MATOKEO ya wanafunzi wa Gredi ya 9, KJSEA ndiyo yaliyokuwa ya kwanza kutolewa rasmi kupitia Mtaala wa Utendaji na Umilisi (CBE), tukio linaloonyesha jinsi mfumo wa elimu unavyoendelea kubadilika nchini. Zamani kupitia mfumo wa 8-4-4 wanafunzi walitilia mkazo tu alama walizozipata ila mfumo huu unajikita sana katika Vipaji na uelewa mpana wa masomo anayoyapenda mwanafunzi. Chini ya mfumo wa CBE, mwanafunzi anatathminiwa kuanzia Gredi ya Kwanza hadi afanye KJSEA. Chini ya uliokuwa mfumo wa 8-4-4, wanafunzi walikuwa wakifanya Mitihani ya Kumaliza Elimu ya Msingi(KCPE) ambayo alama za mtahiniwa ndizo zilikuwa zikitathminiwa katika kila somo, alama ya jumla ikiwa 500. Hata hivyo, KJSEA inachangia tu asilimia 60 ya alama ya mtahiniwa wa Gredi ya 9. Asilimia 40 zilizosalia nazo hugawanywa ambapo asilimia 20 hutoka kwa mtihani wa Gredi ya 6 KPSEA, kisha asilimia 20 nyingine huchangiwa na alivyofanya mwanafunzi katika masomo ya vitendo shuleni. “Mfumo huu hautegemei alama kati...
Marato tv - Sauti ya Jamii