Skip to main content

Posts

Showing posts from June 13, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

SERIKALI YADHAMIRIA KUWAENDELEZA WACHIMBAJI WADOGO NCHINI

 ▪️Taarifa ya mapendekezo ya kuwaendeleza Wachimbaji wadogo yawasilishwa ▪️Prof Mkumbo aeleza umuhimu wa sekta ya madini kufikia Dira 2050 Lengo ni Kuongeza Ajira, Kupunguza Umaskini na Kukuza Uchumi ▪️Mfuko wa Dhamana kutatua changamoto ya mitaji kwa wachimbaji ▪️Serikali yaanzisha mfuko wa Madini kwa ajili ya Utafiti wa Madini 📍 Dar Es Salaam Serikali imesisitiza kufanyia kazi kwa haraka Mapendekezo yaliyotolewa na Timu ya Wataalamu iliyoundwa Kuishauri Wizara ya Madini kuhusu namna ya Kuwaendeleza Wachimbaji Wadogo Kiuchumi na kueleza kuwa, utatuzi wa changamoto za Mitaji, Teknolojia na upatikanaji wa taarifa sahihi za Kijiolojia kwa Wachimbaji Wadogo wa Madini ni hatua muhimu ya kuongeza ajira kwa watanzania, kupunguza umaskini na kukuza uchumi wa Taifa kuelekea Dira 2050. Hayo yamebainishwa Juni 13, 2026 jijini Dar Es Salaam na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Mipango na Uwekezaji, Profesa Kitila Mkumbo, wakati wa hafla ya Kupokea Mapendekezo ya Kuwaendeleza Wachimbaji Wadog...

WAZIRI MKUU: FEDHA ZA MAJI, BARABARA NA UMEME KWENDA MOJA KWA MOJA KWENYE MIFUKO HUSIKA

 Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali imewasilisha bungeni mapendekezo yatakayowezesha fedha za miradi ya maendeleo katika sekta za maji, barabara na nishati kupelekwa moja kwa moja kwenye mifuko husika ili kuongeza kasi ya utekelezaji wa miradi na kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi. Dkt. Mwigulu amesema hayo leo, Jumamosi Juni 13, 2026, alipokuwa akizungumza na wananchi wa Tarafa ya Ndago katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Shule ya Msingi Ndago, Wilaya ya Iramba mkoani Singida. Amesema hatua hiyo inalenga kuhakikisha fedha zinazotengwa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi zinafika moja kwa moja katika sekta husika na kuwezesha utekelezaji wa miradi kufanyika kwa ufanisi na kwa wakati. “Fedha zote zinazokwenda kwenye barabara, maji na umeme hazitapita tena kwenye Mfuko Mkuu wa Serikali. Zitakwenda moja kwa moja kwenye mifuko husika ili kuhakikisha utekelezaji wa miradi unaongezeka kasi,” amesema Dkt. Mwigulu. Waziri Mkuu amesema hatua hiyo itaon...

WASIRA AMJULIA HALI MANGULA

 Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Ndugu Stephen Wasira, leo tarehe 13 Juni, 2026, amemtembelea na kumjulia hali Makamu Mwenyekiti Mstaafu wa CCM Bara, Ndugu Philip Mangula, katika makazi yake jijini Dodoma.

RAIS DKT. MWINYI AJUMUIKA KATIKA MAZISHI YA MSANII MKONGWE, MAREHEMU MZEE ONYANGO

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, leo tarehe 13 Juni 2026, amejumuika na wanafamilia, ndugu, jamaa, wasanii, na mamia ya waombolezaji katika mazishi ya msanii mkongwe, marehemu Issa Joseph Mohamed, maarufu kwa jina la Mzee Onyango, yaliyofanyika Kawe , Wilaya ya Kinondoni, Jijini Dar es Salaam. Mazishi hayo yamehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akiwemo Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma, pamoja na wasanii wa fani mbalimbali na wananchi waliofika kutoa heshima zao za mwisho kwa marehemu. Mara baada ya kuwasili, Rais Dkt. Mwinyi alisaini kitabu cha maombolezo na kutoa mkono wa pole kwa wanafamilia. Marehemu Issa Joseph Mohamed alizaliwa tarehe 14 Aprili 1950 na kufariki dunia tarehe 11 Juni 2026, akiwa anapatiwa matibabu katika Hospitali ya Jeshi ya Lugalo, Jijini Dar es Salaam. Wakati wa uhai wake, marehemu alipata umaa...

CCM:TANZANIA INAHITAJI HOJA ZA MAENDELEO SIYO MAANDAMANO

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesema Tanzania inahitaji zaidi ujenzi wa hoja za maendeleo kupitia majadiliano ya kidemokrasia na utekelezaji wa mipango ya maendeleo, badala ya maandamano na vitendo vinavyoweza kuhatarisha amani na utulivu wa taifa. Akizungumza na waandishi wa habari leo Jun 13,2026,jijini Dodoma, Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Kenani Kihongosi, amesema CCM itaendelea kusimamia na kuimarisha siasa za maendeleo zinazolenga moja kwa moja kutatua changamoto za wananchi na kuboresha maisha yao. Amesema chama hicho kinaendelea kutekeleza majukumu yake kwa vitendo kupitia ziara mbalimbali za viongozi wake nchini, ambapo hukutana na wananchi katika mikutano ya hadhara na majukwaa tofauti kwa lengo la kusikiliza kero zao na kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu kwa kushirikiana na Serikali. Kihongosi ameongeza kuwa CCM inaelewa vipaumbele vya wananchi ambavyo ni pamoja na huduma bora za afya, maji safi na salama, elimu bora, miundombinu imar...