Skip to main content

Posts

Showing posts from August 17, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

GEL yatoa fursa za udahili wa papo kwa papo maonesho ya Dar

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI ya Global Education Link (GEL) imewataka wanafunzi wanaotaka kujiunga na vyuo vikuu kuwa makini na kozi wanazochagua wanapotaka kujiunga na vyyuo vikuu mbalimbali ndani na nje ya nchi. Ushauri huo ulitolewa jana  na Meneja Mkuu wa GEL, Regina Lema, wakati wa  maonesho ya kitaaluma ya vyuo vikuu mbalimbali kwa wanafunzi wa shule za sekondari zaidi ya 102 za Mkoa wa Dar es Salaam. Alisema GEL imekuwa ikitoa mwongozo kwa wanafunzi mbalimbali kuhusu kozi sahihi wanazopaswa kuchukua wanapokwenda kusoma vyuo vikuu mbalimbali na kwenye maonesho hayo wametoa elimu hiyo. Regina alisema mbali na kutoa elimu hiyo, GEL imetoa huduma za udahili wa papo kwa papo, pamoja na ushauri wa taaluma na malezi ya kitaaluma kuwawezesha wanafunzi kuelewa vyema nini cha kusomea kwa ajili ya kufanikisha malengo ya Taifa ya mwaka 2025 hadi 2050. Regina  alisema kuwa kupitia ushiriki huo, GEL pia limeimarisha uhusiano wake na shule za msingi na sekondari kwa kushirikiana na ...

Waziri Mkuu Atumia Treni Kutoka Dodoma Kwenda Dar es saalam

WAZIRI MKUU AKIENDELEA NA MAJUKUMU YAKE NDANI YA TRENI WAKATI AKISAFIRI KUTOKA DODOMA KUELEKEA DAR ES SAALAM

Dkt. Stergomena Lawrence Tax Aukabidhi Ukumbi wa Ccm Magu Baada ya Ukarabati

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mheshimiwa Dkt. Stergomena Lawrence Tax (Mb) tarehe 15 Agosti 2025, ameukabidhi Uongozi wa Chama cha Mapinduzi CCM wilayani Magu Mkoa Mwanza, Ukumbi wa CCM baada ya kukamilisha maboresho na ukarabati mkubwa.  Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo yaliyofanyika viwanja vya Ofisi ya CCM Magu, Dkt. Tax, alieleza kuwa amekamilisha ukarabati huo ikiwa ni utekelezaji wa maombi yaliyowasilishwa kwake na Kamati ya Siasa ya Wilaya ikiwa mchango wake kama Mwana CCM na Mwana Magu. Aidha, amewakumbusha wana CCM Magu, kuendelea kutoa ushirikiano na kuwatia moyo kwa kuwaunga mkono Viongozi na wanachama wanaojitilea kuchangia katika shughuli za maendeleo katika jamii, ili kuwapa hamasa na kuondokana na mtazamo hasi kuwa wanaojitolea  wanataka nafasi za Uongozi, Mitazamo ya aina hiyo hufifisha ari.  Naye Mwenyekiti wa CCM Magu, Komredi Enos Ndobeji Kalambo kwa niaba ya wana CCM Magu, alimshukuru Waziri Tax, kwa moyo wake wa kujitoa na kuainis...

Kikwete: Serikali Kusaini Muongozo Wa Kima Cha Chini Cha Mshahara Kwa Sekta Binafsi

SERIKALI imesema hivi karibuni inatarajia kusaini kuwa Sheria miongozo Wa kima cha chini Cha mshahara kwa TaasisiI binafsi zinazofanywa kazi nchini. Imesema katika miongozo huo inatarajia kuainisha viwango vipya vya mshahara ambapo wafanyakazi Wa sekta binafsi watakuwa wanalipwa. Waziri Wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi,Ajira  Vijana Na Wenye Ulemavu  ,Ridhiwan Kikwete amesema hayo jijini Arusha katika uzinduzi wa jengo la  biashara Shirikisho La Vyama Vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) lililoko mkabala na soko kuu. Kuhusu miongozo huo amesema mazungumzo yameshafanyika baina ya wadau ambao ni Taasisi binafsi na wasimamizi wa sera lakini pia uongozi wa timu Ya Wizara iliyopewa jukumu la kusimamia marekebisho hayo. Amesema kikao kilichobakia ni Cha mashauri ambapo watashauriana na wenzao juu ya viwango vilivyowekwa na baada ya hapo mapema mwezi ujao huenda wakasaini marekebisho hayo. “Hivyo nawaambia Wafanyakazi kuwa Rais Dkt Samia anathamini sana maslahi yenu,” amesema Ridhi...

Serikali yampongeza Dk Rweikiza kwa uwekezaji sekta ya elimu

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imempongeza Mkurugenzi wa shule ya St Anne Marie Academy ya Mbezi Kimara kwa Msuguri jijini Dar es Salaam, Dk Jasson Rweikiza kwa uwekezaji mkubwa ambao ameufanya kwenye sekta ya elimu. Pia imeipongeza shule hiyo kwa kuendelea kufanya vizuri kitaaluma mwaka hadi mwaka katika mitihani ya kitaifa. Pongezi hizo zilitolewa mwishoni mwa wiki na Beatrice Mbawala aliyemwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Albert Msando, kwenye mahafali ya 21 ya kidato cha nne ya shule hiyo. “Nimeambiwa hapa kwamba kuna watumishi zaidi ya 350 sasa kama shule ya St Anne Marie Academy isingekuwepo hawa wangekuwa wapi, na hawa wanandugu na jamaa wanaowategemea kwa hiyo serikali inajivunia uwekezaji huu kwasababu umepunguza tatizo la ajira nchini,” alisema Alisema hata maendeleo ya taaluma ya shule hiyo yamekuwa yakiridhisha mwaka hadi mwaka kuanzia matokeo ya mitihani ya ngazi ya Wilaya, Mkoa na Taifa kwa kufanya vizuri kitaaluma. “Nimejionea maonesho mbalimbali ya kitaaluma, yaani wanaf...

Serikali Tunajivunia Mchango wa Taasisi za Dini Kimaendeleo - Dkt. Biteko

📌 Dkt. Biteko amwakilisha Makamu wa Rais, Dkt Philip Mpango maadhimisho ya miaka 125 Parokia ya Kome - Geita 📌 Rais Samia achangia Tsh.Milioni 50 Ujenzi wa mradi wa maji Parokia ya Kome 📌 Maaskofu Waishukuru Serikali kwa ushirikiano na Taasisi za dini Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema Serikali  itaendelea kuziunga mkono na kushirikiana na taasisi zote za dini ili kuleta na kuchagiza maendeleo na Ustawi wa wananchi. Dkt. Biteko amesema hayo Agosti 17, 2025 wakati akimwakilisha  Makamu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Mpango kuwa mgeni maalum katika maadhimisho ya  miaka 125 ya Ukristo na Uinjilishaji katika Parokia ya Kome, Jimbo Katoliki la Geita. “ Niseme Serikali itaendelea kushirikiana na taasisi zote za dini katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo na hii ni kuhakikisha wananchi wanapata maendeleo” amesema Dkt. Biteko na kuongeza kuwa Serikali inafarijik...

Mwenge wa Uhuru wazindua Daraja la Kinyang'erere

#Wananchi watakiwa kuitunza miundombinu hiyo  Mara. Jumla ya shilingi Milioni 148.5 zimetumika Kujenga Daraja la kinyang'erere lililopo katika kijiji cha kinyang'erere halmashauri ya Musoma Mkoani Mara. Akisoma Taarifa ya ujenzi wa Mradi huo Kaimu Meneja wa TARURA Wilaya ya Musoma Mhandisi Mohmed Etanga amesema daraja hilo limekamilika ujenzi wake kwa asilimia mia moja na kutoa huduma kwa Wananchi kama ilivyo kusudiwa. Mhandisi Etanga ameongeza kuwa daraja hilo ni kiungo muhimu kwa wakazi wa kijiji hicho kwaajili ya usafirishaji wa Mazao na kwenda kupata huduma za kijamii katika vijiji vingine ambapo kuna kituo cha Afya pamoja na wanafunzi kuvuka kwenda shule. Ameongeza kuwa kipindi cha Masika wakazi hao walikuwa wakipitia kadhia ya kushindwa kuvuka mto ambao unakuwa umejaa maji jambo lilikuwa likisababisha baadhi ya wajawazito kujifungulia njiani na kushindwa kuuza mazao yao kutokana na ubovu wa barabara . Naye Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa Ndugu Ismail Ali Ussi ameipon...