Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Afya Tamisemi Dkt. Charles Mahera amewaelekeza Makatibu wa Afya Mikoa na Halmashauri nchini kufuatilia, kushughulikia na kutatua kero za watumishi wa Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe ili waweze kufanya kazi zao za kuwahudumia wananchi. Kauli hiyo imetolewa kwa niaba yake na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Afya ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe Bi. Subisya Kabuje tarehe 23 Julai, 2024 mkoani Kigoma wakati akiongea na timu ya usimamizi wa huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe katika ziara ya siku mbili inayoendelea mkoani humo. Amesema watumishi wa Afya ngazi ya vituo vya afya na zahanati wamekuwa na changamoto nyingi ambazo zinawakwamisha katika utekelezaji wa majukumu yao kila siku katika kuwahudumia wananchi hivyo zinapaswa kutatuliwa. Huku akitaja miongoni mwa changamoto hizo ni upandishwaji wa madaraja kwa watumishi wa Sekta ya Afya. Aidha amemtaka Afisa maendeleo ya jamii wa Manispaa ya Kigoma mjini kusimamia kwa ukaribu vikundi vya...
Marato tv - Sauti ya Jamii