Skip to main content

Posts

Showing posts from January 23, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Waziri Mkuu Kumwakilisha Rais Dkt. Samia Katika Mazishi Ya Mzee Edwin Mtei*

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Januari 24, 2026 amewasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) ambapo anatarajiwa kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika mazishi ya marehemu Mzee Edwin Mtei, yanayofanyika Tengeru, jijini Arusha. Mzee Mtei ambaye aliwahi kuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) katika kipindi cha mwaka 1966 hadi 1974 alifariki  usiku wa Januari 19, 2026 jijini Arusha.

Waziri Mkumbo Aanza Ziara Rasmi Uingereza Katika Kuendeleza Diplomasia ya Uchumi

London, Uingereza  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Mheshimiwa Prof. Kitila Alexander Mkumbo (Mb.), amewasili jijini London kuanza ziara rasmi ya kikazi nchini Uingereza kuanzia tarehe 22 hadi 27 Januari 2026, yenye lengo la kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi, biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na Uingereza. Mara baada ya kuwasili, Mheshimiwa Waziri alifanya kikao cha kazi katika Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jijini London, akiwa na mwenyeji wake Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Mheshimiwa Mbelwa Kairuki, ambapo walijadili masuala ya kuimarisha mahusiano ya kiuchumi, mazingira ya uwekezaji na fursa zilizopo kwa wawekezaji wa Uingereza nchini Tanzania. Ziara hii inaashiria mwanzo wa utekelezaji wa mikutano na shughuli mbalimbali ikiwemo kukutana na wawekezaji, taasisi za kifedha, makampuni ya kimataifa na wadau wa maendeleo, kwa lengo la kutangaza fursa za uwekezaji nchini Tanzania na kuendeleza diplomasia ya uchumi. Katika ziara hiyo, Mhesh...

Waziri Mkumbo Aanza Ziara Rasmi Uingereza Katika Kuendeleza Diplomasia ya Uchumi

London, Uingereza  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Mheshimiwa Prof. Kitila Alexander Mkumbo (Mb.), amewasili jijini London kuanza ziara rasmi ya kikazi nchini Uingereza kuanzia tarehe 22 hadi 27 Januari 2026, yenye lengo la kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi, biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na Uingereza. Mara baada ya kuwasili, Mheshimiwa Waziri alifanya kikao cha kazi katika Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jijini London, akiwa na mwenyeji wake Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Mheshimiwa Mbelwa Kairuki, ambapo walijadili masuala ya kuimarisha mahusiano ya kiuchumi, mazingira ya uwekezaji na fursa zilizopo kwa wawekezaji wa Uingereza nchini Tanzania. Ziara hii inaashiria mwanzo wa utekelezaji wa mikutano na shughuli mbalimbali ikiwemo kukutana na wawekezaji, taasisi za kifedha, makampuni ya kimataifa na wadau wa maendeleo, kwa lengo la kutangaza fursa za uwekezaji nchini Tanzania na kuendeleza diplomasia ya uchumi. Katika ziara hiyo, Mhesh...

Dkt Akwilapo Aelekeza Hatua Kuchukuliwa Kwa Wadaiwa Kodi ya Ardhi

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo, amezielekeza Ofisi za Makamishna wa Ardhi Wasaidizi wa Mikoa nchini kuhakikisha zinachukua hatua kwa wadaiwa wote wa kodi ya pango la ardhi. Mhe. Dkt. Akwilapo ametoa kauli hiyo leo, tarehe 23 Januari, 2026, wakati wa kikao chake na watumishi wa Sekta ya Ardhi kilichofanyika jijini Dodoma. Amesema Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ina jukumu la kukusanya mapato yatokanayo na Sekta ya Ardhi, hadi sasa imekusanya asilimia 37 ya lengo lake la kukusanya kiasi cha shilingi bilioni 290. "Ninatambua kuwa kila mkoa umepewa lengo la kukusanya maduhuli; hivyo, kila mmoja wetu atapimwa utendaji wake katika kufikia malengo ya makusanyo yaliyowekwa na mfanye bidii na uonekane unafanya vinginevyo tutakuita na kukuliza kama unatosha hapo ulipo," amesema. Ikumbukwe kuwa tarehe 23 Desemba, 2025, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, alitoa taarifa kwa umma ya kuwataka wamiliki wote wa ardhi kuli...

Ofisi za Ardhi Zapatiwa Vifaa Vya Tehama 1,429 Kuboresha Utendaji

* Mhe. Dkt Akwilapo asisitiza matumizi ya TEHAMA Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo, amekabidhi jumla ya vifaa vya TEHAMA 1,429 vyenye thamani ya Shilingi Bilioni 5.2 kwa ajili ya Ofisi za Ardhi katika halmashauri 184 nchini, pamoja na ofisi za Makamishna wa Ardhi Wasaidizi wa Mikoa. Makabidhiano hayo yamefanyika tarehe 23 Januari, 2026, jijini Dodoma, wakati wa kikao kazi kati ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na watumishi wa sekta ya ardhi pamoja na wale wa taasisi zilizo chini ya Wizara. Vifaa vilivyokabidhiwa ni juhudi ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kuhakikisha huduma katika sekta ya ardhi zinaimarishwa na kuboreshwa kwa ofisi za ardhi kupatiwa vifaa ili kurahisisha utendaji kazi wao katika kuwahudumia wananchi. Vifaa vya TEHAMA vilivyokabidhiwa ni Kompyuta za kawaida 424, Kompyuta zenye uwezo mkubwa kwa ajili ya kazi za ardhi (GIS computer) 250, Sk...

Mv New Mwanza Yazinduliwa Rasmi

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba, amezindua meli ya kisasa MV New Mwanza, akibainisha kuwa ni uwekezaji wa kimkakati wa Serikali katika kuimarisha usafiri wa majini, usalama wa abiria na kukuza uchumi wa Kanda ya Ziwa.  “Serikali imejidhatiti kuhakikisha usafiri wa majini unakuwa salama, wa uhakika na unaowanufaisha wananchi,” — Dkt. Mwigulu Nchemba.  MV New Mwanza ina uwezo wa kubeba abiria 1,200, mizigo tani 400 na magari, huku safari ya Mwanza–Bukoba ikichukua takribani saa 6. Mradi huu umegharimu USD 51.83 milioni (takribani TSh bilioni 120.56).

Mapinduzi Makubwa Uwezeshaji Mitaji Kwa Wachimbaji Wadogo

▪️Wizara ya Madini na CRDB waingia makubaliano ya utekelezaji wa programu ▪️Wachimbaji wadogo kukopeshwa Mitambo ya Uchenjuaji (CIP), Vifaa vya Kuchimba na Fedha za Uendeshaji ▪️Kikundi cha SAZA GOLD FAMILY wakaribia kuanza kunufaika kupitia leseni ya uchimbaji iliyokuwa inamilikiwa na BAFEX ▪️Ni leseni aliyoelekeza Rais Samia kwa wachimbaji wadogo Dodoma Ikiwa ni mkakati wa kuwawezesha wachimbaji wadogo wa madini kimitaji, Wizara ya Madini imeingia makubaliano na Benki ya CRDB kupitia programu maalum kwa ajili ya kuwasadia wachimbaji wadogo kwa kuwapatia mikopo kwa ajili ya ununuzi wa mitambo ya uchenjuaji (CIP), vifaa na gharama za uendeshaji. Akizungumza kwenye kikao cha kujadili mapendekezo ya ushirikiano kati ya Benki ya CRDB na Tume ya Madini katika utoaji wa mikopo kwa wachimbaji wadogo wa madini, Waziri Mavunde amesema kupitia makubaliano haya, wachimbaji wadogo wenye leseni za madini wataweza kuomba na kupatiwa mikopo na benki hiyo na kuwezesha uzalishaji wao kuwa wenye tija n...

CTI yasema ushirikiano na serikali umetatua changamoto za wenye Viwanda

Na Mwandishi Wetu SHIRIKISHO la Wenye Viwanda Nchini (CTI), limesema ushirikiano mzuri baina ya serikali na shirikisho hilo umechangia kwa kiwango kikubwa kutatua changamoto mbalimbali zzilizokuwa zikiwakabili wenye viwanda. Hayo yamesemwa na Makamu Mwenyekiti wa Shirikisho hilo, Mhandisi Benedict Lema, wakati akizungumza kwenye ziara ya Waziri wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga kwenye viwanda mbalimbali jijini Dar es Salaam. Mhandisi Lema alisema CTI na wenye viwanda nchini wanathamini uhusiano mzuri uliopo baina ya serikali na wenye viwanda ambao umekuwa na manufaa makubwa kwenye kutatua changamoto zao. “Kuna uhusiano wa karibu sana baina ya ofisi ya Waziri wa Viwanda na CTI, ushirikiano huu ndio unafanya wawekezaji kuwa na mori wa kufanya zaidi na kutimiza malengo ya serikali yetu, mheshimiwa Waziri ziara yako yaa leo ni uthibitisho wa kutosha tosha kuonyesha uhusiano mwema baina ya ofisi yako na wazalishaji wa viwandani,” alisema Alisema viwanda vinatekeleza ajenda ya serikali ...

PSSF Yaimarisha Huduma Kwa Wanachama Wake

Ada Ouko na Timothy Itembe, Musoma. MFUKO wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSF) umeanza kulipa stahiki za watumishi mbalimbali wa umma wakiwemo ambao walioondolewa katika mfumo wa ajira kutokana na kuwa na vyeti feki. Kaimu Meneja Pssf Mkoa wa Mara Nuru Mahinya amebainisha hayo wakati akifungua semina ya siku moja janury 22,2026 inayolenga kuwajengea  waandishi wa habari mkoani humo namna kuripoti taarifa zinazohusiana na mfuko huo wa jamii. "Tumieni kalamu zenu katika kufikisha ujumbe huu kwa jamii na katika hili tuna maana ya watumishi wale walioondolewa kazini kwa sababu ya vyeti feki tayari wame lipwa stahiki zao ambazo ni asilimia tano waliochangia kwenye mfuko huo wakati wa utumishi wao. alisema Nuru.  Alisema mfuko huo pia umeanza kulipa pensheni ya mkupuo wa miezi 36 mstaafu aliyefariki kundi hilo linalohusisha watumishi wa umma waliostaafu kwa umri au ugonjwa tu.  "Malipo haya ya mkupuo yatalipwa kwa wategemezi wa marehemu wanaotambulika kisheria kama ...