📍 Asema watu walimshangaa alipomteuwa kuwa Naibu Waziri 📍Walisema msanii wa Kurap atafanya nini serikalini 📍 Asema MwanaFA ni msaada mkubwa Serikalini 📍Awataka wana-Muheza wamsaidie kumlea katika kazi zake za ubunge 📍 Mwenyewe MwanaFA amshukuru Rais kwa kumrahisishia ubunge wake miaka hii minne 📍 Changamoto zote tatu alizomuomba Rais zapata majibu mazuri Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa watu walikuwa na wasiwasi alipowateua Hamis Mwinjuma kuwa Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, pamoja na Nickson Simon (Nikk wa Pili) kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kibaha. Hata hivyo sasa wamethibitisha kuwa hatua ya kuwateua hakukosea kwa kuwa wamekuwa na msaada mkubwa katika Taifa. Akizungumza leo tarehe 27 Februari, 2025, wilayani Muheza, Mkoani Tanga, Rais Samia amesema: "Nawashukuru sana Muheza kwa kumlea kijana wetu Mwana FA, Mh. Hamisi Mwinjuma, Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, na Mbunge wenu. Kijana huyu anatusaidia sana...
Marato tv - Sauti ya Jamii