Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mheshimiwa Dkt. Doto Mashaka Biteko amekutana na Waziri wa Nishati wa Umoja wa Visiwa vya Comoros, Dkt Aboubacar Anli na kukubaliana maeneo kadhaa ya ushirikiano katika Sekta ya Nishati. Awali, Waziri wa Nishati wa Comoros alieleza umuhimu wa ushirikiano kwenye sekta hiyo baina ya Comoro na Tanzania hususan kuanza mazungumzo kwa ngazi ya wataalam ili kufanya upembuzi wa maeneo muhimu ya kuanzia hususan katika uzalishaji na usambazaji umeme kwenye visiwa hivyo akieleza pia azma ya Serikali yao kuzalisha umeme kwa vyanzo vya nishati ya mvuke (Geo Thermal) inayopatikana kwa wingi visiswani humo. Aidha, aliipongeza Serikali ya Tanzania kwa maandalizi mazuri na mkutano wa mafanikio wa Wakuu wa Nchi kuhusu Nishaki uliomalizika hivi karibuni. Kwa upande wake, Naibu Waziri Mkuu Dkt.Biteko alieleza utayari wa Tanzania katika kushirikiana na Comoro kwenye maeneo tajwa na kuelekeza taratibu rasmi ili kuweza kufikiwa makubaliano rasmi kwenye Sekta...
Marato tv - Sauti ya Jamii