Dhana kwamba elimu ya ufundi stadi ni kwa watu waliokosa fursa za elimu ya juu inaendelea kupotea, huku wahitimu wenye vyeti, stashahada, shahada na hata shahada za uzamili wakijitokeza kujiunga na mafunzo ya ufundi stadi ili kuongeza ujuzi na kukidhi mahitaji ya soko la ajira. Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), CPA Anthony Kasore, amesema katika kipindi cha mwaka 2022/2023 hadi 2025/2026, jumla ya waombaji 794 wa mafunzo ya ufundi stadi walikuwa tayari na elimu za juu katika taaluma mbalimbali. Amesema kati yao, 522 walikuwa na vyeti vya taaluma nyingine, 120 walikuwa na stashahada, 151 walikuwa na shahada na mmoja alikuwa na shahada ya uzamili. Kasore ameyasema hayo leo, Septemba 4, 2026, jijini Dodoma, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu nafasi ya VETA katika kujenga Taifa lenye wananchi wenye ujuzi. Amesema ongezeko hilo linaonesha mabadiliko makubwa katika mtazamo wa jamii kuhusu elimu ya ufundi stadi, ambayo kwa muda mrefu ime...
Marato tv - Sauti ya Jamii