Skip to main content

Posts

Showing posts from July 28, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Majaliwa: Actif 2025 itoe Majibu ya Changamoto za Kibiashara na Uwekezaji

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema kuwa Jukwaa la Nne la Biashara na Uwekezaji kati ya Afrika na Karibiani (ACTIF) linapaswa kuja na majibu ya changamoto za kibiashara na uwekezaji zinazoyakabili mataifa ya Afrika na yale ya eneo la Karibiani. Amesema kuwa changamoto hizo zinapaswa kujadiliwa kwa uwazi na kutaja bayana vikwazo vyote vinavyosababisha kutofanyika kwa biashara kati ya mataifa hayo Ameyasema hayo jana (Jumatatu, Julai 28, 2025) wakati akishiriki mjadala ya Wakuu wa Nchi na Serikali kwenye ufunguzi wa Jukwaa la Nne la Kibiashara na Uwekezaji kati ya Afrika na Karibiani (Afri-Caribbean Trade and Investment Forum-ACTIF 2025) linalofanyika katika kituo cha mikutano cha Radisson jijini St. George’s, nchini Grenada. Mheshimiwa Majaliwa anahudhuria jukwaa hilo kwa niaba ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan. “Mbali ya kujadili changamoto hizo, nchi zetu zinapaswa kutengeneza mazingira mazuri ya kuvutia uwekezaji na kutoa ushirikiano kwa wawekezaji wenye nia ya kuwekeza kwenye mataifa...

Kampeni ya "Badilika, Tokomeza Ukatili"

  Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. Dorothy Gwajima amezindua rasmi kampeni ya 'Badilika, Tokomeza Ukatili' itakayotekelezwa kwa miaka miwili 2025/27 mkoani Kigoma. Akizindua kampeni hiyo iliyoandaliwa na shirika la maendeleo la nchini Ubelgini ENABEL katika uwanja wa Mwanga Centre mkoani Kigoma Jumatatu Julai 28, 2025, Waziri Dkt. Gwajima ametoa wito kwa jamii kubadili tabia, mitazamo na mienendo inayochochea ukatili dhidi ya wanawake na watoto. Amesisitiza kuwa kila mwananchi anapaswa kuwa sehemu ya mabadiliko huku akijiunga mwenyewe kama balozi wa mabadiliko na Kampeni ikilenga kuvuna mabalozi 150,000 katika mkoa huo. Amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeweka msukumo mkubwa katika kutokomeza ukatili kupitia sera madhubuti na mikakati ya kitaifa kama Sera ya Taifa ya Jinsia ya mwaka 2023 na Mpango wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto (MTAKUWWA II). Aidha Waziri Dkt. Gwajima ameli...

Kampeni ya "Badilika, Tokomeza Ukatili"

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. Dorothy Gwajima amezindua rasmi kampeni ya 'Badilika, Tokomeza Ukatili' itakayotekelezwa kwa miaka miwili 2025/27 mkoani Kigoma. Akizindua kampeni hiyo iliyoandaliwa na shirika la maendeleo la nchini Ubelgini ENABEL katika uwanja wa Mwanga Centre mkoani Kigoma Jumatatu Julai 28, 2025, Waziri Dkt. Gwajima ametoa wito kwa jamii kubadili tabia, mitazamo na mienendo inayochochea ukatili dhidi ya wanawake na watoto. Amesisitiza kuwa kila mwananchi anapaswa kuwa sehemu ya mabadiliko huku akijiunga mwenyewe kama balozi wa mabadiliko na Kampeni ikilenga kuvuna mabalozi 150,000 katika mkoa huo. Amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeweka msukumo mkubwa katika kutokomeza ukatili kupitia sera madhubuti na mikakati ya kitaifa kama Sera ya Taifa ya Jinsia ya mwaka 2023 na Mpango wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto (MTAKUWWA II). Aidha Waziri Dkt. Gwajima amelipo...

Waziri Mavunde awasili wilayani Namtumbo maandalizi ya ziara ya Rais Samia

Waziri wa Madini Mh. Anthony Mavunde leo amewasili Wilaya ya Namtumbo,Mkoani Ruvuma kwa ajili ya ukaguzi wa maandalizi ya ziara ya Mh. Rais Dkt. Samia S. Hassan kwenye mradi wa madini ya Urani unaotekelezwa na Kampuni ya Mantra Tanzania Ltd. Tarehe 30.07.2025 Mh. Rais Dkt. Samia S. Hassan atazindua Kiwanda cha Uchenjuaji madini ya Urani na pia atazindua rasmi kuanza kwa ujenzi wa mgodi wa Urani na ujenzi wa Mtambo mkubwa wa kuchenjua madini ya Urani ambao unakadiriwa kuwa gharama ya zaidi ya Tsh 3.06 Trilioni.

Rais Samia aendelea kuongoza Kikao cha Kamati Kuu usiku huu

  Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) chini ya Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kikiendelea usiku huu Jijini Dodoma tarehe 28 Julai, 2025 kupitia na kuchuja mapendekezo ya majina ya wagombea wa Ubunge wa Majimbo, Ujumbe wa Baraza la Wawakilishi, Viti Maalum vya Ubunge na Baraza la Wawakilishi.

Majaliwa Ashiriki Ufunguzi wa Mkutano wa Actif 2025, Grenada

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Julai 28, 2025 ameshiriki katika ufunguzi wa Jukwaa la nne wa Kibiashara na Uwekezaji kati ya Afrika na Karibiani (Afri-Caribbean Trade and Investment Forum - ACTIF 2025) mjini St. George’s, nchini Grenada, Julai 28,2025 ambapo alimwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan. Mkutano huo unaolenga kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi kati ya mataifa ya Afrika na visiwa vya Karibiani umehudhuriwa na Wakuu wa Nchi na Serikali kutoka maeneo hayo.