Skip to main content

Posts

Showing posts from August 6, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Uhuru Kenyata;Nitaunga Mkono Raila Odinga Kuwania Urais ikiwa ataachana na Rais Ruto

  CHAMA cha Jubilee kinachoongozwa na Rais Mstaafu wa Kenya Uhuru Kenyatta kimetangaza kuwa kiko tayari kumuunga mkono Kinara wa ODM Raila Odinga kuwania urais 2027 kikisema kuwa bado kinamtambua kama Kiongozi wa Muungano wa Azimio. Naibu Mwenyekiti wa Jubilee David Murathe, amesema kuwa Rais Mstaafu Uhuru Kenyatta, jana aliwaambia kuwa yupo tayari kumuunga Raila mnamo 2027 mradi tu asambaratishe uhusiano wake na utawala wa sasa. Bw Kenyatta jana aliongoza mkutano wa Kamati Kuu ya Jubilee kwenye makao makuu ya chama hicho, kikao kilichofanyika baada ya mrengo wake kushinda kesi ya mzozo wa uongozi wa Jubilee mahakamani. “Bado tunamtambua Raila kama kiongozi wa Azimio. Na kama muungano tunaamua mwelekeo wetu, hata hivyo nakuambia tuko na Tinga (Raila) hadi hali iwe vingine. Raila ndiye kiongozi wetu na Uhuru mwenyekiti wetu,” akasema Bw Murathe. “Watu pia wanaweza kuamua tuunde muungano mpya na tuwashirikishe viongozi wengine zaidi,” akaongeza. Chama cha Jubilee kinaonekana kimeshaa...

Umoja na Mshikamano ni Silaha ya Mtangamano Imara wa Sadc

Umoja na mshikamano imeelezwa kuwa ni silaha pekee ya Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), ya kuimarisha mtangamano imara na wenye nguvu, utakaowezesha kufikia malengo yaliyowekwa na jumuiya hiyo. Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa Kikao cha Maafisa Waandamizi wa SADC ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Biashara za Kimataifa wa Zimbabwe, Balozi Albert Chimbindi alipokuwa anasoma hotuba ya ufunguzi ya kikao hicho jijini Antananarivo Agosti 06, 2025. Katika kikao hicho ambacho ujumbe wa Tanzania unaongozwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Bi. Amina Khamis Shaaban imeshuhudiwa Zimbabwe kupitia Balozi Chimbindi ikikabidhi uenyekiti wa kikao hicho kwa Madagascar ambapo Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Bw. Eric S. Ratsimbazafy alipokea na kuahidi kuendeleza yale yote mazuri yaliyoanzishwa na mtangulizi wake. Balozi Chimbindi alisema katika kipindi cha uenyekiti wake, mtangamano wa SADC umeendelea kuimarika na mafanikio makubwa yamepa...

Mchengerwa: Miaka 10 ya mapinduzi ya fikra, naomba ridhaa tuijenge Rufiji ya ndoto yetu

Na John Jayros  Mbunge anayetetea jimbo la Rufiji Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema katika kipindi chote amekuwa mtumishi wa watu, mwanamapinduzi wa kweli anayejali maendeleo ya wananchi hivyo amewaomba wajumbe wampe ridhaa ya kuwaongoza ili kuendelea kuleta maendeleo. Kauli hiyo ameitoa leo kwenye mkutano wa kuomba ridhaa ya kuchaguliwa kesho kwenye kura za maoni kuwa mgombea wa jimbo hilo kwa mara ya tatu mfulizo. Mkutano huo umefanyika Ikwiriri na uliohudhuriwa na maelfu ya wajumbe na wananchi waliokuja kusikuliza sera za watia nia wanne wa jimbo hilo ikiwa ni pamoja na Mhe. Mchengerwa anayetetea jimbo lake. Amesema katika kipindi chake cha miaka 10 cha mapinduzi ya fikra na mageuzi makubwa ya maendeleo jimboni humo kumekuwa na mabadiliko kwenye kila sekta. "Ndugu zangu katika safari hii sote tumejionea mapinduzi na mafanikio yaliyopatikana hivyo nawaombeni kwa kasi hii hii nipeni imani ili tuendelee kufanya maendeleo ya kweli ya jimbo letu". Amesisitiza Mhe. Mchengerwa  A...