Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa(JKT) Dkt. Stergomena Lawrence Tax, Julai 02 mwaka 2025 amezindua rasmi Mashindano ya Mkuu wa Majeshi (CDF CUP), huku akisisitiza umuhimu wa kudumisha uzalendo, amani, mshikamano ukakamavu ikiwa na lengo la kuunga mkono dhamira ya amiri jeshi mkuu na rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania DK SAMIA SULUH HASSAN katika kukuza sekta ya michezo hapa nchini. Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, katika uwanja wa AZAM COMPLEX Dkt. Tax amesema kwakua michezo ni nyenzo muhimu katika kuunganisha jamii na taifa kwa ujumla, ni dhahiri kuwa upo muhimu kwa jeshi na wananchi kushirikiana katika kuinua na kuiendeleza sekta hiyo kikamilifu ambayo pia licha michezo kuwa sehemu ya mazoezi lakini pia inalenga kupata wanamichezo watakashindana kupata timu za jeshi kwaajili ya kushiriki katika mashindano mbalimbali ya kitaifa na kimataifa. Aidha DK TAX amempongeza mkuu wa majeshi nchini Jenerali Jacob John Mkunda kwa kuendeleza mashindano ya majeshi kwani lich...
Marato tv - Sauti ya Jamii