_Ni sehemu ya magari 89 na pikipiki 140 zinazotarajiwa kununuliwa_ _Lengo kuboresha Sekta ya Madini_ _Aagiza Magari kufungwa GPS_ _Ampongeza Rais Samia kwa kuiongezea bajeti Wizara ya Madini_ *DODOMA* Ikiwa ni mkakati wa kuimarisha usimamizi katika Sekta ya Madini hasa kwenye ukusanyaji wa maduhuli, Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde amezindua magari mapya 25 kwa ajili ya kusambazwa kwenye Ofisi za Maafisa Madini Wakazi wa Mikoa sambamba na kukabidhi magari hayo kwa Maafisa Madini Wakazi wa Mikoa waliohudhuria uzinduzi huo. Uzinduzi huo umehudhuriwa pia na Naibu Waziri wa Madini, Mhe. Dkt. Steven Kiruswa, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Msafiri Mbibo, Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Mhandisi Ramadhani Lwamo na watendaji wengine kutoka Wizara ya Madini na Taasisi zake. Akizungumza kwenye uzinduzi huo, Mhe. Waziri Mavunde amesema kuwa Wizara imepanga kununua magari 89 na pikipiki 140 kama sehemu ya uboreshaji wa usimamizi wa Sekta ya Madin...
Marato tv - Sauti ya Jamii