Skip to main content

Posts

Showing posts from April 13, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Mhe. Ghati Chomete Ashiriki Ziara ya Kamati ya Bunge ya Viwanda Tanga, Atembelea Viwanda Vitatu Kwa Mpigo

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mara, Mhe. Ghati Zephania Chomete, ameshiriki ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo, Mifugo na Uvuvi iliyofanyika jijini Tanga, ikiwa ni sehemu ya ufuatiliaji wa maendeleo ya sekta ya viwanda nchini.  Ziara hiyo imelenga kujionea hali halisi ya uzalishaji viwandani, tathmini ya mchango wa sekta ya viwanda katika uchumi wa taifa, pamoja na kubaini changamoto zinazokwamisha ufanisi wa uzalishaji. Katika ziara hiyo, Kamati ilitembelea viwanda vitatu vikubwa vilivyopo jijini humo ambavyo ni Tanga Cement PLC, Yogi Polypack Ltd na Neel Kanth Chemical Ltd, ambapo wajumbe walijionea mchakato wa uzalishaji, ubora wa bidhaa, pamoja na mchango wa viwanda hivyo katika kutoa ajira na kukuza mnyororo wa thamani. Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mhe. Ghati Chomete alieleza umuhimu wa kuendelea kuimarisha mazingira ya uwekezaji katika sekta ya viwanda ili kuongeza tija, kuchochea ukuaji wa uchumi, na kuongeza ushindani wa bidhaa za Tanzania ...

Sekta ya Nishati Yapiga Hatua Mpya: Taifa Gas Yachukua Hisa Songosongo

SEKTA ya nishati nchini Tanzania imeingia katika hatua mpya ya mageuzi baada ya kampuni ya Taifa Gas Tanzania Limited kutangaza makubaliano ya kununua hisa katika biashara ya gesi ya Orca Energy Group Inc., hatua inayotarajiwa kuimarisha ushiriki wa wazawa katika rasilimali za kimkakati. Kwa mujibu wa taarifa ya Aprili 13, 2026, Taifa Gas itanunua asilimia 49 ya hisa katika PanAfrican Energy Corporation, huku Amber Energy Investment L.L.C-FZ ikishikilia asilimia 51 iliyobaki. Makubaliano hayo pia yanahusisha ununuzi wa asilimia 100 ya shughuli za Orca nchini Tanzania, zikiwemo haki zote katika mradi wa gesi wa Songo Songo Gas Field, ambao ni chanzo kikuu cha gesi inayochangia uzalishaji wa umeme na maendeleo ya viwanda. Hatua hiyo inaonekana kama mabadiliko makubwa katika sekta ya nishati, ambapo umiliki wa ndani unaendelea kupewa nafasi kubwa zaidi katika usimamizi wa rasilimali muhimu za taifa. Akizungumzia makubaliano hayo, mfanyabiashara Rostam Aziz amesema lengo ni kuhakikisha Tan...

Dcea Yakamata Kilo 1,983 za Dawa za Kulevya, Yabaini Mitandao Mipya

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imesema imefanikiwa kukamata jumla ya kilogramu 1,983.31 za dawa za kulevya katika operesheni zilizofanyika nchini kote mwezi Machi 2026, huku mitandao mipya ya usafirishaji ikibainika. Akizungumza jijini Dar es Salaam, Kamishna Jenerali wa DCEA, Aretas Lyimo, amesema mafanikio hayo yanatokana na mkakati wa Mamlaka kujikita zaidi katika operesheni za mashambani na kwenye njia kuu za usafirishaji baada ya kuimarisha udhibiti bandarini na mipakani. “Katika kipindi cha mwezi Machi 2026, tumekamata jumla ya kilogramu 1,983.31 za dawa za kulevya aina mbalimbali, pamoja na kilogramu 3,012.5 na lita 17,960 za kemikali bashirifu ambazo zingetumika kuzalisha dawa hizo,” amesema Lyimo. Ameeleza kuwa ongezeko kubwa limeonekana katika ukamataji wa mirungi, ambapo pekee yake ilifikia kilogramu 1,267.12 sawa na asilimia 64 ya dawa zote zilizokamatwa katika kipindi hicho. Kwa mujibu wa Kamishna huyo, opereshe...

Tanzania lazima inufaike na rasilimali zake za asili - Rostam Aziz

Kampuni ya Taifa Gas Tanzania Limited inayomilikiwa na mfanyabiashara Rostam Aziz, imeingia makubaliano ya kununua sehemu ya hisa katika biashara ya gesi ya Orca Energy Group Inc. nchini Tanzania, hatua inayotajwa kuwa ya kihistoria katika sekta ya nishati. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Aprili 13, 2026, Taifa Gas itanunua asilimia 49 ya hisa za kampuni ya PAE PanAfrican Energy Corporation (PAEM), huku kampuni ya Amber Energy Investment L.L.C-FZ ikichukua asilimia 51 iliyobaki. Makubaliano hayo yanahusisha uuzaji wa asilimia 100 ya biashara ya Orca nchini Tanzania, ikiwemo haki zake zote katika mradi wa gesi wa Songo Songo, ambao ni mhimili muhimu wa uzalishaji wa gesi kwa matumizi ya umeme na viwanda. Hatua hiyo inatajwa kuwa sehemu ya mabadiliko makubwa ya umiliki katika sekta ya gesi, ambapo wawekezaji wa ndani wanaanza kuchukua nafasi kubwa zaidi katika rasilimali za kimkakati. Akizungumzia maendeleo hayo, Rostam alisema mpango huo umechukua muda mrefu kuandaliwa na unalenga kuh...

Dkt.Mwigulu aongoza harambee ya kuchangia sherehe za Mei Mosi 2026

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Aprili 13, 2026 ameongoza harambee ya kuchangia sherehe za Mei Mosi ambazo mwaka huu kitaifa zitafanyika mkoani Njombe. Katika harambee hiyo kiasi cha shilingi bilioni 1.105 kilichangishwa

Wateja wa Benki ya Azania kufaidika na Huduma mpya ya Malipo ya Azania Lipa

Benki ya Azania imezindua rasmi huduma mpya ya malipo ya kidijitali ijulikanayo kama Azania Lipa, ikiwa ni sehemu ya kuendeleza mkakati wake wa kuboresha huduma za kifedha kupitia teknolojia na kuleta urahisi zaidi kwa wateja wake. Huduma ya Azania Lipa ni mfumo wa kisasa unaowawezesha wateja kufanya malipo kwa urahisi kupitia QR code, namba ya malipo (till number), pamoja na kutumia simu za mkononi kupitia Mobile Banking au USSD. Mfumo huu umeundwa kuunganisha huduma za benki, mitandao ya simu na wafanyabiashara katika jukwaa moja lenye ufanisi. Uzinduzi wa Azania Lipa umeongozwa na Mkuu wa Kitengo cha Ubunifu na Mikakati, Ndg. Jackson Lohay ( wanne kutoka kushoto) Benki hiyo imewahimiza wafanyabiashara, wajasiriamali na wananchi kwa ujumla kuanza kutumia Azania Lipa ili kufurahia urahisi, usalama na ufanisi wa huduma hiyo mpya. Uzinduzi wa Azania Lipa unaendelea kudhihirisha dhamira ya Benki ya Azania ya kuwa mstari wa mbele katika utoaji wa suluhisho bunifu za kifedha zinazokidhi ma...

Rais Samia Afanya Mazungumzo na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amekutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) Mhe. Balozi Stephen Mbundi, Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma tarehe 13 Aprili, 2026.

Dkt. Mwigulu Ateta na Balozi wa Slovakia Nchini

Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba leo Aprili 13, 2026 amefanya mazungumzo na Balozi wa Slovakia nchini Tanzania, Ivan Lancaric ofisini kwake Bungeni jijini Dodoma.