Skip to main content

Posts

Showing posts from August 19, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Rc Mtambi Aongoza Majadiliano ya Uelekeo wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025-2050

MKUU wa mkoa wa Mara  Kanali Evans Mtambi ameongoza majadiliano yaliyohusisha wananchi na viongozi kuelekea maandalizi ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2026-2050. Akizungumza kwenye kikao maalum cha kamati ya ushauri ya mkoa ( RCC ) kilichofanyika agosti 19 kwenye ukumbi wa uwekezaji amesema tayari majadiliano hayo yamefanyika ngazi ya wilaya na sasa ni mkoa kabla ya kupelekwa maoni ngazi ya taifa kwenye tume ya mipango. Amesema Dira ya Taifa ya Maendeleo ni suala la msingi katika masuala mbalimbali hivyo mkoa unayo nafasi kwa wananchi na viongozi kujadiliana Mtambi amesema lengo la kikao hicho ni kutoa fursa kwa wananchi na viongozi wa mkoa wa Mara kutoa maoni yao kuhusu Dira ya Maendeleo ya Taifa ya mwaka 2050 ambayo ipo katika hatua za maandalizi.  “Dira inaonyesha matamanio na vipaumbele vya wananchi,serikali na taasisi binafsi zinapo tamani kufikia kwa muda flani na mipango mbalimbali inawekwa ili kufikia lengo hilo”  Mchakato wa maandalizi ya Dira ya Taifa ya Maendeleo...

Washiriki wa Miss Mara Watakiwa Kuwa Wabunifu

Na Shomari Binda-Musoma MKURUGENZI wa Le Grand Victoria Hotel ya mjini Musoma Rama Msomi Bwana amewashauri washiriki wa shindano la Miss Lake Zone kuwa wabunifu na kuutagaza utalii wa ndani. Kauli hiyo imetolewa kwa  niaba yake na meneja wa hotel hiyo Paul Mutinda alipokuwa akizungumnza nao kwenye kikao na Waandishi wa Habari kilichofanyika ukumbi wa Le Grand Beach. Amesema urembo ni fani na inahitaji ubunifu kama zilivyo fani nyingine ili kuwafanya kuwa juu zaidi na kujitangaza. Mkurugenzi huyo amesema warembo ndio wanaotangaza masuala ya utalii na wakiweka ubunifu wataifanya kazi yao vizuri. Amesema wapo waliofanya fani ya urembo na wamefanikiwa kufika mbali na kuwataka washiriki wa miss lake zone kujitambua na kuwa na tabia njema. Mkoa wa Mara na kanda ya ziwa ni kitovu cha utalii hivyo mkurugenzi anawashauri   kuwa mabalozi wa masuala ya utalii"Amesema. Kwa upande wao washiriki wa shindano la Miss Lake Zone wamesema wamezunguka mkoa wa Mara kwa siku 4 wameona fursa zi...

MTUME KISINZA ATOA PONGEZI KWA RAIS SAMIA

MCHUNGAJI wa Kanisa la Uzima Tele Mtume Samuel Kisinza ameipongeza Serikali ya awamu ya Sita chini ya Dkt Samia Suluhu Hassan kwa jitihada zake inazofanya kwenye sekta mbalimbali hapa nchini ambazo zinachochea ukuaji wa uchumi. Alisema hayo Jana katika Ibada ya Jumapili kwenye Kanisa hilo Nundu Jijini Mwanza ambapo alipongeza kuanza kwa safari za Reli ya Kisasa (SGR),kuanza kwa uzalishaji Umeme kwenye Bwawa la Mwalimu Nyerere, kukaribia kukamilika kwa daraja la Kigongo Busisi na kukamilika kwa Miradi ya kimkakati katika Mikoa mbalimbali. Mtume Kisinza amesema jitihada hizo zimedhihirika katika maeneo ya sekta za kilimo,uvuvi,mifugo,usafirishaji,elimu,Afya ambapo mikoa yote hapa nchini imeguswa na kazi za Serikali ya Awamu ya Sita. Alisema vilevile kuwepo kwa usitahimilivu wa kijamii hapa nchini nayo ni njia mojawapo mhimu kwa Ujenzi wa uchumi unaofanywa na Serikali hii.

MBUNGE WA MSALALA AWATAKA WANANCHI KUCHAGUA VIONGOZI BORA

Mbunge wa Jimbo la Msalala, Iddi Kassim Iddi, ametoa wito kwa wananchi wa jimbo lake kuchagua viongozi bora ambao watakuwa tayari kusikiliza kero za wananchi na kuibua maendeleo katika maeneo yao.  Akizungumza katika Wilaya ya Shinyanga, Mbunge Iddi alisisitiza umuhimu wa wananchi kufanya maamuzi sahihi wakati wa uchaguzi ili kuleta ustawi wa kijamii na kiuchumi kwenye jamii yao. Aidha, alibainisha kuwa maendeleo ya Jimbo la Msalala yanategemea sana ushirikiano kati ya wananchi na viongozi wanaochaguliwa. Viongozi wenye maono na nia ya dhati wataweza kutatua changamoto za wananchi na kusaidia kuboresha maisha yao.