Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe Hamza Johari amesema tasnia ya sheria nchini imepata pigo kubwa kufuatia kifo cha mwanasheria mkuu wa Serikaki mstaafu na Jaji mstaafu wa mahakama kuu Frederick Mwita Werema. Ametoa kauli hiyo katika kijiji cha Kongoto wilaya ya Butiama mkoani Mara,wakati wa mazishi Jaji Werema, yaliongozwa na Jaji mkuu wa Tanzania mh Prof Ibrahim Juma, januari 4-2025. Akitoa salamu za Pole, Mwanasheria huyu Mkuu wa Serikali, amesema kuwa Jaji Werema alijitolea kwa hali na mali katika kuhakikisha kwamba Serikali inatekeleza majukumu yake kwa kufuata sheria na kwa uwazi. Alipambana na changamoto nyingi zilizokuwa zikiikabili tasnia ya sheria na hakusita kuanzisha mabadiliko yaliyoleta matokeo chanya kwa wananchi na taifa kwa ujumla. Huu ni urithi mkubwa ambao utaendelea kuwa mfano na msingi wa kazi yetu sote tunaoendelea nayo leo. Aidha, Mwanasheria Mkuu wa Serikali amesisitiza kuienzi na kuiendeleza misingi na mifumo ya sheria aliyoianzish...
Marato tv - Sauti ya Jamii