, alitaka kila mtu kujituma na kutoa mchango wake kwa Taifa kwa njia ya kazi.  Aliamini kuwa hiyo ndiyo njia pekee inayoweza kuondoa umaskini, katika ngazi ya mtu mmoja mmoja, kaya na hata Taifa kwa ujumla. Makamu wa Rais amesema katika uongozi, funzo kutoka kwa Hayati Dkt. John Pombe Magufuli ni ujasiri na uthubutu wake katika kufanya maamuzi magumu na yenye manufaa kwa ...