Skip to main content

Posts

Showing posts from April 5, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Polisi yaokoa vijana 87 kwenye upatu wa mtandaoni

JESHI la Polisi Mkoani, Tanga limefanikiwa kuzima mtandao wa utapeli wa kidijitali na kuwaokoa vijana 87 waliokuwa wamenaswa kwenye mtego wa biashara haramu ya upatu, huku likiwashikilia wasimamizi wawili wa kundi hilo kwa tuhuma za kujipatia mamilioni ya fedha kwa njia ya udanganyifu. Operesheni hiyo kabambe iliyofanywa na Kikosi cha Upelelezi wa Makosa ya Jinai (CID), imefichua madudu ya kampuni inayojiita Champions E-Commerce Education, ambayo imekuwa ikitumia kivuli cha mafunzo ya biashara mtandaoni kuwarubuni vijana kutoa kiasi cha kuanzia Sh600,000 hadi Sh Milioni 4 kwa ahadi ya utajiri wa haraka. Akithibitisha tukio hilo jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, ACP Almachius Mchunguzi, amesema vijana hao walikutwa wakiishi katika mazingira duni wakisubiri "utajiri hewa" huku watuhumiwa Mohammed Hamlima Idrisa (24) na Fidolini Hamisi Rashidi (21) wakiendelea kuratibu mkusanyiko huo haramu. "Vijana hawa waliahidiwa faida kubwa ndani ya muda mfupi baada ya kutoa mamili...

Waziri Mkuu akagua madhara ya moto soko la simu 2000

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Aprili 6, 2026 anakagua madhara yaliyotokana na kuungua kwa soko la wafanyabiashara wadogo la Simu 2000, lililopo Ubungo jijini Dar es Salaam.  Ajali hiyo ya moto katika Soko hilo ilitokea Aprili 4 2026 ambapo inakadiriwa vibanda takribani 500 vya wafanyabiashara wadogo viliteketea kwa moto.

Waziri Mkuu ashiriki Tamasha la Mtoko wa Pasaka, asisitiza Amani

_Atoa pole kwa wafanyabiashara wa Soko la Mawasiliano (Simu 2000) waliopata ajali ya moto_ Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, leo Aprili 5, 2026, ameshiriki Tamasha la Pasaka la Mtoko na Christina Shusho lililofanyika katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam. Akizungumza katika tamasha hilo, Waziri Mkuu amesema kuwa Pasaka ni kipindi muhimu kinachowakumbusha Watanzania kuishi kwa upendo, mshikamano na kudumisha amani katika jamii.  “Amani si kwa ajili ya faida ya Rais wala Serikali, bali ni kwa ajili ya kila mwananchi. Pasipo amani hata shughuli ndogo kama kujitafutia kipato haziwezi kufanyika.” Ameeleza kuwa mnufaika wa kwanza wa amani ni mwananchi mwenyewe, kwani bila utulivu hata shughuli za kiuchumi, kijamii na ibada haziwezi kufanyika ipasavyo. Aidha, amempongeza mwimbaji wa muziki wa Injili, Christina Shusho, kwa kuandaa tamasha hilo kubwa lililovuta maelfu ya waumini, akisema mafanikio yake yanaonesha kuwa lina kibali cha Mungu.  “Ukiona jambo linafanikiwa kia...

CRJE yaungana na Watanzania kuwaenzi mashujaa waliojenga Reli ya TAZARA

Na Mwandishi Wetu Kampuni ya CRJE (East Africa) Ltd imeungana na watanzania jijini Dar es Salaam katika hafla ya kuweka maua katika makaburi ya note kutoka China waliofariki wakati ujenzi wa jengo la Tazara kati ya mwaka 1970 na 1976.  Wafanyakazi wa Kampuni hiyo waliweka maua juu ya makabili ya mazungumzo hao ambao ni zaidi ya 65.  Watu waliohudhuria shughuli hiyo walikumbuka kujitoa kwa hao wakishiriki katika ujenzi wa reli hiyo ambao umeleta mchango mkubwa na unaokumbukwa daima katika mahusiano ya karibu zaidi kwa serikali ya Tanzania na China ambapo Reli hiyo yaZARA imekuwa ni ishara ya urafiki na ushirikiano kati ya nchi mbili hizo. Happy Kiula, wa Kitanzania katika Kampuni hiyo ya CRJE (East Africa) Ltd, alisema: "Tumekuja leo kuwakumbuka mashujaa maisha kutoka China ambao walipoteza wakati wakishiriki katika ujenzi wa reli. Tunaendelea kuwaombea kwa Mungu aendelee kuwaweka mahali pema peponi." Li Yuanhang nchini China, alisema Kampuni hiyo kutoka kwa sehemu ya kampuni ...

Tanzania: CRJE (East Africa) Ltd Pays Homage to TAZARA's Visionaries

  By Prosper Makene  CRJE (East Africa) Ltd joined other Chinese and Tanzanians to pay tribute to the Chinese experts who devoted their lives to the construction of the Tanzania-Zambia Railway (TAZARA). The Qingming memorial activity was a poignant reminder of the sacrifices made by these individuals, who left their homes and families to contribute to the development of Tanzania and the region. The TAZARA Railway, a symbol of China-Tanzania friendship and cooperation, was built in the 1970s to connect Zambia and Tanzania, providing a vital transportation link for landlocked countries in southern Africa. The project was a testament to the strong ties between China and Tanzania, and the Chinese experts who worked tirelessly on the project paid the ultimate price, with many losing their lives in the process. As the team gathered to pay tribute, they were reminded of the history of the TAZARA Railway, a story of cooperation, determination, and sacrifice. The railway was built at a...

Askofu Mulenga apiga marufuku siasa za uchonganishi madhabahuni

  Na Mwandishi Wetu, Tanga ASKOFU Mkuu wa Kanisa la The Free Pentecostal Church of Tanzania (FPCT), Stivie Mulenga, ametoa onyo kali kwa viongozi wa dini nchini kuacha mara moja kutumia majukwaa ya kidini kuhubiri uchonganishi na chuki, badala yake wahubiri amani, upendo, na mshikamano wa kitaifa. Akizungumza katika Ibada Maalum ya Pasaka jijini Tanga, Askofu Mulenga amesisitiza kuwa madhabahu ni mahali patakatifu pa kumtukuza Mungu na siyo jukwaa la mashambulizi ya binafsi, upendeleo, au chuki zinazoweza kuigawa jamii na kuhatarisha usalama wa nchi. "Ni muhimu kwa viongozi wa dini kutambua uzito wa majukwaa waliyonayo. Ibada zinapaswa kubaki kuwa chemchemi ya upendo na uvumilivu. Tunapofanya kinyume chake na kueneza mifarakano, tunasaliti msingi wa imani ya Kikristo ambayo chimbuko lake ni amani aliyoiacha Yesu Kristo," alisisitiza Askofu Mulenga. Uhuru wa Kuabudu na Mmomonyoko wa Maadili Katika mahubiri hayo yaliyosheheni ujumbe wa kizalendo, Askofu Mulenga ameipongeza Seri...