CHAMA cha Jubilee kinachoongozwa na Rais Mstaafu wa Kenya Uhuru Kenyatta kimetangaza kuwa kiko tayari kumuunga mkono Kinara wa ODM Raila Odinga kuwania urais 2027 kikisema kuwa bado kinamtambua kama Kiongozi wa Muungano wa Azimio. Naibu Mwenyekiti wa Jubilee David Murathe, amesema kuwa Rais Mstaafu Uhuru Kenyatta, jana aliwaambia kuwa yupo tayari kumuunga Raila mnamo 2027 mradi tu asambaratishe uhusiano wake na utawala wa sasa. Bw Kenyatta jana aliongoza mkutano wa Kamati Kuu ya Jubilee kwenye makao makuu ya chama hicho, kikao kilichofanyika baada ya mrengo wake kushinda kesi ya mzozo wa uongozi wa Jubilee mahakamani. “Bado tunamtambua Raila kama kiongozi wa Azimio. Na kama muungano tunaamua mwelekeo wetu, hata hivyo nakuambia tuko na Tinga (Raila) hadi hali iwe vingine. Raila ndiye kiongozi wetu na Uhuru mwenyekiti wetu,” akasema Bw Murathe. “Watu pia wanaweza kuamua tuunde muungano mpya na tuwashirikishe viongozi wengine zaidi,” akaongeza. Chama cha Jubilee kinaonekana kimeshaa...
Marato tv - Sauti ya Jamii