*📌 Dkt. Biteko asisitiza teknolojia itumike uchakataji zao la ndizi* *📌Dkt. Biteko ahimiza uwekezaji viwanda vya kuongeza thamani mazao ya uvuvi na ufugaji* *📌 Kagera yaongoza kwa uzalishaji zao la ndizi nchini kwa asilimia 60* *📌 Mradi wa Mashamba Makubwa ya Kahawa Kagera kunufaisha watu 10,000* *Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati* Wawekezaji kutoka ndani na nje ya nchi wamekaribishwa kuwekeza mkoani Kagera kufuatia hatua mbalimbali za utekelezaji wa miradi ambazo mkoa wa huo umefikia ikiwa ni pamoja na mipango ya maendeleo na fursa nyingi za uwekezaji zilizopo. Mkoa wa Kagera ni wa pili kwa uzalishaji wa samaki na fursa ya uvuvi nchini ukitanguliwa na Mkoa wa Mwanza fursa ambayo inawanufaisha wakazi wake kwa kuwapatia ajira, lishe bora, kipato na maendeleo ya kiuchumi ikiwa ni pamoja na ujenzi wa makazi bora kutokana na shughuli za uvuvi. Akizungumza Desemba 19, 2024 katika Uwanja wa Kaitaba wilayani Bukoba mkoani Kagera wakati aliposhiriki katika Tama...
Marato tv - Sauti ya Jamii