_▪️Ataka matokeo ya tafiti hizo yatumike badala ya kuyafungia_ _▪️Awataka wadau wa Sekta ya Afya kuongeza uwekezaji katika vifaa tiba na teknolojia mpya_ WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ametoa wito kwa watafiti na wapangaji wa Sera kuwekeza katika tafiti zenye tija kwa wananchi.
Amesema kufanya hivyo, kutawezesha kuwa na matokeo ambayo yatatumika kutengeneza sera na mipango ya utekelezaji yenye kuleta mabadiliko halisi katika jamii.
Ametoa wito huo leo Jumatano (Juni 18, 2025) kwenye Kongamano la 13 la Kisayansi la Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) lililofanyika chuoni hapo kampasi ya Mloganzila, jijini Dar es Salaam.
“Tunataka kuona matokeo ya tafiti hizi yanatumika, msiweke tafiti hizi kwenye makabati tu, matokeo haya yanapaswa kuleta tija katika sekta ya afya, Ni matarajio yangu kuwa kongamano hili litatumika kutoa mapendekezo yatakayoimarisha mifumo, sera, na ushirikiano baina ya sekta ya umma na binafsi ili kuhakikisha Watanzania wananufaik...
Marato tv - Sauti ya Jamii