Skip to main content

Posts

Showing posts from April 27, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Bunge Lapitisha Bilion 174.9/- Kwa Wizara ya Madini

*●Yalenga kuchangia trilioni 1.4/- za maduhuli* *●Makusanyo yafikia Trilioni 1 na Milioni 156* *●Jumla ya tani 23.8 za dhahabu zakusaywa ndani ya miezi 18* *●Ni Juhudi za Rais.Dkt.Samia Suluhu Hassan* *Dodoma* Bunge la Jamhuru ya Muungano wa Tanzania, limeridhia na kupitisha bajeti ya Wizara ya Madini ya shilingi bilioni 174.9 kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027 ili kuiwezesha Wizara ya Madini kufanikisha ukusanyaji wa maduhuli ya shilingi trilioni 1.4. Akiwasilisha Bungeni makadirio ya Mapato na Matumizi leo Aprili 27, 2026, Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde amesema fedha hizo zitawezesha kufanikisha utekelezaji wa majukumu ya Wizara pamoja na taasisi zilizo chini yake, huku zikilenga kuendeleza kasi ya ukuaji wa sekta ya madini kwa kufanya tafiti za jiosayansi nchini. Akifafanua mgawanyo wa Bajeti hiyo, Waziri Mavunde amesema kiasi cha  shilingi bilioni 71.5 sawa na asilimia 40.9 zimetengwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo, wakati shilingi bilioni 103.5 sawa na asilimia 59.1 zikiwa...

Waziri Mkuu Atimiza Ahadi ya Pikipiki 10 Kwa Vikundi Vya Bodaboda Rungwe

WAZIRI MKUU,  Dkt. Mwigulu Nchemba, ametimiza ahadi yake ya kutoa pikipiki 10 kwa vikundi vya waendesha bodaboda wilayani Rungwe, mkoani Mbeya, ikiwa ni jitihada za kuwawezesha vijana kiuchumi. Ahadi hiyo ilitolewa Desemba  18, 2025, wakati Waziri Mkuu alipokuwa akizungumza na wananchi wa Kata ya Kiwira, alipokuwa akitoka wilayani Kyela katika ziara ya kikazi. Katika mkutano huo, Furaha Zuberi Mwakyusa aliwasilisha ombi la kupatiwa pikipiki kwa ajili ya vijana wa bodaboda, ambapo Waziri Mkuu aliridhia na kuahidi kutoa pikipiki 10. Pikipiki hizo zimekabidhiwa rasmi na Mkuu wa Wilaya ya Rungwe, Jaffar Haniu, kwa niaba ya Waziri Mkuu, katika hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe, Tukuyu. Katika hafla hiyo, Mkuu wa Wilaya pia alikabidhi pikipiki ya magurudumu matatu (bajaji) kwa Richard Mgongo, Mtendaji wa Kata ya Kiwira mwenye mahitaji maalum, ikiwa ni utekelezaji wa ahadi nyingine ya Waziri Mkuu aliyoitoa siku hiyo hiyo. Akizungumza wakati wa makabi...

CCM na CPC: Maandalizi ya Kupokea Ugeni

Katibu wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC), Siasa na Uhusiano wa Kimataifa (SUKI), Ndugu Rabia Abdalla Hamid akiwa kwenye kikao kazi na Kansela wa Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) wa Ubalozi wa China nchini Tanzania, Ndugu Xu Sujiang, leo Jumatatu tarehe 27 Aprili 2026, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, jijini Dar Es Salaam, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kupokea ugeni wa Mjumbe wa Kamati Kuu ya CPC na Waziri wa Mambo ya Nje wa China, Mhe. Liu Haixing, anayetarajiwa kufanya ziara rasmi nchini Tanzania, mwezi Mei 2026.

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Washiriki Tamasha la kilimo Jijini Mbeya, Wahamasisha Nishati Safi ya Kupikia* .

  📍 *Iwambi, Mbeya*  Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unashiriki katika tamasha la kilimo linalofanyika katika viwanja vya Iwambi jijini Mbeya kuanzia tarehe 25 mpaka 29 Aprili 2026, ambapo zaidi ya watu 100,000 wakiwemo vijana kutoka mikoa mbalimbali ya kanda ya nyanda za juu kusini wanatarajiwa kushiriki. Wakala unatumia jukwaa hilo kuelimisha na kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa wananchi pamoja na kueleza hali ya upatikanaji wa huduma ya umeme katika maeneo ya vijijini. Kupitia banda lake, REA imeonesha bidhaa mbalimbali za nishati safi ya kupikia, ambapo bidhaa kuu zinazohamasishwa ni pamoja na matumizi ya majiko ya umeme, majiko ya gesi pamoja na majiko banifu. Teknolojia hizo zimebainishwa kuwa suluhisho muhimu katika kupunguza matumizi ya nishati chafu kama kuni na mkaa, kulinda mazingira na kuboresha afya za watumiaji. Akifungua rasmi maonesho hayo, Kaimu mkuu wa wilaya ya Mbeya ambae pia ni Mkuu wa wilaya ya Mbarali Mhe. Brig. jen. Maulid Hassan Su...