Skip to main content

Posts

Showing posts from September 28, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Chatanda: CCM imetuheshimisha wanawake, UWT tunatafuta kura za kishindo za Dk. Samia

Na: Mwandishi Wetu, TEMEKE Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Taifa, Mary Chatanda, amesema UWT inashukuru sana maamuzi yaliyofanywa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kumpitisha Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwania nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwani hiyo inadhihirisha imani kubwa ya Chama kwa wanawake katika nafasi za uongozi. Chatanda ameyasema hayo Septemba 28, 2025, aliposhiriki Mkutano wa Mgombea Mwenza wa CCM, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi wilayani Temeke Jijini Dar es Salaam ambapo amesema wanawake wana uwezo mkubwa wa kiongozi na kiutendaji na Dkt Samia Suluhu Hassan ni amethibitisha hili na ni kielelezo kizuri. "Ndugu Mgombea Mwenza (Balozi Dkt. Nchimbi), naomba niwaambie wananchi hawa wa Temeke, kwa sisi UWT, Umoja wa Wanawake Tanzania tunaendelea kuwashukuru Chama chetu kwa namna kilivyotuheshimisha sisi wanawake, Chama hiki kimeteua Mgombea Urais mwanamke, jambo ambalo halijawahi kutokea tangu nchi hii ya Tanzania imeumbwa, imetokea sasa, kwahiyo...

Wasira: Kunung'unika, Kufikisha Ujumbe Kwa Maandamano Hakuleti Chakula.

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira amesema kunung'unika na kufikisha ujumbe wa changamoto mbalimbali kwa njia ya maandamano kumepitwa na wakati. Amesema Watanzania wanataka maendeleo ukiwemo ujenzi wa miundombinu muhimu ambayo itarahisisha shughuli za kiuchumi na ajira kwa wananchi. Wasira amesema hayo leo Septemba 28, 2025 alipokuwa akizungumza na viongozi na wanachama wa CCM kutoka majimbo ya Vunjo na Moshi Vijijini, mjini Moshi. "Wewe unanung'unika tu maandamano utakula maandamano, tunataka reli ya kisasa kwa sababu katika dunia inayoendelea tofauti ya nchi zetu na nchi zilizoendelea ni miundombinu, ukifika tu unaiona barabara pana, kuna reli inakwenda 'speed' kwa hiyo barabara inakwenda speed. "Hakuna biashara ya kisasa ya kutunza vitu kwa matenga umebeba kichwani, hiyo ni biashara ya zamani, biashara ya kisasa ni ile inayokwenda 'very fast' and speed (inayolwenda haraka). Kwa mujibu wa Wasira,  Ilani ya Uc...

Kishindo cha Balozi Dkt.Nchimbi akiwanadi wagombea ubunge CCM Dar

Na Mwandishi Wetu MGOMBEA Mwenza wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Emmanuel Joh Nchimbi leo Septemba 28,2025 amefanya mkutano mkubwa wa kampeni katika  Uwanja wa Mwenbe Yanga jijini Dar es Salaam. Katika mkutano huo,Dkt.Nchimbi pia alipata nafasi ya kuwanadi baadhi ya wagombea Ubunge wa mkoa huo akiwemo Mbunge wa jimbo la Temeke,Ndugu Mariam Kisangi pamoja na Madiwani. Dkt.Nchimbi ni Mgombea mwenza wa Dkt Samia Suluhu Hassan katika Uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025 wakipeperusha bendera ya CCM. Mpaka sasa   mkoa wa Dar es Salaam unakuwa wa 15 kufikiwa na Dkt Nchimbi katika kusaka kura za ushindi  wa Kishindo za Mgombea Urais wa chama hicho Dkt.Samia Suluhu Hassan,Wabunge pamoja na Madiwani.

Serikali Itaendelea Kuwekeza vya Kutosha Kwenye Huduma Bora za Magonjwa ua Moyo-Majaliwa

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema kuwa Serikali itaendelea kufanya uwekezaji wa kutosha ili kuhakikisha Watanzania wanapata huduma Bora za magonjwa ya moyo na mishipa. Amesema kuwa uwekezaji huo unaenda sambamba na dhamira ya kuendelea kupunguza gharama za matibabu hayo kwa kwenda nje ya nchi hivyo kusaidia kuokoa maisha ya Watanzania. Amesema hayo leo Jumapili (Septemba 28, 2025) alipokuwa mgeni rasmi katika mbio za hisani za Saifee Marathon zilizoanzia na kuishia katika viwanja vya green park Oysterbay, jijini Dar es Salaam. Amesema kuwa Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imewekeza katika ununuzi wa vifaa vya kisasa vya kutoa huduma za uchunguzi ikiwemo ECHO, ECG, Ultrasound na Holter. Amesema kuwa takwimu za Shirika la Afya duniani zinaonesha kuwa takribani asilimia 71 ya vifo vyote duniani vinasababishwa na magonjwa yasiyoambukiza. "Inakadiriwa kuwa zaidi ya watu milioni 4.9 wenye umri wa kuanzia miaka 30 hadi 79 wanamatatizo ya moyo na ...

Mkuu wa Majeshi apongeza wanamichezo wanaotumia tone la damu yao kuliletea heshima Jeshi na Taifa

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini Jenerali Jacob John Mkunda amesema kuwa jeshi na Taifa linatambua ushindi na mafanikio makubwa yaliletwa na wanamichezo nchini hasa kwa timu za majeshi kwa kutumia jasho na damu katika kuliheshimisha taifa ndani na nje ya nchi. Jenerali Mkunda ametoa kauli hiyo Septemba 26 mwaka huu 2025 katika viwanja vya Lugalo Goff Club jijini Dar es salaam wakati wa sherehe ya kuwapongeza wanamichezo kutoka kwa jeshi la ulinzi wa wananchi Tanzania (Ngome) Jeshi la kujenga Taifa (JKT,),timu ya Wanawake wa JKT QUEENS na mwanariadha Alphonce Simbu. Mkuu huyo wa mejeshi. katika sherehe hiyo,amesema jeshi limeandaa hafla hiyo kwa kutambua ushindi na mafanikio yaliyoletwa na wanamichezo katika mashindano mbalimbali ndani na nje ya Tanzania. Kwa hiyo ameipongeza timu ya Ngome kwa kutwaa ushindi wa jumla katika mashindano ya BAMMATA Zanzibar na kusema ushindi huo umeonesha thamani ya mshikamano na nidhamu miongini mwao. "Timu ya Ngome imeweka alama na mfano mkubwa wa k...