Mgombea Mteule wa Urais wa Zanzibar kwa Tiketi ya Chama Cha Mapinduzi Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk .Hussein Ali Mwinyi amepokewa na Mamia ya Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi, Viongozi na Wananchi alipowasili Zanzibar akitokea Dodoma alipoteuliwa Kupeperusha Bendera ya Chama hicho katika Uchaguzi Mkuu Ujao katika Mkutano Mkuu Maalum wa CCM Uliofanyika hivi Karibuni. Mgombea Mteule Dk. Mwinyi alipokelewa na Mamia ya Wana CCM, pamoja na Viongozi mbalimbali wa Chama Cha Mapinduzi, Serikali , Vyombo vya ulinzi na usalama na Dini. Mamia ya Wananchi wa Zanzibar na Wana CCM walijitokeza kwa Wingi Pembezoni mwa Barabara kuu ya Uwanja wa Ndege- Kilimani kumpokea Dk ,Mwinyi aliyekuwa katika Gari la Wazi akiwapungia Mkono hadi Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui. Mgombea Mteule wa Urais wa Zanzibar Dk.Hussein Ali Mwinyi alizuru Kaburi la alieyekuwa Rais wa Kwanza wa Zanzibar Hayati Abeid Amani Karume na Kuweka Shada la Maua pamo...
Marato tv - Sauti ya Jamii