Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dr Samia Suluhu Hassan, amepongeza kazi kubwa inayofanywa na shirika la usambazaji wa nishati ya umeme nchini TANESCO, huku akisema Serikali imetoa kiasi zaidi shilingi bilioni mia moja kwa ajili ya ujenzi wa njia ya kusafirishia umeme wa gridi kwenda mkoa wa Katavi, pamoja na shilingi bilioni 48 kwa ajili ya kujenga vituo vya kupozea nishati hiyo katika maeneo ya Sikonge,Inyonga na Mpanda. Mhe.Dr Samia ameyasema hayo leo julai 13-2024 wakati akihutubia maelfu ya wananchi wa Inyonga mkoani Katavi wakati wa ukaguzi wa kituo cha kupoozea umeme cha Inyonga ambapo ujenzi wake umefikia asilimia 97 na kuitaka Tanesco kujipanga kusambaza nishati hiyo kwenda kwa wananchi baada kukamilika kwa ujenzi wa miundo mbinu hiyo. Amesema nishati ya umeme ni huduma lakini wananchi wana wajibu kulipia huduma hiyo muhimu kwa maendeleo yao na kwamba watumie nishati hiyo kuwekeza katika shughuli nbakimbali za kiuchumi na hivyo kuharakisha maendeleo ya mkoa huo. Ra...
Marato tv - Sauti ya Jamii