Na Andrew Chale-Zanzibar TAMASHA kubwa la muziki wa Rege (Reggae) Zanzibar msimu wa Sita linatarajiwa kufanyika kwa siku mbili kuanzia usiku wa Ijumaa Agosti 9-10, 2024, Mambo Club ndani ya Ngome Kongwe, Unguja, Zanzibar. Mkurugenzi wa Tamasha hilo, Said Omary Hamad 'Side Rasta' Akizungumza na Waandishi wa Habari wakati wa kutambulisha wasanii na utayari wa Tamasha hilo, ameishukuru Serikali kwa ushirikiano ambapo ameomba wadau kujitokeza kudhamini kwani ni Moja ya matamasha yanayoongeza fursa za kiuchumi Visiwani humo. Side Rasta amesema Zanzibar Reggae Festival ni moja ya matamasha makubwa Afrika Mashariki kwa sasa hivyo ni wakati wa Makampuni ya binafsi na taasisi za Kiserikali kujitokeza kuweka udhamini wao. "Muziki wa Rege unahamasisha amani na umoja na upendo. Ni muziki wenye ustaarabu na kuponya pia hivyo hii ni fursa ya kipekee kwa Wadau kujitokeza kudhamini ilikuongeza tija kwa vijana na maendeleo katika Nchi. Side Rasta amesema Kenya wameweza kuipa nguvu mziki...
Marato tv - Sauti ya Jamii