*Kutoka: Dawati la Habari Polisi Mwanza* Chuo cha Polisi Wanamaji Mkoa wa Mwanza kimepokea boti moja ya kisasa aina ya Fiber Speed Boat PB 23 PAPA, ikiwa ni hatua muhimu ya kuimarisha mafunzo kwa vitendo, doria za majini na usalama ndani ya Ziwa Victoria. Boti hiyo ilikabidhiwa rasmi tarehe 2 Februari, 2026, baada ya kubadilishiwa matumizi kutoka Makao Makuu ya Kikosi cha Polisi Wanamaji Dar es Salaam, kufuatia uamuzi wa Mkuu wa Jeshi la Polisi wa kusogeza vitendea kazi karibu na maeneo ya utekelezaji wa majukumu. Akikabidhi boti hiyo kwa Mkuu wa Chuo cha Polisi Wanamaji Mwanza, SACP Ndagile Makubi, Mkuu wa Kikosi cha Polisi Wanamaji Tanzania, SACP Moshi Sokoro, alisema uhamisho wa boti hiyo unalenga kuongeza ufanisi wa mafunzo kwa wanafunzi wanaopata mafunzo chuoni hapo, hususan mafunzo ya uokoaji majini, doria, na operesheni maalum. SACP Sokoro alibainisha kuwa kwa muda mrefu chuo na kikosi cha Polisi Wanamaji vilikabiliwa na changamoto ya uhaba wa vitendea kazi vya kufundishia kwa v...