Skip to main content

Posts

Showing posts from February 23, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Azania Bank Yang'ara Kili Marathon

 Azania Bank ndani ya Kili Marathon Wafanyakazi wa Azania Bank wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya kumaliza m kilometre 21 katika mbio za Kili Marathon zilizofanyika jijini Moshi.Imekuwa ni utamaduni wa Benki hiyo kushiriki katika mbili hizo za kimataifa kila mwaka.

Waziri Kikwete kufanya ziara ya Siku tatu Mkoani Songwe

-Atakagua na Kuzindua Miradi ya Maendeleo   Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu -Mhe. Ridhiwani Kikwete leo Februari 23, 2025 amewasili mkoani Songwe kwa lengo la ziara ya  kukagua miradi ya Maendeleo ikiwemo ya sekta  ya Elimu, Afya na Miundombinu   kwa ajili ya ustawi wa maendeleo ya wananchi . Mhe. Waziri Kikwete anatarajiwa kukagua na kuweka Mawe ya msingi katika miradi hiyo ambayo inakadiriwa kugharimu zaidi ya shilingi Bilioni 700 katika Halmashauri zote za mkoa huo. Mara baada ya kuwasili katika  mkoa huo , Waziri Kikwete alipokelewa na Mkuu wa Mkoa huo Ndg. Daniel Chongolo ambaye alimpa hali ya maendeleo ya Mkoa huo na maandalizi ambayo yameshafikiwa kwa ajili ya ziara hiyo. Vile vile Mhe.  Kikwete anatarajiwa pia kukagua Maendeleo ya Kituo cha Vijana cha Sasanda wilayani   Songwe ambapo atakagua  mradi wa Shamba la vijana lililopo kituo hicho.  Mhe.Waziri Kikwete ameambatana...

Kili Marathon Itumike Kutangaza Utalii - Dkt. Biteko

  📌 Watu zaidi ya 20,000 washiriki Kili Marathon 📌 Awaasa kuzingatia ulaji na  kufanya mazoezi 📌 Serikali kuboresha miundombinu ya viwanja vya michezo *Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati* Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ameiagiza Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kushirikiana na Kampuni ya Kili International Marathon ambao ni waandaji wa mbio za Kili marathon kuhakikisha mbio hizo zinatumika kutangaza vivutio vya utalii vilivyoko nchini. Dkt. Biteko ametoa agizo hilo leo Februari 23, 2025 mkoani Kilimanjaro wakati aliposhiriki mbio za Kili Marathon za kilomita 5. “ Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo iangalie namna bora ya kushirikiana na Kili Marathon ili mbio hizi ziwe nyenzo ya kutangaza utalii wetu  na kuwa fursa kwa wageni kutembelea vivutio vyetu vya utalii,” amesema Dkt. Biteko. Amesema mbio hizo zimeendelea kuwavutia watu wengi zaidi ndani na nje ya nchi ambapo mwaka huu zaidi ya watu 20,000 wameshirik...

Rais Samia Afungua Hospitali Ya Wilaya Ya Handeni Mkoani Tanga

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akivuta kitambaa kuashiria ufunguzi wa Hospitali ya Halmashauri ya wilaya ya Handeni iliyopo Mkata mkoani Tanga tarehe 23 Februari, 2025.

Endelezeni Mafunzo Ya Dini -majaliwa

  _▪️Asema ushiriki wa Rais Dkt. Samia kwenye tuzo hizo ni kielelezo cha namna anavyothamini na kuiishi Imani ya Dini ya Kiislam na uhifadhi wa Qur’aan_ _▪️Asema tuzo hizo zinaimarisha imani ya dini na uwezo kwa vijana._   WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ametoa wito kwa viongozi wa madhehebu ya dini kuendelea kufundisha na kuimarisha elimu ya dini ili kutoa fursa kwa watoto na vijana kupata elimu hiyo na kuwaandaa kuwa watu wema. Ametoa wito huo leo Jumapili (Februari 23, 2025) alipomwakilisha Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye kilele cha Tuzo za 33 za Kimataifa za Kuhifadhi Qurani Tukufu. yanayofanyika katika uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. “Jukumu la kuhakikisha maadili bora ni la kwetu sote, madhehebu ya dini yakiwa na mchango mkubwa. ” Aidha, Mheshimiwa Majaliwa amehimiza madhehebu yote ya dini kuendelea kuhubiri amani, mshikamano na utulivu hasa katika kipindi cha kuelekea katika Uchaguzi Mkuu. “Amani na utulivu ni moja ya Tunu katika nchi yetu” A...

Waziri Simbachawene Awaita Viongozi wa Umoja wa Walimu Wasiokuwa na Ajira

  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Simbachawene ameipongeza timu inayosimamia mchakato wa ajira za Ualimu, kwa namna wanavyoendesha zoezi hilo kwa uadilifu na ufanisi. Simbachawene ametoa pongezi hizo leo Februari 23, 2025, alipotembelea na kukagua timu inayosimamia mchakato wa ajira za Ualimu inayoendelea na kazi hiyo katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) mkoani Morogoro. Ametumia fursa hiyo kuwaita ofisini kwake Dodoma kwa mazungumzo viongozi wa vijana waliojitambulisha kwenye andiko lao kuwa ni 'Non Employed Teachers Organisation (NETO)' wenye umoja wao kupitia mitandao ya Kijamii. “Nimesoma makala yao yenye kichwa cha habari Ombi la Wahitimu wa Ualimu Vyuo mbalimbali nchini kati ya mwaka 2015-2023 kwa Serikali, andiko lao ni zuri na linaeleweka ingawa linahitaji ufafanuzi zaidi, hivyo ninatoa wito kwa vijana hao kuja ofisini Dodoma kwa mazungumzo”. amasisitiza Waziri Simbachawene Amesema amewasiliana na Waziri wa...