Na OWM - TAMISEMI, GEITA Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu -TAMISEMI Mhe. Prof. Riziki Shemdoe ameelekeza Maafisa Lishe na Maendeleo ya Jamii wanaosimamia utekelezaji wa Mradi Jumuishi wa Lishe katika Mkoa wa Geita, Tabora na Iringa kupatiwa vyombo vya usafiri ili waweze kwenda kutoa huduma kwenye maeneo yanayokabiliwa na matatizo ya lishe kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano. Prof. Shemdoe ametoa maelelezo hayo leo Machi 03, 2026, wakati akizindua Mradi Jumuishi wa Lishe katika Mkoa wa Geita, ambao utawawezesha watoto wa mkoa wa Geita kukua vizuri kimwili na kiakili, na kuwa na nguvu na afya bora. “Katibu Mkuu na wataalam mnaosimamia mradi huu, hakikisheni kupitia bajeti za mradi mnawapatia Maafisa Lishe na Maendeleo ya Jamii vyombo vya usafiri katika halmashauri zote zinazotekeleza mradi huu ili waweze kutoka sehemu moja kwenda nyingine kuwahudumia watoto,” amesisitiza Prof. Shemdoe. Prof. Shemdoe amesema, kipekee anashukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa...
Marato tv - Sauti ya Jamii