Skip to main content

Posts

Showing posts from September 28, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Mwenyekiti ccm Musoma akumbusha umuhimu wa kufanya mazoezi

Na Shomari Binda-Musoma Viongozi wa Chama cha Mapinduzi(CCM) Wilaya Musoma mjini wamekuwa miongoni mwa wananchi waliojitokeza kushiriki mazoezi ya" jogging" yaliyoandaliwa na mkuu wa Wilaya ya Musoma Juma Chikoka. Mazoezi hayo yamefanyika leo septemba 28 yaliyoanzia na kumalizikia kwenye uwanja wa posta ambapo licha ya viongozi hao makundi mbalimbali yameshiriki. Akizungumza mara baada ya mazoezi hayo Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Musoma Benedict Magiri amemshukuru na kumpongeza mkuu huyo wa Wilaya kwa kuanzisha utaratibu huo muhimu kwa afya. Amesema mazoezi yana umuhimu mkubwa katika kufanya mwili kuwa na afya njema na kuweza kutekeleza vyema shughuli za kiuchumi. Magiri amesema ilani ya uchaguzi ya CCM inazungumzi pia ushiriki wa michezo na wao kama viongozi wanamuunga mkono kwa kuhamasisha wanachama na wananchi kushiriki mazoezi na michezo. Mkuu wa Wilaya ya Musoma Juma Chikoka kwa upamde wake amesema anataka Musoma iliyochangamka kwa matukio ya mara kwa mara yakiwemo ya kim...

Rais Samia aahidi serikali kufikisha asilimia hamsini kilimo cha umwagiliaji ifikapo 2030

Na NIRC Songea, Ruvuma Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema serikali imejipanga kuinua Sekta ya umwagiliaji kwa 50%, ifikapo 2030 “Serikali imewekeza katika sekta ya umwagiliaji, na ifikapo 2030, kilimo cha umwagiliaji kinatarajiwa kufikia asilimia 50 ya kilimo nchini”, amesema Rais Samia Samia amesema hayo wakati akihutubia wananchi katika Viwanja vya Majimaji mkoani Ruvuma, ambapo amezungumza na wananchi kuhusu ziara yake hiyo mkoani humo, na kueleza mafanikio, mipango na maagizo mbalimbali ya serikali Rais Samia amesema alikagua ununuzi wa mahindi katika maghala ya NFRA na kuweka jiwe la msingi kwa ujenzi wa maghala 28 yenye uwezo wa kuhifadhi tani 28,000 za mazao ya nafaka, kisha alitembelea shamba la kahawa la Aviv na kusisitiza umuhimu wa kilimo cha kahawa.  Rais Samia ameongeza kuwa Serikali imetoa ruzuku ya mbolea yenye thamani ya bilioni 83.5, huku matumizi ya mbolea yakiongezeka kutoka tani 32,139 mwaka 2022 hadi tani 123,049 mwaka 20...

Wahitimu darasa la saba waonywa kupokea zawadi zinazoweza kukatisha ndoto zao

Mwandishi wetu Mwanza Mjumbe wa Bodi ya Shirika la EMEDO Bwana Edwin Soko amewataka wahitimu wa Darasa la Saba Shule ya Msingi Sweya kujiepusha na vishawishi vya zawadi na fedha toka mitaani wakati huu wanaposubiri matokeo yao ya kuendelea na masomo ya Sekondari. Soko ameyasema hayo alipokuwa Mgeni rasmi kwenye maafali ya 21 ya Shule ya Msingi Sweya, iliyopo kata ya Luchelele, Wilaya ya Nyamagana Mkoa wa Mwanza. Soko alisema kuwa, Kwa sasa kuna vishawishi vingi huko  Mitaani na wajibu wao wahitimu kujilinda na vishawishi hivyo ili waendelee kubaki salama na kuendelea na masomo yajayo ya Sekondari. Soko pia aliwataka wazazi kuwalinda watoto wawepo Nyumbani maana vitemdo vya ubakaji na ulawiti vinazidi kuongezeka na watoto ni kundi lililo kwenye hatari. Edwin Soko alikuwa Mgeni rasmi aliyemwakilisha Mkurugenzi wa Shirika la EMEDO alisema shirika hilo litatoa mashine ya kurudufusha karatasi (Photocopy machine ) ili kutatua changamoto za kitaaluma shuleni hapo. Jumla ya wahitimu 102 wa...

TECMN Watumia Burudani Kutoa Elimu ya Kupambana na Ukatili na Ndoa za Utotoni

Na Elizabeth Cornely WADAU wa Mtandao wa Kutokomeza Ndoa za Utotoni Tanzania(TECMN), umeendelea na ziara yake wilayani Nzega mkoani Tabora kwa kutoa elimu ya namna ya kupambana na ukatili pamoja na ndoa za utotoni. Mtandao huo unaoundwa na mashirika zaidi ya 80, katika ziara hiyo unawakilishwa na machache ikiwamo Msichana Initiative, Binti Makini Foundation, Theatre Arts Feminist Group, Medea Tanzania, Plan International na My Legacy. Katika kijiji cha Isagenhe wilayani humo, wadau wa mtandao huo waliendelea kutoa elimu kwa njia mbalimbali ikiwamo kwa kutumia nyimbo na burudani kwa lugha asili ya wakazi wa eneo hilo. Wadau hao wanafanya ziara ya kutoa elimu ya kupambana na ukatili na ndoa hizo za utotoni kwa mikoa ya Mara, Shinyanga, Tabora na Dodoma ambayo kwa takwimu inaonyesha iko juu katika ndoa hizo za utotoni. Kwa mujibu wa takwimu za utafiti wa Demografia na Afya(TDHS) za mwaka 2015/2016, asilimia 36 ya wasichana  Tanzania wanaolewa kabla ya kufikia umri wa miaka 18 huku mik...

Waziri mkuu ahutubia baraza kuu la umoja wa mataifa mbele ya wakuu wa nchi mbalimbali

 Asema SDGs ni msingi wa matumaini Waziri Mkuu Kasimu Majaliwa amehutubia Mkutano wa 79 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UNGA79) na kusema Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) ni msingi wa matumaini katika kukabiliana na changamoto za kidunia. Hii ni mara ya pili kwa Waziri Mkuu wa Tanzania kuhutubia Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ambapo mara ya kwanza ilikuwa Septemba 27, 2010 wakati Waziri Mkuu Mstaafu, Mizengo Kayanza Pinda alipolihutubia Baraza la 65 (UNGA65). Ametoa kauli hiyo jana (Ijumaa, Septemba 27, 2024) wakati akihutubia kwenye Mkutano Mkuu wa Mwaka huu wa Umoja wa Mataifa wa Wakuu wa Nchi mbalimbali za dunia jijini New York, Marekani anakomwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan. Alisema chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia, Tanzania imedhamiria kufanikisha malengo endelevu ya kiuchumi, ufugaji, uwekezaji katika miundombinu na mifumo ya kidijitali, uvuvi na nishati. “Lengo letu ni kufikia uhakika wa kupunguza umasikini, kutengeneza ajira mpya na kusukuma mbele maendele...