▪️Taarifa ya mapendekezo ya kuwaendeleza Wachimbaji wadogo yawasilishwa ▪️Prof Mkumbo aeleza umuhimu wa sekta ya madini kufikia Dira 2050 Lengo ni Kuongeza Ajira, Kupunguza Umaskini na Kukuza Uchumi ▪️Mfuko wa Dhamana kutatua changamoto ya mitaji kwa wachimbaji ▪️Serikali yaanzisha mfuko wa Madini kwa ajili ya Utafiti wa Madini 📍 Dar Es Salaam Serikali imesisitiza kufanyia kazi kwa haraka Mapendekezo yaliyotolewa na Timu ya Wataalamu iliyoundwa Kuishauri Wizara ya Madini kuhusu namna ya Kuwaendeleza Wachimbaji Wadogo Kiuchumi na kueleza kuwa, utatuzi wa changamoto za Mitaji, Teknolojia na upatikanaji wa taarifa sahihi za Kijiolojia kwa Wachimbaji Wadogo wa Madini ni hatua muhimu ya kuongeza ajira kwa watanzania, kupunguza umaskini na kukuza uchumi wa Taifa kuelekea Dira 2050. Hayo yamebainishwa Juni 13, 2026 jijini Dar Es Salaam na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Mipango na Uwekezaji, Profesa Kitila Mkumbo, wakati wa hafla ya Kupokea Mapendekezo ya Kuwaendeleza Wachimbaji Wadog...
Marato tv - Sauti ya Jamii