Skip to main content

Posts

Showing posts from December 14, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

"Tuendelee Kuiunga Mkono Serikali Yetu Kwa sababu ni Serikali Sikivu na inatatua Kero za Wananchi", Mtendaji Mkuu Temesa

  Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) Lazaro Kilahala amewaomba wananchi wa Kanda ya Ziwa na maeneo mengine ya Nchi kuendelea kuiunga mkono Serikali ya Awamu ya Sita inayooongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwakuwa Serikali hiyo ni Serikali sikivu inayowajali wananchi wake kwa kutatua kero zinazowakabili hasa za usafiri wa maji ambao ndio umekuwa tegemeo kubwa kwa wakazi wanaoishi visiwani na pembezoni mwa Ziwa Victoria. Kilahala ameyasema hayo leo Tarehe 15 Desemba, 2024 wakati alipofanya ziara ya kikazi katika eneo la Buyagu Wilayani Sengerema Mkoani Mwanza, kukagua maendeleo ya ujenzi wa maegesho mapya ya kivuko cha Buyagu- Mbalika yanayoendelea kujengwa katika eneo hilo.  Kilahala amesema, katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa, Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, inafanya kazi ya ujenzi wa vivuko vipya vitano huku vitatu kati ya hivyo vikiwa vinatarajiwa kupelekwa katika maeneo ambayo hayakuwahi kabisa kuwa na vivuko hapo awali na viwili ...

Rais Dk.Mwinyi azindua Bodi Mpya ya Bmf

  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi ameishauri Bodi mpya ya Wadhamini ya Taasisi ya Benjamin William Mkapa kuhakikisha inaendelea kuwa chombo cha kuaminika na Watanzania kwenye kuimarisha sekta ya afya ndani na nje ya nchi kama ilivyo Dira ya Taasisi hiyo. Rais Dk Mwinyi ameyasema hayo alipozindua Bodi Mpya ya BMF hafla iliofanyika  Ukumbi wa BMF Kawe, jijini Dar es Salaam. Rais Dk. Mwinyi ambae ni Msarifu wa taasisi ya Benjamin Mkapa Foundation ameeleza kuwa ni vema kwa sifa za wajumbe wa taasisi hiyo  kuendelea kudumu ndani ya taasisi  ili kuwavutia washirika zaidi na kuhakikisha ukuaji endelevu wa  kuwahudumia  walengwa wa taasisi hiyo. Halikadhalika Rais Dk. Mwinyi  amefafanua kuwa   Mpango Mkakati wa Taasisi hiyo utakaodumu kuanzia Julai 2024 hadi Juni 2030  utategemea Bodi na Menejimenti katika kutekeleza  na kufikia malengo yaliowekwa na kusisitiza umuhimu wa kudumisha rekodi nzuri y...

Ukaguzi wa Magari ya Kubeba Wanafunzi Wang'oa Nanga Mwanza

Na Kutoka Dawati la Habari Polisi Mwanza Jeshi la Polisi mkoa wa Mwanza limezindua zoezi la ukaguzi wa magari ambapo limeanza na ukaguzi wa magari yanayobeba wanafunzi wa shule kabla ya mhula wa masomo kuanza na baadaye kukagua magari ya abiria na mizigo. Uzinduzi wa ukaguzi huo umefanyika leo Disemba 14, 2024 katika kituo kikuu cha mabasi ya mikoani Nyamhongoro kilichopo Wilaya ya Ilemela Jijini humo.  Lengo la ukaguzi huo ni kuhakikisha vyombo vyote vya moto vinavyotumika katika barabara za umma vinakuwa na ubora kwa matumizi ya umma na kubaini magari yasiyokidhi vigezo kisheria ikiwa ni mkakati wa kuzuia ajali zitokanazo na ubovu wa magari hayo. Akizungumza na wamiliki wa shule, wasimamizi wa sheria, madereva na wadau wa usafirishaji mkoa wa Mwanza; Mkuu wa Operesheni mkoa wa Mwanza, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Aloyce Nyantora kwa niaba ya Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza amesema zoezi hilo ni la hiari kwa sasa na amewataka wamiliki kupeleka magari yao kukaguliwa kabla ya ...

Ccm Mara yawapa Tano Wananchi Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

Chama cha mapinduzi mkoa wa Mara kimefanya kikao chake cha kawaida cha halmasha kuu ya mkoa kwa ajili ya kujadili na kuweka mikakati mbalimbali ya kiasiasa ya kuwezesha kushinda na kushika dola. Katika kikao hicho cha kawaida ambacho kimefanyika mjini Musoma chini ya mwenyekiti wake Patrick Chandi pamoja na mambo mengine kimefanya tathimini ya uchaguzi wa Serikali za mitaa ulifanyika mwisho mwa mwezi novemba mwaka 2024. Pia kikao kimewashukuru wanachama na wananchi ambao wamekiwezesha chama hicho kushinda kwa kishindo katika uchaguzi huo. Katika kikao hicho wajumbe wameendelea kumshukuru mwenyekiti wa Taifa wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Dr Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha nyingi za utekekezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoa wa Mara. Kwa sababu hiyo, kikao hicho kimeendelea kuwaomba Watanzania kumuunga mkono Rais Samia na serikali inayoongozwa na CCM na kwamba CCM inaridhishwa na utekelezaji mkubwa wa ilani ya uchaguzi.

Waziri Mkuu atembelea Kiwanda cha Dawa za Binadamu, Kigamboni

_Awataka kuwekeza katika ubora wa dawa_ _Pia akagua utekelezaji wa maagizo yake ya uwekaji wa taa barabarani, Kigamboni_   WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo Desemba 14, 2024 ametembelea kiwanda cha kutengeneza dawa za binadamu cha CURE AFYA kilichopo Kigamboni jijini Dar es Salaam. Akizungumza baada ya kushuhudia uzalishaji wa dawa kwenye kiwanda hicho chenye thamani ya takribani shilingi bilioni 50, Waziri Mkuu amesema kuwa Serikali inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan itaendelea kuweka mazingira rafiki ya uwekezaji ili kuhakikisha wawekezaji wanapata faida kutokana na shughuli zao. “Serikali imefanya uwekezaji mkubwa kwenye ujenzi wa miundombinu ya utoleaji huduma za afya nchini, na sasa tunahitaji kupata dawa na vifaa tiba kwa ajili ya kuendelea kuongeza nguvu kwenye utoaji huduma, hivyo uwekezaji huu una tija kwa Taifa letu”. Kadhalika, Mheshimiwa Majaliwa ametoa wito kwa wawekezaji hao kuendelea kutengeneza dawa zilizo katika ubora unaokubalika katika viwang...

Serikali yabainisha Mikakati ya Kurejesha hadhi ya Madini ya Tanzanite

-Waziri Mavunde azindua mnada wa ndani Mirerani leo. - Minada ya ndani na nje ya nchi kutumika kutangaza madini ya vito. -Madini yote yatakayokosa wanunuzi kurejeshwa kwa wahusika -Wadau waonesha nia ya kujenga Mji wa Kimadini Mirerani Mirerani MANYARA: Waziri wa Madini Mheshimiwa Anthony Mavunde amesema Serikali imejidhatiti kurudisha hadhi ya Tanzanite kwa kufanya minada ndani na nje ya nchi ili kuyaongezea thamani na wafanyabiashara waweze kunufaika na kuongeza pato la taifa kwa ujumla. Waziri Mavunde ameyasema hayo leo Desemba 14, 2024 Mirerani mkoani Manyara wakati akizindua mnada wa madini ya vito ambao mara  ya mwisho ulifanyika mwaka 2017. Mheshimiwa Mavunde amesema mojawapo ya maeneo yanayosaidia kuongeza mapato ni pamoja na kudhibiti biashara ya madini, kuzuia utoroshaji na kuifanya biashara hiyo kuwa katika mfumo sahihi, uwepo wa minada utachochea uongezaji thamani ya madini ya vito. “Madini ya Vito  yananunuliwa kwa asilimia kubwa kwa ajili ya ‘luxury’ ni ufahari n...