Skip to main content

Posts

Showing posts from December 17, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

REA Kusambaza Mitungi ya Gesi 26,040 Kwa bei ya Ruzuku Mkoani Mwanza

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unaendelea kutekeleza Mradi wa usambazaji wa mitungi ya gesi ya kilo 6 kwa bei ya ruzuku, ambapo inatarajia kugawa mitungi 26,040 katika mkoa wa Tanga, Mradi huo utagharimu jumla ya shilingi milioni 455. Mkuu wa mkoa wa Tanga, Mhe. Balozi, Dkt. Batilda Burian, tarehe 17 Desemba, 2024 ameupokea rasmi Mradi huo wa kusambaza mitungi ya gesi kwa Wananchi wa mkoa wa Tanga, ambapo mkoa unataraji kuanza zoezi la kusambaza mitungi hiyo kwa Wananchi mwezi Januari, 2025. REA, iliingia mkataba na mtoa huduma; kampuni ya Manjis Logistic Ltd, kampuni ambayo, itahudumia wilaya 8 za Mkoa wa Tanga kwa kuuza mitungi hiyo ya gesi ya kilo 6 kwa bei ya ruzuku ya shilingi 17,500 pamoja na vifaa vyake, katika maeneo ya vijijini na pembezoni mwa miji. Mhe. Balozi, Dkt. Batilda Burian, amewaomba REA kuhakikisha kuwa teknolojia za nishati safi ya kupikia, zinapatikana kwa wakati na kuwafikia Wananchi muda wote ili kuhakikisha matumizi ya nishati safi yanakuwa endelevu.  Mku...

Maisha Jela kwa Kosa la Kumlawiti Mtoto Mwenye Umri wa Miaka Minne

Mkazi wa kitongoji cha Mwankuba, kijiji cha Nyambiti, Wilaya ya Kwimba, mkoani Mwanza, Mashauri Ng'oga Shauri (20)  amehukumiwa kifungo cha maisha baada ya kukutwa na hatia ya kumlawiti mtoto wa miaka minne ambaye jina tunalihifadhi kwa sababu za kisheria, mkazi wa kijiji cha Nyambiti ambaye ni ndugu wa mshtakiwa ambaye ni mtoto wa baba yake mdogo. Hukumu hiyo imesomwa leo Disemba 17, 2024 kitika shauri la jinai namba 31963 la mwaka 2024 na Hakimu mkazi mwandamizi wa Mahakama ya wilaya ya Kwimba John Jagadi mbele ya mwendesha mashtaka wa Serikali Juma Kiparo. Kwa mujibu wa hati ya mashtaka kama ilivyosomwa na mwendesha mashtaka wa Serikali Juma Kiparo, mshtakiwa alitenda kosa hilo mnamo tarehe 27.10.2024 huko katika kijiji cha Nyambiti, kilichopo wilaya ya Kwimba na mkoa wa Mwanza kinyume na kifungu cha 154(1) (a) na (2) cha Kanuni ya Adhabu sura namba 16 ya sheria marejeo ya mwaka 2022. Mtuhumiwa alifikishwa mahakamani tarehe 11.11.2024 na kusomewa shitaka la kulawiti na siku hiyo...

Wapiga Ramli Chonganishi Mwanza Kusakwa

Jeshi la polisi mkoa wa Mwanza limedhamiria kufanya operesheni kali ya kubaini na kukamata watu wanaofanya ramli chonganishi na kuchochea uhalifu ikiwemo mauaji yatokanayo na imani za ushirikina. Hayo yamebainishwa  na kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Wilbrod Mutafugwa wakati wa kikao kazi na waganga, wakunga wa tiba asilia pamoja, maafisa wa wanayapori (TAWA) na wadau mbalimbali kilichofanyika katika Bwalo la Polisi Mabatini.  Pamoja na mambo mengine, Kamanda Mutafugwa amewaonya baadhi ya waganga wanaojihusisha na upigaji wa ramli chonganishi na kusema Jeshi la polisi halitasita kuchukuwa hatua kali za kisheria dhidi yao. "Sisi Jeshi la Polisi mkoa wa Mwanza hatuwezi kuacha kuwashughulikia ndiyo maana mwaka huu tumekuwa na Operesheni zaidi ya nne za kuwasaka wahalifu kwa lengo la kuzuia mauaji ya watu" Amesema Mutafugwa  Naye afisa mhifadhi daraja la kwanza Mary Kadeshi wa kituo kidogo cha Mwanza (TAWA) pamoja na kutoa elimu kuhusu nyara za...

Mahakama yapongezwa kwa kuzingatia Misingi ya ajira kwa wenye Ulemavu

Maneno hayo yamesemwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi,Vijana,Ajira na Wenye Ulemavu wakati akifunga mafunzo ya Watumishi  wa Serikali, Mahakama na Taasisi za Umma yaliyodhaminiwa kwa ushirikiano wa Mahakama Kuu ya Tanzania na Taasisi ya OSHA inayosimamia Usalama na Afya mahala pa Kazi, yaliyofanyika katika ofisi za OSHA,Dodoma.  Katika mkutano huo, Kikwete amewakumbusha umuhimu wa kuzingatia mafundisho waliyoyapata na kuendelea na mapambano ya kupinga unyanyasaji dhidi ya watu wenye Ulemavu.   Pamoja na hilo Waziri huyo wa Kazi amewapongeza Mahakama  kwa kutoa kipaumbele kwa wenye Ulemavu katika kada zote za kiutendaji ndani ya Muhimili huo wa Nchi. Pamoja na salamu hizo Waziri wa Kazi aliwakumbusha watendaji hao hatua mbalimbali zinazofanywa na serikali ya awamu ya Sita katika kuhakikisha Haki na Maslahi ya Wenye Ulemavi yanasimamiwa kwa kutunga sera na mipango mbalimbali  ikiwemo inayowezesha Sera hizo kutekelezeka. 

Kazi njema na ya Kizalendo inayofanywa na Mpc yamgusa Dc Ngubiagai

Na Obunde Michael;Mwanza Waandishi wa habari mkoani Mwanza wameaswa kutumia Uhuru wa habari uliopo nchini kuandika na Kutangaza habari zenye tija ili kuimarisha ustawi wa Jamii pamoja na kuchochea maendeleo ya kijamii na Kiuchumi.  Mkuu wa wilaya Ukerewe Christopher Ngubiagai ametoa wito huo Jijini Mwanza wakati wa hafla ya usiku wa waandishi wa habari na wadau wa habari mwaka 2024. Ngubiagai aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa Mwanza Said Mtanda kwenye hafla hiyo amesema kuwa vyombo vya habari vina Jukumu la Kutoa Taarifa kwa usahihi pamoja na kuzingatia maslahi mapana ya umma kwenye kila hatua ya kutoa habari.  "Mi binafsi Nina furaha kubwa kumwakilisha Mkuu wetu wa Mkoa katika Tukio hili muhimu ambalo linaadhimisha mchango wa vyombo vya habari katika maendeleo ya Jamii yetu na Taifa kwa Ujumla,Lakini kwanza kabisa natoa pongezi za dhati kwa chama cha waandishi wa habari Mkoa Mwanza (MPC) Nawapongeza Sana kwa kazi kubwa,njema na ya kizalendo mlioifanya kwa miezi yote 12,hongereni s...

Uadlifu ni kipimo cha mtu kuchaguliwa kiongozi

  Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Christopher Ngubiagai ambaye ni Mgeni Rasmi kwenye mafunzo ya Viongozi wa CCM amesema Chama hicho kitaendelea kutawala kwa sababu wanaoomba kutawala bado hawajajiandaa, akawasisitiza vijana kujiandaa vyema kwani ndio viongozi wa kesho. Amesema vijana wasomi wa Tanzania wanapaswa kuwa wazalendo, ili Taifa liwe na rasilimali watu watakaoisaidia nchi yetu kwa ustawi wa vizazi vyetu "Kijana ili awe Kiongozi bora anapaswa kuwa na ari ya kujifunza na kuleta mabadiriko, bila kusahau nia ya kweli ya kuwatumikia watanzania, sambamba na kushiriki katika kuleta maendeleo, Ujana sio umri bali ni fikra za kujipambanua katika kufanya kazi ili kuleta maendeleo" - DC Ngubiagai Aidha amesema, vijana hawapaswi kuwa watazamaji bali kuwa mstari wa mbele katika kujenga Taifa letu na kuongeza kuwa ukabila ni sumu ya maendeleo kwa maana inaweza kuchelewesha maendeleo na uzalendo. "Kiongozi thabiti anayefaa anapaswa kuwa muwajibikaji, mwadilifu, mbunifu,, msikivu na...

Mkuu wa Majeshi atoa ahadi Jwtz kushirikiana na Chuo Kikuu cha Iringa

 Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda amepewa tuzo na Chuo Kikuu cha Iringa kwa kutambua na kuthamini ushirikiano mkubwa na kujitoa kwake katika kuchangia mafanikio na ukuaji wa Chuo hicho. Tuzo hiyo iliyotolewa tarehe 13 Disemba 2024 imekabidhiwa kwake leo tarehe 17 Desemba 2024. Jenerali Mkunda amekishukuru Chuo hicho  kwa kupewa heshima ya kustahili tuzo hiyo na kuthamini mchango wake kwa niaba ya JWTZ. Jenerali Mkunda ameahidi kuendeleza ushirikiano uliopo baina ya Chuo hicho na JWTZ.