Skip to main content

Posts

Showing posts from March 11, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Waziri Mkuu Atoa Maagizo Mazito Kwa Wakuu wa Mikoa Nchini

_Asema waandae mapendekezo kuhusu utitiri wa taasisi za udhibiti na kodi_ _Ataka yawasilishwe kwa Waziri wa Fedha, yaingizwe katika Muswada wa Sheria ya Fedha wa mwaka huu_ WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amewataka Wakuu wa Mikoa na watendaji wao katika mikoa yote nchini wajipange kutoa taarifa kuhusu uwekezaji na ukuzaji wa biashara kwenye mikoa yao kila wanapotoa taarifa kwa viongozi wa kitaifa. “Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa, Makatibu Tawala na Wakurugenzi wa Halmashauri mbebe jukumu la kuwa mabalozi wa kwanza wa uwekezaji katika maeneo yenu kwa kutambua na kutangaza fursa mbalimbali zilizopo katika maeneo yenu.” “Tubebe hili jukumu, kila Mkuu wa Mkoa anapotoa taarifa atapaswa aseme ameongeza uwekezaji kwa kiasi gani, amekuza biashara kwa kiasi gani na katika kuongeza biashara mpya Ametoa wito huo leo jioni (Jumatano, Machi 11, 2026) wakati akifunga Mkutano wa Kuhakiki Rasimu ya Pili ya Mpango wa Kuboresha Mazingira ya Biashara na Uwekezaji (Mkumbi II) uliofanyika katika ukumbi wa Kam...

Rais Samia kumuasili mtoto aliyetelekezwa kunavyodhihirisha upendo wake kwa jamii

Na: Dkt. Reubeni Lumbagala, Tanga Watoto wana haki zao za msingi. Wanapaswa kupendwa, kulindwa, kusikiliza, kupewa malezi na matunzo.  Pia, watoto wanapaswa kupewa mahitaji yote ya msingi yaani chakula, mavazi na malazi. Kimsingi, ni wajibu wa msingi kwa wazazi na walezi hukakikisha watoto wanapata haki na mahitaji yao muhimu ili waweze kufurahia maisha kwa kuzingatia kuwa watoto ni kiungo muhimu katika familia na maendeleo ya Taifa. Serikali kama mdau muhimu wa ustawi na maendeleo ya watoto, inawajibika kuweka mazingira mazuri ya ustawi wa watoto. Aidha, serikali inawajibika kutunga sheria zitakazowalinda watoto ili kesho zao ziweze kutimia na Taifa linufaike kupitia uwepo wao. Ipo changamoto katika jamii zetu kwa baadhi ya wanawake kutupa watoto pindi wanapojifungua watoto hao. Wengine huwatupa katika mazingira ambayo ni rahisi kuokotwa na wapita njia lakini baadhi yao huwatupa katika mazingira mabaya mathalani jalalani ambapo kwa bahati mbaya wengine huokotwa wakiwa  tayari...

Mkemia Mkuu wa Serikali Atoa 'shavu' Kwa Vijana wa Kitanzania

 DODOMA SERIKALI kupitia Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali inatoa fursa kwa vijana wabunifu wa Kitanzania wanaoweza kubuni na kuunda mifumo wezeshi ya TEHAMA na Akili Unde ili kuiwezesha serikali katika kuboresha utendaji kazi. Akieleza utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo na Fursa za vijana zilizopatikana katika Siku 100 za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mkemia Mkuu wa Serikali, Fedelice Mafumiko amesema fursa hiyo kwa vijana wabunifu ni dhamira ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuifanya nchi kuwa na wataalamu wengi katika sekta Mbalimbali hapa nchini. "Wabunifu wa Kitanzania wanaoweza kubuni na kuunda mifumo wezeshi ya TEHAMA na Akili Unde watasaidia kupunguza gharama za uendeshaji na kupunguza urasimu katika utoaji wa huduma kwa wananchi na wadau mbalimbali". Amesema  Sambamba na hayo, Mkemia Mkuu huyo amesema Pamoja na Mamlaka kuendelea na utaratibu wa Kutumia wataalam wake wa ndani kufanya matenegenezo na matengenezo kinga ya mitambo na vifaa vya maabara l...

Serikali imeanza Ujenzi wa Bomba la Kusafirisha Gesi

 DODOMA. KATIKA kuchochea ukuaji wa uchumi na kuimarisha upatikanaji wa nishati nchini, Serikali kupitia Shirika la Maendeleo ya Petrol Tanzania (TPDC) imesema Mradi wa ujenzi wa bomba la kusafirishia gesi asilia kutoka Dar es Salaam Hadi Chalinze umeanza kutekelezwa. Ujenzi wa mradi huo unatarajiwa kuanza Januari 2027 na kutekelezwa kwa kipindi cha miezi 15 hadi kukamilika kwake. Akieleza Mafanikio yaliyopatikana katika siku 100 za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan Leo jijini Dodoma, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) Mussa Makame amsesema Utekelezaji wa mradi huo umeshaanza Amesema hadi Sasa mkuza kutoka Kinyerezi hadi Chalinze umepatikana na tathmini ya hali ya udongo kwa eneo lote la mkuza ipo hatua za mwisho kukamilika.  "Upembuzi yakinifu wa mradi (feasibility study) inaendelea na Ujenzi wa mradi unatarajiwa kuanza Januari 2027 na kutekelezwa kwa kipindi cha miezi 15 hadi kukamilika kwake". Amesema  "Mradi huu ukikamilika utafungua ...

Askofu wa Jimbo Katoriki la Musoma Awataka Wanasiasa, Waandishi,Jeshi la Polisi Kuheshimu Maeneo ya Kanisa

Na mwandishi wetu Jovina Massano;Musoma. Askofu wa Jimbo katoriki Musoma Michael Msonganzila awataka wanasiasa, waandishi wa habari na Jeshi la Polisi kuheshimu maeneo ya kanisa. Ameyasema hayo  mbele ya waandishi wa habari Machi 10,2026 Ofisini kwake huku akilaani vitendo vilivyotokea siku ya Ibada Machi 8,2026 na kuzua taharuki kwa waamini wa kanisa kuu la Jimbo katoriki Musoma. Amesema ni vema Jeshi la Polisi likajenga  mahusiano mazuri na jamii lakini pia amewataka wanasiasa kutofanya shughuli za kisiasa katika eneo la kanisa kwa kuwa vyama hivyo vina ofisi zao za kisiasa. " Kanisa halikuwa na taarifa yeyote ya uwepo wa wanasiasa siku hiyo ya Ibada, bali kulikuwa na maombi ya kutumia eneo viwanja vya matumaini katika Vijana linalomilikiwa na kanisa katoriki baada ya kupata taarifa ya zuio kutoka Jeshi la Polisi kwa kuwa tuliwakubalia ilibidi tuwape taarifa ya kuwaeleza kuwa kwa kuwa hamna kibali Cha kufanya mikutano,na makongamano nchini,"amesema Msonganzila. Ameendelea k...

Waziri Mkuu Aongoza Kikao cha Kujadili Mapendekezo ya Kufanya Maboresho ya Sheria ya Mapato ya Baadhi ya Mifuko

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Machi 11, 2026 ameongoza Kikao cha kujadili Mapendekezo ya kufanya Maboresho ya Sheria ya Mapato ya baadhi ya Mifuko kilichofanyika kwenye ukumbi wa Waziri Mkuu,  Bungeni jijini Dodoma, Machi 11, 2026.  Baadhi ya viongozi walioshiriki katika Kikao hicho ni pamoja na Waziri  wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, William Lukuvi, Waziri wa Ujenzi Abdallah Ulega, Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Mussa Omar, Waziri wa Madini, Anthony Mavunde na Waziri wa Nishati, Deogratius Ndejembi. Wengine ni Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Wanu Hafidh Ameir, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu- Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Ummy Nderiananga, Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Dkt. Jim Yonaz na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Dkt. Natu El - maamry

Mary Chatanda atimiza ahadi ya ng'ombe wawili kwa Magereza

Na: Mwandishi Wetu, KOROGWE Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Taifa, Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa (MCC) na Mbunge wa Viti Maalum wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM, Mary Chatanda, ametimiza ahadi yake ya kutoa ng'ombe wawili wa maziwa kwa Magereza mawili ya wilayani Korogwe mkoani Tanga. Hafla hiyo imefanyika Machi 09, 2026, ambapo viongozi wa CCM ngazi ya wilaya walimwakilisha Chatanda Katika kukabidhi ng'ombe hao. Katika Gereza la Kwamngumi viongozi wa Chama walikabidhi ng'ombe wa maziwa kwa kikundi cha wake wa Askari Magereza huku ng'ombe mwingine akikabidhiwa kwa uongozi wa Gereza la Manundu. Akizungumza katika makabidhiano hayo, Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Korogwe, Thobias Nyakusagira alisema "Utoaji wa ng'ombe hawa ni utekelezaji wa ahadi ya Mama Mary Pius Chatanda baada ya kufanya ziara Magerezani na akapokea changamoto na leo tupo hapa kutekeleza ahadi yake."  Kwa upande wa Katibu wa CCM ...

Rais Samia Amuasili Mtoto Mchanga Aliyetelekezwa Nzega

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, amemuasili mtoto mchanga wa kike leo tarehe 11 Machi, 2026, katika makazi yake, Ikulu Chamwino, mkoani Dodoma. Mtoto huyo aliyepewa jina la Grace Samia Suluhu Hassan alitelekezwa mjini Nzega, mkoani Tabora, na amekabidhiwa kwa Rais Dkt. Samia na Mkuu wa Wilaya ya Nzega, Mhe. Naitapwaki Tukai. Akizungumza wakati wa kumkabidhi mtoto huyo, Mkuu wa Wilaya Tukai alisema mtoto huyo aliokotwa tarehe 17 Januari, 2026 akiwa ametelekezwa katika eneo jirani na nyumba ya wageni ya Kasulu, Nzega Mjini.  Alieleza kuwa baada ya kupokea taarifa hizo, alishirikiana na Jeshi la Polisi kumchukua mtoto huyo na kumpeleka hospitalini kwa uchunguzi na uangalizi, huku juhudi za kumtafuta mama yake zikiendelea bila mafanikio. Rais Dkt. Samia amemkaribisha mtoto huyo katika familia yake na kuahidi kumpatia malezi, ulinzi na huduma zote muhimu ili akue katika mazingira salama na yenye upendo. “Wanaotupa watoto hawajui wanalolifanya...

Prof. Kabudi Akutana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Canada

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Kazi Maalum), Prof. Palamagamba Kabudi, amefanya mazungumzo na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Canada, Mhe. Robert Oliphant. Mazungumzo hayo yamefanyika jijini London, Uingereza, pembezoni mwa Mkutano wa 26 wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Jumuiya ya Madola uliofanyika Machi 8, 2026, ambapo viongozi hao wamejadili namna ya kuimarisha ushirikiano wa kimataifa kati ya Tanzania na Canada pamoja na kuendeleza uhusiano wao ndani ya Jumuiya ya Madola kwa kuzingatia misingi na tunu za jumuiya hiyo katika kukuza ushirikiano na maendeleo ya pamoja. Viongozi hao wamebainisha kuwa uhusiano kati ya Tanzania na Canada umejengwa juu ya msingi wa urafiki wa kihistoria, ushirikiano wa kiuchumi pamoja na uanachama wao ndani ya Jumuiya ya Madola, hali inayofungua fursa zaidi za kupanua ushirikiano katika nyanja za biashara, uwekezaji na kubadilishana uzoefu katika sekta mbalimbali za maendeleo. Aidha, viongozi hao wameangazia mchango wa diaspora wa Tanzania na Canada katika ...