Skip to main content

Posts

Showing posts from July 24, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Dr Charles Mahera Awataka Makatibu wa Afya Mikoa na Halmashauri Kutatua Kero za Watumishi wa Afya

Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Afya Tamisemi Dkt. Charles Mahera amewaelekeza Makatibu wa Afya Mikoa na Halmashauri nchini kufuatilia, kushughulikia na kutatua kero za watumishi wa Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe ili waweze kufanya kazi zao za kuwahudumia wananchi. Kauli hiyo imetolewa kwa niaba yake na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Afya ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe Bi. Subisya Kabuje tarehe 23 Julai, 2024 mkoani Kigoma  wakati akiongea na timu ya usimamizi wa huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe katika ziara ya siku mbili inayoendelea mkoani humo. Amesema watumishi wa Afya ngazi ya vituo vya afya na zahanati wamekuwa na changamoto nyingi ambazo zinawakwamisha katika utekelezaji wa majukumu yao kila siku katika kuwahudumia wananchi hivyo zinapaswa kutatuliwa. Huku akitaja miongoni mwa changamoto hizo ni upandishwaji wa madaraja kwa watumishi wa Sekta ya Afya. Aidha amemtaka Afisa maendeleo ya jamii wa Manispaa ya Kigoma mjini kusimamia kwa ukaribu vikundi vya...

Shamrashamra za Miaka 60 ya JWTZ Zimeanza Baada ya Kuwasili Kwa Meli Vita Tatu Kutoka China

MELI vita tatu za kisasa kutoka Jeshi la Ukombozi la watu wa China,zimewasili katika Bandari ya Dar es Salaam zikiwa na askari na maafisa kadhaa wa jeshi hilo, kwa lengo la kushiriki na kufanya zoezi la pamoja la kivita na jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania JWTZ.  Akipokea meli hizo kwa niaba ya mkuu wa majeshi nchini, Mkuu wa kamandi ya jeshi la wanamaji Tanzania Rear Admiral Ameir Ramadhan, amesema Meli hizo za kijeshi zimekuja  nchini pamoja na mambo mengine zitashiriki kufanya zoezi la pamoja la kivita linajulikana Kwa jina la "AMANI UMOJA"  Kwa kuhusisha Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania  Zoezi Hilo la kivita linakwenda sambamba  na kuelekea kilele cha maadhimisho ya Miaka 60 ya ushirikiano Kati ya Tanzania China,ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ tarehe 01 Septemba 1964. Amesema zoezi hilo lita litashirikisha kamandi zote za JWTZ linatarajiwa kuanza 29 Julai 2024 na kumalizika tarehe 11 Agosti 2024. Amesema  w...