📍Aisifu GSM na Rais Hersi kwa kukuza vipaji vya watoto Na Mashaka Mhando Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma (MwanaFA), amemwagia sifa Klabu ya Yanga na Taasisi ya GSM Foundation kwa jitihada zao za kuwekeza katika soka la vijana nchini, akisema hatua hiyo ni mustakabali wa mafanikio ya Taifa katika mchezo wa mpira wa miguu. Mhe. Mwinjuma aliyasema hayo jana alipokuwa Mgeni Rasmi katika ufunguzi wa programu ya "Safari ya Soka" iliyoandaliwa na Klabu ya Yanga kwa kushirikiana na GSM Foundation, tukio lililofanyika katika viwanja vya Gymkhana Club, Dar es Salaam. Akipokelewa na mwenyeji wake, Rais wa Klabu ya Yanga, Injinia Hersi Said, Naibu Waziri huyo alipata fursa ya kushuhudia vijana wadogo wakionyesha umahiri wao uwanjani, jambo ambalo alikiri kuwa limempa matumaini makubwa. "Nimejionea mwenyewe, nchi hii ina 'mafundi' wa soka haswa. Vipaji vipo vingi sana, kinachohitajika ni uangalizi wa karibu na weledi kama huu unaofany...
Marato tv - Sauti ya Jamii