Skip to main content

Posts

Showing posts from December 24, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Rais Dkt. Samia awapa Zawadi ya Sikukuu Wananchi Jimbo la Musoma Vijijini

Na Shomari Binda-Musoma WANANCHI wa jimbo LA Musoma vijini wamepokea zawadi ya sikukuu ya Krismass na mwaka mpya kutoka kwa Raid Dkt.Samia Suluhu Hassan. Zawadi iliyotolewa ni gari la kubeba wagonjwa( Ambulance) lililokabidhiwa na mbunge wa jimbo hilo Profesa Sospeter Muhongo. Gari hilo limekabidhiwa jana disemba 24 kwenye kituo cha afya cha Kata ya Bugwema na kupokelewa kwa shangwe na wananchi walioshuhudia tukio hilo. Wanavijiji kutoka Kata hiyo yenye vijiji vinne vya (Bugwema, Kinyang'erere, Masinono na Muhoji) wamemshukuru sana  Rais Dkt.Samia kwa kuwapatia gari jipya la wagonjwa ambalo litawasaidia kwa huduma za afya.  Wanavijiji hao wameahidi kumpatia  Rais Samia kura zote za Kata hiyo kwenye uchaguzi mkuu wa mwakani (2025). " Tunamshukuru sana Rais Dkt.Samia kwa zawadi hii nzuri kwetu na tuna muombea maisha marefu ili aendelee kutuhudumia watanzania"anasema Musa Jumapili. Akikabidhi gari hilo mbunge wa jimbo la Musoma vijijini Profesa Sospeter Muhongo amesema Rais ...

Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar asifu Kazi Nzuri inayofanywa na Rais Mwinyi

  Na Kitengo cha Habari ; Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar.  Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Othman Masoud Othman, amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inaendelea kusimamia na kuhakikisha watoa huduma za afya wanapatiwa maakazi mazuri ili kutoa huduma bora kwa wananchi, na kuwaongezea ufanisi zaidi, katika utekelezaji wa majukumu yao. Mheshimiwa Othman ameyasema hayo leo Jumanne Disemba 24, 2024 akiwa Mgeni Rasmi katika Hafla ya Uwekaji wa Jiwe la Msingi wa nyumba za wafanyakazi wa hospitali ya wilaya ya Wete, huko Kinyasini Mkoa wa Kaskazini Pemba. Amesema ujenzi wa makaazi ya wafanyakazi, karibu na hospitali au jirani na vituo vyao vya kazi, lengo lake ni kuwapunguzia masafa pamoja na gharama za usafiri kwa kuwafata madaktari bingwa, na ili kuimarisha huduma za matibabu na kuhakikisha kila muhitaji anapata matibabu kwa wakati.   “Nyumba hizi zinazojengwa na zinatarajiwa kuhudumia makaazi ya takriban Familia 16, zitakua msaada mku...

Meja Jenerali Mstaafu Busungu afariki dunia

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda anasikitika kutangaza kifo cha Meja Jenerali Martin Shuminzi Busungu(Mstaafu) kilichotokea Desemba 24 Mwaka huu, Majira ya Saa kumi na robo za Jioni.  Katika Utumishi wake Jeshini,Jenerali Busungu aliwahi Kushika Madaraka Mbalimbali yakiwemo Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa Mwaka 2018 hadi 2019. Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania, Gaudentius Gervas Ilonda imeeleza kuwa Taarifa za Utoaji wa heshima za mwisho kwa marehemu pamoja na shughuli za mazishi zitatolewa baadaye.

Jeshi la Polisi Lapiga Marufuku Disco Toto

Na Angela Sebastian  JESHI la polisi mkoani Kagera limepiga marufuku disco toto wakati wa sikukuu za Christmas na mwaka mpya kwasababu kumbi zinazotumika hazina viwango vinavyotakiwa hivyo, atakayetaka kuendesha zoezi hilo apate kibari cha polisi baada ya kuwafanyiwa ukaguzi na kujilidiisha. "Kwa wale wanaopenda kuendesha disco toto polisi Kagera tumepiga marufuku kwasababu mara nyingi wanaoendesha disco kwa ajili ya watoto hawazingatii uwezo wa kumbi zao, tumeishashuhudia katika baadhi ya maeneo tumepoteza watoto wengi japo siyo Kagera "anaeleza kamanda Chatanda  Amesema tukio kama hilo liliwahi kutokea kule mkoani Tabora miaka ya nyuma ambapo watoto wengi walipoteza maisha na sababu ilikuwa ni uzembe kwasababu mmiliki alichokua anangalia ni kupata fedha na si usalama wa watoto. "Kwa yule ambaye anadhani anaweza akakidhi vigezo aje polisi twende tukague tujiridhishe kama eneo linafaa na liwe eneo la wazi na kuhakikisha kuwa halina viashiria hivyo,mpaka saaa sijapata mt...